Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuchangia kuhusiana na Azimio hili la Mkataba wa Marrakesh.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tarehe 14 Novemba, 2017, niliuliza swali ambalo lilihusu Mkataba huu wa Marrakesh. Katika majibu yao, Serikali waliahidi kulifanyia kazi na kulileta hapa ili mkataba huu uweze kuwasaidia watu wenye ulemavu wa kutoona. Kipekee kabisa naishukuru Serikali imeonesha wa vitendo kwamba kile walichokiahidi wamekifanyia kazi. Nakupongeza sana Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana pamoja na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jitihada hizi ambazo kwa kweli zinaleta faraja kubwa sana kwa watu wenye ulemavu pamoja na Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Marrakesh? Marrakesh ni kwa sababu mkutano huu ulifanyika nchini Morocco katika Mji wa Marrakesh na nchi 20 zikaridhia Azimio hili ambapo katika mkataba huo waliridhia kuhusiana na kuweza kuruhusu vitabu mbalimbali viweze kutafsiriwa kwa kuchapishwa katika maandishi ambayo yatawasaidia wenzetu wenye uono hafifu na wale wasioona. Kwa kweli kama ambavyo wengine wamesema, Serikali imefanyia kazi jambo hili haraka sana na tunawashukuru kwa hilo kwa sababu wanafunzi wengi waliokuwa wakisoma katika vyuo vikuu walikuwa wakilazimika kutafsiriwa na wakati mwingine kutafsiriwa huwezi jua nini ambacho wakati mwingine kimekosekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa mkataba huu watu wasioona utaweza kuwasaidia kwa mapana zaidi ili basi maandishi mbalimbali iwe kwenye michoro, vitabu au kwa lugha nyingine zozote zile uweze kutafsiriwa na kuwasaidia kupata elimu. Elimu ndiyo kila kitu na hasa kwa watu wenye ulemavu elimu ndiyo mtaji wake. Kwa hiyo, naipongeza sana Serikali kwa kuleta Mkataba huu wa Marrakesh ili basi watu hawa waweze kufaidika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu tunafahamu kabisa kwamba hapa nchini kwetu haki ya kupata taarifa hasa kwa watu wenye ulemavu wa kutoona ilikuwa ni shida hapo awali. Kwa hivi sasa, kwa Serikali hii ya Awamu ya Tano tunaona kabisa Mheshimiwa Rais amekuwa na jitihada kubwa. Kwa hiyo, Baraza la Mawaziri pia na kwa kuwa tayari katika Baraza hilo la Mawaziri tunaye pia mtu ambaye anatuwakilisha, tunaona sasa haya yote yakifanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa kweli Awamu hii ya Tano imekuwa na jicho la ziada katika kuhakikisha kwamba hakuna anayeachwa nyuma wakiwemo watu wenye ulamavu. Ni pongezi za pekee kwa kweli nazitoa kwa Mheshimiwa Rais pamoja na Baraza la Mawaziri na Serikali yote kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika kutafsiri huku wakati mwingine wako wengine ambao watataka kujinufaisha. Naomba Serikali iwe makini kuhakikisha kwamba kile ambacho kimekubaliwa basi watu wenye ulemavu wa kutoona waweze kusaidiwa kwa haki na vile vingine ambavyo havitokuwa na manufaa basi sheria iweze kufuata mkondo wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Sheria ya Hakimiliki ambayo iko chini ya COSOTA tuone sasa kwamba sasa ni kwa jinsi gani iendane na mkataba huu wa Marrakesh; na yenyewe pia tuna haja na kila sababu ya kuweza kubadilisha vile ambavyo vinahitaji viingie huko na kusiwepo na kipingamizi chochote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwakweli kutokana na hili lililofanyika, langu kubwa ni pongezi lakini pia kuona kwamba sasa wakati huu tunapokwenda tuone na mikataba mingine ambayo kwa namna moja au nyingine bado imeachwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante.