Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii

Hon. Maulid Said Abdallah Mtulia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia mimi pamoja na Wabunge wenzangu leo kupata fursa ya kujadili hoja zote mbili zilizotolewa na Wenyeviti wetu wa Kamati; pili nikushukuru na wewe kwa kunipa fursa hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, upande wangu mimi naunga mkono hoja zote mbili na Maoni ya Kamati. Hata hivyo nilikuwa nataka niseme hapa, kama kuna Kamati amabzo zinaonyesha namna gani Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi ilivyotekeleza Ilani na inavyojali maendeleo ya watu, basi hoja za leo zinathibitisha kwa wazi kabisa kwamba Serikali si tu inajali maendeleo ya vitu bali pia imezingatia sana maendeleo ya watu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii adhimu kabisa kumpongeza Rais wetu mpendwa, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kusimamia kwa dhati, kwa umahiri mkubwa kabisa, kujenga na kuleta maendeleo ya watu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nayasema hayo ukizingatia kwamba hivi sasa pesa za elimu bure kila mwezi Serikali inatoa bilioni 23. Ukipiga hesabu kwa Mwaka unapata biloni 276, na ukizidisha miaka mitano ya Awamu hii unapata trilioni 1.38

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo; ukienda kwenye mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, tumetoka katika bilioni 337 mpaka bilioni 450; na kama nayo utaizidisha mara miaka mitano unapata trilioni 1.7.

Mheshimiwa Naibu Spika, nayasema haya, haya matrilioni nayataja kwasababu ukienda kwa lile jambo ambalo linasemwa sana la ndege si zaidi ya trilioni 1.2. Kwahiyo utaona kwa haya mambo mawili niliyoyataja ya Wizara hii ya Elimu imezidi gharama tulizoziweka kwenye ndege kwa sababu tu Serikali inajali maendeleo ya watu na inahakikisha watu wentu wanapata maendeleo sambamba na maendeleo ya vitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ukija kwenye afya huko ndiko hatari kabisa. Utakumbuka huko nyuma iliwahi kutokea Mtu alifanyiwa operation ya kichwa badala ya operation ya goti; lakini leo Serikali yetu imenunua vifaa vikubwa kabisa. Kuna angle-suit inanunuliwa pale MOI kwa ajili ya kufanya operation ya Ubongo kwa kutumia mshipa wa paja. Kwahiyo leo Mtu unaweza kumkuta anafanyiwa operation kwa kutumia mshipa wa paja lakini operation ya kichwa, mambo ya kwenda kufumua ubongo sasa hayapo tena. Haya yanapatikana Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia gharama za vifaatiba na dawa za Wizara ya Afya inafika trilioni 1.35. Sasa wakati mwingine wenzetu wengine wanaweza wakasema hatufanyi hiki, hatufanyi kile, hatufanyi vile lakini lazima tuwaoneshe Serikali inafanya vitu gnai ambavyo vinaleta maendeleo kwa Wananchi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukienda kwenye michezo; leo tu umemtambulisha yule kijana bondia amekuja na mkanda wake hapa; lakini najua kuna Bondoa Mwakinyo amekuja na mkanda hapa. Mwaka jana tumekwenda kule Misri kwenda kuipeleka timu yetu; ambapo tangu miaka ya 1980 hatujawahi kwenda katika Mashindano ya Afrika, lakini tumeenda katika Utawala huu. Mimi nasema kwamba Utawala huu umekuja na mavumba, umekuja na kismati unafanyakazi kweli kweli.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Simba mambo waliyoyafanya ni makubwa. Wewe unajua kwamba tumefika robo fainali kwenye robo fainali kwenye Mashindano ya Afrika. Hivi tunavyozungumza, Bwana Ally Samatta yuko Uingereza; kwa mara ya kwanza tumepeleka mchezaji kule anapiga soccer katika Premier League ya Uingereza. Mtu mwingine anaweza akayaona haya yanatokea kama uyoga. Wakati wenzetu wengine wanasema hatuhajafanya huki, hatujafanya hiki sisi tunaenleza tumefanya hili, tumefanya hili, kazi inapigwa kweli kweli.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukienda wkenye Maoni ya Kamati; Kamati inaitaka serikali sasa kwenye michezo waje na uboreshaji wa viwanja vyetu vya michezo; lakini si uboreshaji peke yake na kuongeza idadi ya viwanja vya michezo pale Dar es salaam na Mafia, lazima Mafia tupeleke viwanja vya michezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na hili, tunataka sasa tuje na Kampuni, viwanda ambavyo vitaleta nafuu katika gharama za vifaa vya michezo (Sports industry). Tukifanya hivi kwenye michezo tutafika mbali sana. Nchi nyingine zote, katika idara ya michezo, idara ya sanaa, idara ya mambo ya music ni miongoni mwa idara tajiri sana, lakini kwetu bado inaonekana kuna umasikini. Serikali ikiongeza nguvu kwenye michezo hapa tunaweza kupoata ajira nyingi sana kwa vijana wetu na vijana wetu wakapata maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kamati imesisitiza umuhimu wa Baraza letu la Kiswahili kushirikiana na Wizara ya Elimu kutengeneza vyuo vingi vya kufundisha walimu wa Kiswahili kwenda kuwafundisha Kiswahili wasiokuwa Waswahili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama utakumbuka Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amejaribu kukimiliki Kiswahili na kuuonesha ulimwengu kwamba Kiswahili wenyewe ni Watanzania, na amefanya juhudi kubwa sana. Vilevile kuna soko kubwa sana East Africa, kuna soko kubwa sana SADC, kuna soko kubwa sana Afrika nzima na ulimwenguni. Tunapokuwa hatuna vyuo vingivya kutoa walimu wengi wa kufundisha Kiswahili kwa wasio waswahili, soko hili litachukuliwa na watu wengine na sisi tutakosa fursa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tumefika mahali, tunakwenda kwenye uchumi wa kati, lakini uchumi wa kati una utamaduni wake. Ifike mahali Wizara yetu ya Elimu na Serikali kwa ujumla itengeneze chombo kitakachopitia mitaala yetu yote ili tuje na kitu ambacho kitatupeleka latika uchumi wa kati. Uchumi wa kati hauwezi kwenda kwamba wanaume wako wanawakata masikio wake zao, uchumi wa kati hauwezi kwenda wanaume wako wanawabaka watoto wadogo, wanawalawiti, uchumi wa kati una ustaarabu wake. Ili tuingie kwenye ustaarabu wa uchumi wa kati lazima na mitaala yetu iwa-shape watu wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, miaka ya zamani tulikuwa tunafundisha sayansi kimu watu wapige mswaki, watu wafanye hivi lakini leo lazima tuwafundishe watu utamaduni huu wa kiulimwengu wa watu kuwa wastaarabu, kwasababu uchumi wa kati unataka watu
wafanyakazi, wawe wastaarabu, wawe wavumilivu, wawe hivi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tulikuwa tunazungumza hapa kwamba kuna watu wanazidai hospitali maiti, hospitali watu wapate matibabu, wazee na vijana; suluhisho ni kuja na Sheria ya Bima ya Afya kwa Wote; isiwe leo Watanzania mtu akijijua ana tatizo la figo ndipo anakwenda kukata bima. Tunapokuwa na watu wa bima ambao tayari wameshajijua wagonjwa, na ni wengi ndipo wanakwenda kukata bima, hapana. Tuje na nima ya watu wote kwasababu watu wengi watachangia na wachache wenye matatizo ndio tutakaowatatulia matatizo yao. Leo unamkuta mtu anasema hapa tupeleke watu nje, Serikali haijakosa kupeleka watu nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, zamani tulikuwa tunapeleka watu zaiid ya 600 kwenda kutibiwa nje, leo tunapeleka watu 65 sasa ukipiga mahesabu ya kipesa hapa, pesa tunazookoa ni zaidi ya trilioni 1.835. Haya ni mambo ya fedha. Uthibitisho kwamba watu wanapelekwa nje Mheshimiwa Lwakatare yule pale amepelekwa nje, na uthibitisho wa kwamba watu wanafanyiwa opetation za figo, siku hizi operation za figo ziko hapa Dodoma. Mtu akipata tatizo la figo, wala Wanyamwezi hawaji tena Dar es salaam, wanaishia Dodoma hapa hapa, wanafanyiwa operation ya figo, hayo Mabusha ndiyo usiseme wanamaliza kabisa, kule kwetu hakuna fujo siku hizi mambo yanakwenda vizuriā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaj)

NAIBU SPIKA: Ahsante Mheshimiwa muda wako umeksiaha, ahsante sana.

MHE. MAULID S. A. MTULIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naunga mkono hoja zote mbili za Kamati.