Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya pamoja ya ziada ya Nagoya – Kuala Lumpur kuhusu Uwajibikaji Kisheria na Fidia kwa Madhara yanayoweza kutokea kutokana na matumizi ya Bioteknolojia ya Kisasa katika Kutekeleza Itifaki ya Cartagena (Nagoya – Kuala Lumpur Supplementary Protocol on Liability and Redress on Cartagena Protocol on Biosafety) pamoja na Azimio la Kuridhia Itifaki ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika kuhusu Kulinda Haki Miliki za Wagunduzi wa aina mpya za Mbegu za Mimea. (Protocal for Protection of New Varieties of Plants (Plant Breeder’s Rights) in The Southern African Development Community – SADC) pamoja na Azimio la Kuridhia Mkataba wa Marrakesh wa mwaka 2013 unaowezesha upatikanaji wa kazi zilizochapishwa kwa watu wasioona, wenye uoni hafifu au ulemavu unaomfanya mtu kushindwa kusoma (The Marrakesh Treaty to Facilitate Access to Published Work For Persons Who Are Blind, Visually Impaired or Otherwise Print Disabled)

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia. Leo nimeamua tu nichangie niweze kuongea na Waheshimiwa Wabunge wenzangu kwa maana ya kukumbushana majukumu yetu. Ukiangalia trend ya michango yetu sisi wote humu ndani kama Wabunge kuanzia jana pamoja na leo na hotuba zetu sisi za Kambi jana pamoja na leo tumeamua kuunga mkono moja kwa moja Maazimio haya yaliyoletwa mbele hapa na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo makusudi ili kuweza kuwakumbusha wenzetu kwamba jukumu letu la Kibunge la kwanza kabisa ni pamoja na kutunga sheria. Suala la pili ambalo ni majukumu yetu pia ni kusimamia na kuishauri Serikali katika kutekeleza mipango mbalimbali. Tukifika kwenye hiyo juncture wote tukajua majukumu yetu kimsingi hatuwezi kuvutana kwenye haya mambo yanayojitokeza humu ndani na kuharibu atmosphere ya Bunge wakati fulani kwa sababu tunakaa na kusikilizana. Kwa hiyo, hali ya hewa inakuwa nzuri kabisa kama ambavyo mmeona imetokea jana na leo pia ilivyotokea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nachotaka nikiseme ni kwamba haya Maazimio ambayo yamekuja mbele ya Bunge lako Tukufu, wote tunaungana mkono kusema kwamba yameletwa ndani ya Bunge hili kwa kuchelewa. Yangekuja mapema sana shida tunazozipata huko Majimboni kwetu, kwa mfano, mimi natokea Wilaya ya Masasi ambapo tuna Shule ya Msingi ya Masasi ambapo mimi nilisoma pale darasa la pili mpaka darasa la tano. Pale ndani tuna walemavu wa macho na vijana wenye uoni hafifu, wanavaa miwani lakini bado hawawezi kuona, wanatumia haya maandishi ya nukta nundu. Kipindi cha nyuma walikuwa wanatumia Braille ambazo ziko kama rula, wanachoma kwa vidoti wanaendelea, baadaye waka- improve wakaweka pale mashine, mashine zile kule ndani zimechakaa kabisa na haziwezi kuwasaidia, vijana wapya wanaoingia pale wanashindwa kupata hizi mashine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Ikupa alinisaidia na Mwalimu Kamtande alisema nikushukuru kwa sababu niliweza kupata kwa kufuatilia Serikalini mashine ya kuchapa kwa kutumia nukta nundu. Suala linalokuja na matatizo tunayoyapata, tumempelekea pale mwalimu ambaye ni mwajiriwa kabisa wa Serikali anafundisha shule ya Msingi Chibugu, bahati mbaya sana lakini kutokana na pesa anazozipata hawezi tena kutumia mshahara wake kwa ajili ya kwenda kununua karatasi maalum kwa ajili ya kwenda kuchapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapoingiza hii teknolojia mpya tunataka sasa nukta nundu zianze kutumika maalum kabisa na Serikali imeiridhia tuone na namna ya kuongeza bajeti. Bahati mbaya sana jambo limekuja baada ya bajeti kuu kupitishwa. Sina uhakika kama Wizara kuna fungu ambalo wamelitenga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo limenipa mshangao, mimi ni Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara na jambo hili limewasilishwa pale na Waziri wangu wa Viwanda na Biashara, hivi kuna mahusiano gani kati ya nukta nundu na Waziri wa Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani hili jambo lingekwenda kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ajili ya kulisimamia vizuri upande unaoshughulika na masuala ya walemavu na wengine, kwa mfano Wizara anayosimamia Mheshimiwa Ikupa hapa lingekuwa na maana zaidi labda na bajeti yake pale ingekwenda vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tumesema tunaunga mkono Azimio hili, hatuna pingamizi lolote. Hata mawazo mazuri yatakayoletwa na Serikali hapa kwa kusikilizana yakianzia kwenye Kamati zetu za mtambuka na baadaye yakaja ndani ya Bunge, wote tukaona tuna nia moja ya kujenga nchi yetu, Taifa letu liweze kuongea kwa lugha moja tunaweza tukafika sehemu nzuri kushauriana kwa kusikilizana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina mengi ya kusema, nilitaka niseme tu hayo machache niwaambie kuna haja ya kuridhiana na kuweza kwenda pamoja. Ahsante sana. (Makofi)