Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

Hon. Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba Kigosi Kuwa Hifadhi ya Taifa Kigosi pamoja na Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji wa Hadhi Sehemu ya Eneo la Pori la Akiba la Igalla Kuwa Hifadhi ya Taifa ya Mto Ugalla pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Minamata kuhusu Zebaki (Minamata Convention on Mercury)

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi niweze kutoa mchango wangu tunapoelekea katika kuazimia azimio hili la Minamata Convention.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa bila kupoteza muda naipongeza Serikali kwa kuleta azimio hili ndani ya Bunge. Ukiangalia umuhimu mkubwa wa kuridhia Azimio la Minamata; Minamata kwanza yenyewe kama jina la convention yenyewe imetokana na madhara ambayo yaliwapata nchi ya Japan katika hilo eneo ambalo linaitwa Minamata. Madhara ambayo yalitokana na disposal ya hii sumu ya zebaki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muhimu sasa nchi kama Tanzania na sisi kuweza kuridhia mkataba huu kwa ajili ya kuweza kulinda afya za wananchi hususan wachimbaji wadogowadogo katika migodi ya dhahabu ambao ndio watumiaji wakubwa sana wa zebaki katika uchenjuaji wa dhahabu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona wananchi wengi sana hususan Kanda ya Ziwa ambako ndio kumezungukwa na migodi mingi wakipata athari za sumu inayotokana na zebaki kwa ajili ya kuchenjua dhahabu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi natokea Kanda ya Ziwa, kule kina mama wanajifungua watoto wenye vichwa vikubwa, kule ndio tunaongoza kwa tatizo hilo. Hatujaishia hapo, kule Kanda ya Ziwa wakina mama ndio wanaongoza kwa kupata watoto ambao wanakuwa na ulemavu wa viungo mbalimbali kwenye mwili. Kwa hiyo, ukiangalia ukubwa wa tatizo hili ni jambo zuri sana Serikali imeona kwamba ilete azimio hili ili sisi kama Bunge tuweze kuliridhia na hatimaye kupata faida mbalimbali katika kuridhia mkataba huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nchi Tanzania tutapata faida zipi, moja; tutapata faida ya kwamba tunaweza tukapata mbadala wa matumizi ya zebaki. Kama tumeona kwamba zebaki ina matatizo ambayo yanasababisha matatizo ya kiafya kwa wananchi hususan hawa wachimbaji wadogo wadogo, ina maana kama nchi tunaporidhia mkataba huu, tutapata faida ya kupata mbadala wa matumizi ya zebaki, kwanza kwa sababu katika nchi zote ambazo zimeridhia mkataba huu kutakuwa na mambo matatu ambayo yatafanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kwanza, ni kuweza kupunguza matumizi ya zebaki katika kuchenjua dhahabu kwenye migodi. Lakini kitu kingine ni kwamba ni nchi zote ambazo zimeridhia mkataba huu zitazuiwa kuchimba hii zebaki. Sasa kama zile nchi ambazo zinachimba zebaki zitazuiliwa sisi kama Tanzania tusiporidhia mkataba huu tutajipanga vipi kupata matumizi mbadala ya zebaki kama zebaki itakuwa imezuiliwa. Kwa hiyo, utaona ni vizuri kama nchi tukaridhia mkataba huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nina jambo moja la kushauri Serikali pamoja na kwamba tunaenda kuridhia mkataba huu ninaomba wazingatie article 18 ambayo inazitaka nchi zilizoridhia Mkataba huu kutoa elimu kwa watumiaji wa zebaki, lakini pia kuhakikisha kwamba inawasaidia wananchi kufahamu ni madhara gani wanayapata katika utumiaji wa zebaki. Naomba Serikali iweke mpango mkakati wa kuhakikisha kwamba wanatoa elimu kwa wananchi ambao wanaathirika na zebaki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia naiomba Serikali izingatie article 16 ambayo inazitaka nchi ambazo zimeridhia huu mkataba kuhakikisha wanatoa huduma bora za kiafya kwa zile sehemu/yale maeneo ambayo wameathirika na matumizi ya zebaki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa hiyo naomba Serikali waweke mpango mkakati kuhakikisha kwamba yale maeneo ambayo yameathirika kutokana na matumizi ya zebaki wanapata huduma bora za kiafya ili kuweza kuwasaidia wananchi ambao tayari wamekwisha kuathirika, lakini pia ninaiomba Serikali kuzingatia ushauri huu katika mkataba huu wa zebaki umeweka kipengele ambacho kipo katika article 26 ambayo inazitaka nchi kuomba waweze kufanya amendment katika mkataba huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tusijifunge, katika mkataba huu matumizi yamewekwa kwamba kuacha kutumia ndani ya miaka kumi na tano, kwa hiyo naomba Serikali izingatie article 26 ili waweze kufanya amendment kupunguza muda wa matumizi ya zebaki ili kuweza kuwaokoa wananchi wetu. Ahsante na ninaunga mkono hoja. (Makofi)