Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kufuta Hasara itokanayo na Maduhuli ya Madeni ya Nyuma ya Ada na Leseni za Magari, Riba na Adhabu kwa kipindi kinachoishia tarehe 30 Juni, 2019

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kufuta Hasara itokanayo na Maduhuli ya Madeni ya Nyuma ya Ada na Leseni za Magari, Riba na Adhabu kwa kipindi kinachoishia tarehe 30 Juni, 2019

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikushukuru wewe binafsi kwa kuendesha mjadala huu vizuri, lakini pia niwashukuru Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati ya PAC. Lakini pia Mheshimwa Ernest Silinde aliyetoa Maoni ya Kambi ya Upinzani Bungeni, lakini vilevile Mheshimiwa Allan Kiula, Mheshimiwa Godbless Lema, Mheshimiwa Richard Ndassa, Mheshimiwa Naghenjwa Kaboyoka kwa mara nyingine na Mheshimiwa Stanslaus Mabula. Lakini pia wale ambao wametoa miongozo mbalimbali kama sehemu ya mjadala.

Mheshimiwa Naibu Spika, basi na mimi baada ya shukrani hizo naomba nihitimishe kwanza kwa kutoa ufafanuzi kidogo. Ilihojiwa hapa kwamba mapato yasiyokusanywa basi nayo yahesabike kama hasara, hili sio sahihi. Kwa mujibu wa Kanuni namba 17 ya Kanuni za Fedha za Umma ya mwaka 2001 upotevu au hasara upo wa aina kama nne. Kwanza kuna hasara ya fedha taslimu yaani cash losses, lakini kuna hasara ya vifaa (store losses), kuna hasara kutokana na misamaha yaani waivers and or abandonment. Lakini pia kuna hasara kutokana na matumizi yasiyo na faida au tija kiingereza inaitwa nugatory payments.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa kanuni hii kodi au mapato yasiyokusanywa sio sehemu ya hasara inayotambuliwa kisheria, lakini labda nilieleze kwa lugha nyepesi kidogo. Kwa mfano kama mwezi uliopita nilipanga niuze ngo’mbe wangu wawili ili nifyatue matofali 1000; nikaenda na wale ng’ombe wawili mnadani nikafanikiwa kuuza mmoja tu nikapata fedha za kutosha kufyatua matofali 500 badala ya matofali 1000 niliyolenga, sasa huwezi kuhesabu hiyo kwamba yule ni hasara kwa kuwa nilipoenda sokoni nilitamani niuze wawili nikauza mmoja. Kwa hiyo kwa kweli sio hasara by definition kwa mujibu wakanuni tulizojiwekea, lakini hata katika logic ya kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, ilitolewa hoja hapa kwamba matumizi ya Serikali yanafanyika kinyume na zile ambazo zilipitishwa na Bunge. Hili sio sawa mapato ya Serikali yanakusanywa kwa mujibu wa sheria, sheria zilizotungwa na Bunge, Kodi ya Mapato, VAT, Local Government Finances Act na kadhalika. Lakini pia kila mwaka tunaleta hapa Sheria ya Fedha, huo ndio msingi wa kukusanya mapato ya Serikali na matumizi ya Serikali Waheshimiwa Wabunge yanafanyika kwa mujibu wa Appropriation Act ambayo nayo inakuja hapa Bungeni na sio tofauti na hii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nieleze tu kwamba ambacho Serikali inaweza kufanya ni reallocation (kufanya uhamisho) na huu umeelekezwa kwenye Sheria ya Bajeti Cap. 439 na inasema wazi katika kifungu cha 41(1) imeeleza Afisa Masuhuli akipata ridhaa ya Waziri muhusika anaweza kuhamisha fedha. Lakini pia kifungu cha 41(2) kinaweka mazingira matano ambapo Accounting Officer hawezi kufanya uhamisho wa fedha. Kifungu cha 41(3) kinaweka pia mzingira ambayo Accounting Officer kuhamisha fedha baina ya program au kati ya ndani ya vifungu katika mwaka unaohusika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kifungu cha 44(4) kinanipa Waziri mamlaka ya kuruhusu uhamisho wa fedha kupitia kanuni na kifungu cha 41(5) kinaweka mazingira ambayo mamlaka ya Waziri kufanya uhamisho wa fedha yamezuiliwa/yamekatazwa lakini siyo hiyotunaleta pia reallocation warrants hapa mbele ya Bunge lako tukufu kila mwaka hapa Bungeni. Kwa hiyo, madai kwamba Serikali inafanya matumizi nje ya fedha zilizoridhiwa na Bunge sio sahihi hata kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, labda nieleze tena, Mheshimiwa Lema alikuwa na wasiwasi kwamba fedha hizi ni nyingi labda zinakwenda kwenye uchaguzi, sio kweli, fedha hizi kweli ni nyingi lakini kwamba zinakwenda kwenye uchaguzi hapana.

Mheshimwia Mwenyekiti wa Kamati ya PAC ameeleza kabisa vizuri dhana kwa nini ni lazima Serikali ije kuomba msamaha huu kwamba Bunge liridhie kufuta hiki ambacho tumekuja kukiomba leo. Lakini niseme hivi taarifa ambayo CAG alikagua ina kurasa 8,503; lakini magari pia yanayohusika ni magari ambayo ni ya kipindi kirefu kwa kipindi ambacho sheria inatumika mpaka pale tulipokuja kama Serikali kulieleza Bunge lako tukufu kwamba tunayafuta ambayo ni with effect from tarehe 1 Julai, 2017. Kwa hiyo ndio sababu kwamba kwa nini imechukua muda mrefu, lakini pia ni utaratibu wa kawaida kabisa. Kwa hiyo, ni shutuma za uongo kabisa hatupeleki fedha hizi kwenye uchaguzi hata kidogo na kama ambavyo imeelezwa jamani jipangeni, CCM imejipanga katika kugharamia uchaguzi wake. Sasa na ninyi jipangeni, haya madeni ni cumulative ya kipindi kirefu sana. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Rudia hatujasikia.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, aaah, nimesema hivi CCM imejipanga kikamilifu kwa ajili ya uchaguzi wa mwezi Oktoba, na hawa rafiki zetu wajipange.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mwenyekiti wa Kamati ya PAC alieleza vizuri, tunafuata utaratibu huu ili kuondoa hoja za ukaguzi ambazo zimekaa muda mrefu, lakini vilevile kurekebisha vitabu, lakini ni nafasi pia ya kupokea ushauri wa Bunge imeelezwa vizuri sio suala la kuja kugharamia uchaguzi hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Mabula ametukumbusha kwamba hatua hii imeletwa kwa sababu ilikuwa ni kero kubwa kwa wananchi wetu na lilishangiliwa sana, lakini pia tunataka kusafisha vitabu kama alivyoeleza kwa ajili ya hizi hoja. Sasa hoja za muda mrefu kwenye Halmashauri ni ahidi Bunge lako tukufu kwamba tunaendelea kuzifanyia kazi tukishakamilisha basi zitakuja kwa ajili ya kuomba ridhaa ya Bunge kwa kupitia utaratibu wa kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maelezo hayo naomba kutoa hoja. (Makofi)

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki. (Makofi)