Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kufuta Hasara itokanayo na Maduhuli ya Madeni ya Nyuma ya Ada na Leseni za Magari, Riba na Adhabu kwa kipindi kinachoishia tarehe 30 Juni, 2019

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kufuta Hasara itokanayo na Maduhuli ya Madeni ya Nyuma ya Ada na Leseni za Magari, Riba na Adhabu kwa kipindi kinachoishia tarehe 30 Juni, 2019

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja hii iliyopo mbele yetu. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya PAC na hoja hii ililetwa na Waziri tukaijadili na leo tumeleta wasilisho letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukifuatilia tutakumbuka kwamba, katika Hotuba ya Bajeti ya Mwaka 2017/2018, Bunge ndio pendekezo hili lilikuja na tukalipitisha kwamba, hiyo ada ya mwaka ifutwe, madeni, malimbikizo yote yafutwe na tulipiga makofi sana hapa. Ni kweli, ilionekana kwamba, ada hiyo inaleta kero, tulikubaliana, lakini kiutaratibu sasa wenzetu wale wa TRA hawawezi kufuta bila Bunge kuridhia na vitabu vyao vimeendelea kuwa na hesabu hiyo. Kwa hiyo, leo ni hitimisho tu la uamuzi ambao tuliupitisha wakati huo. Jambo lingine kubwa ni kwamba TRA watasafisha mahesabu yao na kumbukumbu zitakuwa sahihi, kwa hiyo utengenezaji wa mahesabu utakwenda na utakuwa umekaa sawa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimeshangaa kidogo kusikia Kambi ya Upinzani kuleta hoja kwamba mjadala haukufanyika, Kamati ni Bunge dogo, kwa hiyo kule kwenye Kamati tulikojadili sisi tulijadili kwa niaba yenu. Mjumbe pia anaruhusiwa kuhudhuria kwa nini hakuja kule siku ile? Halafu jambo la pili amesema kiwango kinaleta mashaka CAG tunafanya kazi kufuata takwimu tunazoletewa na CAG na CAG alileta kuthibitisha jambo hili. (Makofi)

Sasa kama jambo limethibishwa na CAG labda aende yeye kukagua sasa ajipe Mamlaka mwenyewe aende kukagua. Kwa hiyo suala la kumbukumbu kuwa zina mashaka au kutokuwa na mashaka halina mantiki hapa, suala ni kwamba CAG amehakiki deni hili la Sh.398,845,888,750 na madeni yako mengi lakini hili ndiyo linahusiana na kufutwa kwa ada ya mwaka ya magari. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo naunga mkono hoja iliyoletwa na Waziri lakini na maelezo ya Kamati tunaunga mkono na jambo hili tusilifanye refu kwa sababu Bunge ndiyo lenye mamlaka, tufute tuendelee na kazi zingine. Tunaleta malumbano mengine ambayo hayana tija hapa, vinginevyo sasa tunaanza kufanya kazi ambazo siyo zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)