Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

Hon. Eng. Christopher Kajoro Chizza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

MHE. ENG. CHRISTOPHER K. CHIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nami naomba niipongeze Serikali kwa kuleta maazimio haya. Kwanza hata mimi naona tumechelewa, tungeanza jana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba moja kwa moja niipongeze Serikali kwa kufanya mabadiliko katika kanuni zile za matumizi salama ya bioteknolojia. Kwa wale ambao walikuwa wanafuatilia kwa jambo hili, jambo hili la Strict liability, hiki kipengele kwa muda mrefu kimekuwa kikwazo kikubwa sana kwa watafiti wetu katika nchi hii. Maana mtatiti anapoona kwamba yeye akifanya utafiti halafu yeye mwenyewe tena anakamatwa, anashikiliwa, anaadhibiwa kwa utatiti ambao ameufanya, basi amekuwa anakosa nguvu ya kuendelea na utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Ibara hii ya 12 ambayo Mheshimiwa Waziri wa Mazingira ameileta, kwa kweli naona imeleta ahueni na motisha kwa watafiti wetu kuendelea sasa kujikita kwenye utafiti. (Makofi)

Mwenyekiti Mwenyekiti, mbegu bora, mbegu zenye ukinzani na magonjwa, mbegu ambazo zinazalisha, zinaleta tija katika uzalishaji ndizo tunazozitaka. Tukijifanya sisi hatutaki kufanya utafiti, tutaendelea kutumia tafiti ambazo wenzetu wamefanya uko nje ambazo haziendani na ekolojia ya nchi yetu. Kwa hiyo, tusiogope kufanya utafiti katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hiyo, nashauri tuache kabisa tabia ya kutotenga fedha za utafiti. Nakumbuka kabisa mwaka 2003 nchi yetu tulikubaliana, tuliridhia pamoja na ile nchi za SADC katika Azimio la Maputo, pamoja na nchi za AU kwamba nchi zetu zitenge kila moja asilimia kumi ya bajeti zake kwenda kwenye kilimo. Nasi tukajiongeza kwamba katika hiyo, asilimia moja iende kwenye utafiti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina uhakika jambo hili tumelifanya kwa wakati gani, lakini kama tumechelewa, basi huu ndiyo wakati sasa tuanze kutenga fedha hizi, watafiti wetu wafanye kazi vizuri kwa uhuru, wapate motisha ili angalau waweze kutupeleka mbele sasa katika kutafiti mbegu za mimea ili tuweze kuongeza tija katika uzalishaji hasa wakati huu ambao tutahitaji zaidi kuzalisha malighafi za kilimo kwa ajili ya viwanda vyetu vya kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe ushauri, tunapokwenda kwenye utafiti huu, tunazungumza pia hakimiliki za kulinda wagunduzi. Amesema vizuri Mheshimiwa Dkt. Ishengoma, watafiti hawa hawafanyi kazi peke yao, wanafanya kazi na wakulima. Baadhi ya watu watakaoathirika na matokeo ya utafiti yakiwa ni hasi au chanya, ni wakulima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, napendekeza tuweke utaratibu, tukitenga fedha za utafiti, tutenge fedha za kutosha za kutoa elimu kwa wagunduzi, wafanyabiashara wa mbegu pamoja na wakulima wetu ikiwa ni pamoja na kuwafundisha wakulima wetu wajue haki zao ni zipi nao wanalindwaje wakati wanapopata matatizo yanayotokana na matokeo hasi yanayotokana na utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono maazimio haya kwa asilimia mia kwa mia. Ahsante. (Makofi)