Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya eneo la Pori la Akiba la Selous kuwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere

Hon. Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Mapendekezo ya Ubadilishaji Hadhi Sehemu ya eneo la Pori la Akiba la Selous kuwa Hifadhi ya Taifa ya Nyerere

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nami niungane na wenzangu kuunga mkono azimio lililo mbele yetu, ila niendelee kuishauri Serikali katika hili kwamba, eneo hili sisi tunapendekeza lote eneo la Selous liwe Nyerere Conservation Area. Kwa nini tunapendekeza eneo lote liwe conservation area; ni kwa sababu hili eneo tutalilinda lote na hatutaligawa ikawa sehemu moja tunaithamini zaidi nyingine tunaidharau, lakini pia tutaifanya Serikali iweze kuwekeza miundombinu na kuwahamasisha wawekezaji kuja kuwekeza mle ndani ili pato la Taifa liwe kubwa zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kuigawa vipande vipande utakichukua kipande kimoja utakithamini zaidi na kingine utakichukua kama ni cha kwako tu. Kwa hiyo, tunapendekeza hii Selous iwe Nyerere Conservation Area yote na isiwe vipande vipande, ili uhifadhi uwepo zaidi, lakini tuweze kuiendeleza zaidi kwa maana ya kwamba, tuone faida na pato la Taifa linakua.

Mheshimiwa Spika, napendekeza vilevile kama tunalipa jina la Nyerere basi tusimkate, Mwalimu alikuwa na heshima yake kubwa sana hapa Tanzania, Afrika na duniani kote, kwa nini tusiliite Mwalimu Nyerere Conservation Area? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, neno Mwalimu linaleta heshima na hadhi yake kwa Baba wa Taifa. Kwa hiyo, tusikate tu ikawa Nyerere, nadhani itakuwa, kwa mimi nahisi kama kutakuwa kuna mapungufu fulani hivi katika kumpa ile heshima ambayo amekusudiwa kupewa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la tatu ambalo nataka kuchangia ni suala la marketing. Tunapoipa jina la Mwalimu Nyerere Conservation Area au Mwalimu Nyerere National Park, whatever na inatoka kutoka Selous wakati duniani Selous ni worldwide inajulikana itabidi hapo Wizara isimame vizuri sana kufanya suala la marketing kwamba unapoisema hii Mwalimu Nyerere Conservation Area au Mwalimu Nyerere National Park wale wageni kule au wanaokuja kutembelea waelewe kwamba ni ileile Selous na imebadilishwa jina tu.

Sasa hiyo kazi ya marketing kubadilisha inachukua muda kidogo; nafahamu ugumu wa marketing katika biashara hii ya utalii. Kwa hiyo, lazima Serikali iwe makini sana katika kulipeleka suala hili huko kuiuza hiyo Selous.

Mheshimiwa Spika, la mwisho Mheshimiwa Waziri wakati mnabeba jukumu hili la kubadilisha Selou kutoka kuwa pori la akiba na kuifanya kuwa national park na sisi tunapendekeza kwamba liwe conservation area basi tulikuwa tunaomba ile miundombinu kama ambavyo ameeleza Mbunge anayetoka katika mikoa hiyo kwamba, ile miundombinu mle iboreshwe. Utakapoboresha ile miundombinu mle na ukafanya vilevile marketing kuwahamasisha wawekezaji kuja kuwekeza mle ndani basi, lile suala zima la kuhifadhi lile eneo na lile suala zima la kwamba tunataka kuikusudia kuitangaza hii Stiegler’s ambayo inajengwa pale itakuwa imepata maana kamili maana wawekezaji watakapoongezeka mle ndani baada ya kuboreshwa kwa miundombinu maana yake ni kwamba, pato la Taifa litaongezeka na uhifadhi utaongezeka zaidi kuliko kuacha tu sehemu ikawa inahifadhiwa na sehemu ikaachwa kuwa nini.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunapendekeza iwe Mwalimu Nyerere Conservation Area eneo lote la Selous badala ya kuchukua kipande tu. Hii tunapendekeza sana kitaalamu Mheshimiwa Waziri na tunaomba Serikali ikae ilifikirie hili na hili eneo tusiligawe vipandevipande itakuwa tunaliharibu ule uasilia wake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukumbuke kwamba Selous ni worldwide, kwa hiyo, tukiigawa tunaanza kuipotezea ile heshima yake. Jina kubadilika tu sio tatizo, lakini ile heshima ya Selous ibaki kama ilivyo na tunapendekeza iwe Mwalimu Nyerere Conservation Area, ili iweze kukidhi mahitaji na matakwa ya dunia, lakini mahitaji na matakwa yetu na pato la Taifa liongezeke. Nakushukuru. (Makofi)