Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

Hon. George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwanza kuwashukuru sana Mwenyekiti wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira Mheshimiwa Sadiki Muradi pamoja na Makamu Mwenyekiti Kanali Mstaafu Masoud Ali Khamis pamoja na Wajumbe wote wa Kamati ya Viwanda, Biashara na Mazingira kwa umoja wao na kwa ushirikiano pamoja kuwa na Serikali katika kuhakikisha kwamba azimio hili linafikia hatua hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nishukuru sana Msemaji wa Kambi ya Upinzani Mheshimiwa Cecil Mwambe kwa kutoa maoni mazuri ambayo kimsingi kwa pande zote mbili Kamati pamoja na Upinzani wameunga mkono hoja hii. Pia niwashukuru wachangiaji wengine wote waliozungumza na wale walioandika kimsingi hakuna hata mmoja aliyepinga azimio la matumizi ya zebaki yaani The Minamata Convention on Mercury.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwa pongezi hizi na na kwa kuwa hakuna aliyepinga nataka nisema kwa ujumla wake tu kwamba mengi yaliyosemwa yamelenga zaidi katika kuonesha namna gani sasa kama tumeshakubaliana kwamba zebaki ni kitu kibaya, kina madhara kwa binadamu kwa afya ya binadamu na mazingira. Pia yako madhara ambayo yanaonekana na yanatokea na tunayafahamu na mifano tunaijua. Lakini pia liko kundi la wachimbaji wadogo ambao wao wanaathirika moja kwa moja kwa sababu wanaichezea zebaki kwa kuishika kwa mikono hapa tuna kazi ya kufanya na ndio maana Jumuiya ya Kimataifa na dunia imeona ikae na kuja na mapendekezo ya makubaliano haya ambayo leo tumeyaridhia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi suala la zebaki ni suala gumu kwa sababu viko vitu ambavyo hatuna namna bado tunahitajika kutumika kutumia zebaki kwa sababu ya aina ya teknolojia ambazo bado tunazihitaji kwa ajili ya huduma, kwa ajili ya matibabu, kwa ajili ya mila na kwa ajili ya baadhi ya utengenezaji wa vitu vingine ambavyo tunavihitaji. Na teknolojia mbadala wa vitu hivyo haujapatikana, kwa hiyo itatutuchukua muda kidogo na ndio maana hata katika kuridhia na hata azimio lenyewe linazungumzia juu ya kuondokana na matumizi ya mercury kidogo kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ifikapo kwa 2030 kusudia la mkataba huu ni kuhakikisha kwamba tuwe tumeondoka kabisa, sasa haya ni malengo na kimsingi the legal status ya convention hizi za Kimataifa huwa sio kwamba unapokuwa haujafikia level unaadhibiwa, lakini kutoingia na kukubali na kuridhia mikataba kama hii unaweza ukakosa faida za kushirikiana na wenzako duniani katika kuondokana na jambo ambalo si zuri kama ilivyo zebaki.

Kwa hiyo, kimsingi mimi nikubaliane na Wabunge wote na niseme tu kwamba Serikali imejipanga chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais kuhakikisha kwamba tunakuwa na mpango mkakati wa kutekeleza azimio hili na tumekwishaanza maandalizi ya mpango mkakati huo na ifikapo mwezi ujao tutakuwa tayari tumeukamilisha mpango mkakati ambao utakuwa na majibu ya hoja nyingi sana zilizoulizwa na Waheshimiwa Wajumbe namna ambavyo tutaweza kuondokana na matumizi ya zebaki kwa sababu ya ubaya ambao wote tumedhihirisha hapa kwamba ni kitu kibaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kuomba na kusihi Waheshimiwa Wajumbe wakubaliane na maoni haya yaliyotolewa na watu wote pia msimamo wa Serikali katika kuamua kuridhia azimio hili ili tuwe pamoja na dunia tusiweze kukosa fursa nyingine za ushirikiano wa kusaidia na wenzetu duniani katika kuondokana na matumizi ya zebaki ambayo ni mbaya kwa afya ya binadamu lakini pia kwa mazingira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie kwa kumshukuru Naibu Waziri Mheshimiwa Mussa kwa kushirikiana na mimi na kunisaidia na hata tumeweza kulifikisha azimio hili mahala hapa na kwa kumalizia nichukue nafasi hii kukuomba wasihi Waheshimiwa Wajumbe na Wabunge wote waweze kuridhia azimio hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja. (Makofi)