Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Kamati naomba niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge ambao wamechangia katika hoja yetu. Katika mjadala huu, Waheshimiwa Wabunge ambao waliochangia Taarifa yetu ni Wabunge 14. Sehemu nyingi ya michango hii ilikuwa ni ushauri, tunaichukua michango ile kama ushauri lakini yako mambo machache ambayo nilidhani ni vizuri tuyatolee ufafanuzi.

Mheshimiwa Spika, Kaka yangu Mwijage amesema hapa kwamba mimi nimepitia kwenye mikono yake, ni kweli. Kipindi kile naanza kufinyangwa katika Utumishi wa Umma nilianzia pale TPDC na miongoni mwa watu waliofanyakazi kubwa ya kutuonyesha sekta ya Nishati iko vipi ni Kaka yangu Mwijage, na siku zote manshukuru sana kwa kazi kubwa aliyoifanya.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mwijage ameibua mambo makubwa katika Taarifa yetu. Kwanza ameonesha hofu kwamba yapo mambo ya msingi hatukuyatendea haki katika taarifa yetu. Jambo kubwa alilolizungumzia ni uwekezaji unaofanywa na TPDC katika suala zima la kutafiti mafuta na gesi. Ukipitia taarifa yetu ni kweli hatulisema kwa undani jambo hili; na tulifanya hivi makusudi kwasababu mbili:-

Mheshimiwa Spika, jambo hili tumekuwa tukilisema mara kwa mara kwenye Taarifa zetu zilizopita; ni jambo ambalo Serikali inalifanyiakazi. Nataka nimtoe hofu; katika Bajeti tuliyopitisha hapa tulitenga fedha kwa ajili ya kazi ya utafiti; ipo kazi inaendelea kufanywa na TPDC. Hata hivyo kama Kamati tuliamua kufanya uamuzi wa makusudi wa kutoliibua sana jambo hili ndani ya nyumba yako hii kwasababu tuna mfano halisi, nchi inapojenga matumaini makubwa kwa wananchi msipoya-manage matumaini hayo mnaweza kuzalisha tatizo ndani ya Nchi.

Mheshimiwa Spika, kwahiyo kimsingi tuliamua ku-manage expectation kwa taifa letu; na kama kuna jambo ambalo huwa linajenga matumaini makubwa kwa wananchi ni wanaposikia suala la mafuta. Ukiwaambia tu kuna utafiti kesho yake asubuhi wanakwambia nchi yetu ina mafuta. Kwahiyo tulidhani tuwe makini katika kufanya jambo hili. Itoshe kusema, katika bajeti ya mwaka huu tulitenga shilingi bilioni 33.2 kwa ajili ya Kitalu cha Mnazi Bay kule Kaskazini. Ipo kazi inafanywa kule na TPDC, zipo kazi zimeshafanyika, anatafutwa mshauri mwelekezi ili aweze kushauri jinsi ambavyo tunaweza kufanyakazi ya kuchoronga visima kwa ajili ya utafiti wa mafuta.

Mheshimiwa Spika, vilevile kwenye kitalu cha Easi Wembere nako tulitenga bilioni 6.3, ipo kazi inafayika na kazi inakwenda vizuri. Pia lipo eneo la Kitalu Namba Nne kwenye maji ya bahari ya kina kirefu, tulitenga bilioni 22.62, ipo kazi inaendelea. Nataka niliambie Bunge hili kwamba utafiti uliofanya na TPDC ulitumia the best technology in the World katika kufanya utafiti wa kupata mambo haya. Kwahiyo, itoshe kusema kwamba ipo kazi kubwa inafanyika.

Mheshimiwa Spika, lipo jambo lingine kaka yangu Mwijage amelisema. Hili msingi wake ni kazi ambayo Kamati imekuwa ikiifanya kwa muda mrefu. Hoja ya kuwa na hifadhi ya pamoja (Strategic reserve) ya mafuta katika nchi hii ni hoja ambayo Kamati yangu imekuwa ikiishughulikia kwa muda mrefu. Hivi tunavyozungumza, TPDC ina mkakati wa kutumia matenki yaliyopo Kigamboni kufanya ukarabati ili matenki yale yaweze kuhifadhi mafuta. Kama haitoshi, TPDC imeshapata maeneo kule Tanga kwa ajili ya kujenga matenki ya kuhifadhi mafuta.

Mheshimiwa Spika, vilevile yamekuwepo mazungumzo kwamba tunaweza kutumia refinery yetu iliyoko kule Kigamboni ili kuwa na mfumo huu wa uingizaji wa mafuta kwa pamoja. Imekuwa na changamoto zake, wadau wamekuwa wakipishana, na jambo hili alikabidhiwa TR ili kuweza kuja na majibu ya jinsi gani tunatoka hapa. Kuna kazi inaendelea, kwasababu haijafika sehemu nzuri tulidhani tusillibue ndani ya Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Spika, lakini sambamba na hilo, wenzetu wa Mamlaka ya Bandari nao huenda wakaingia wkenye kujenga matenki haya ili yaweze kutumika katika uhifadhi wa mafuta. Ninachoweza kukubaliana nae ni kwamba ni kweli, jambo hili ni la msingi sa, pengine tumechelewa kulifanyiakazi, ni vizuri Serikali ikaongeza kasi katika kushughulikia jambo hili.

Mheshimiwa Spika, amezungumzia katika suala la upotevu wa mafuta, amezungumzia suala la flow meter na margin; haya ni mambo ambayo yanajenga ule msingi wa dhamira yetu ya kuwa na hifadhi ya pamoja ya mafuta. Kwahiyo, nimuondoe hofu, mambo haya Kamati inayashughulikia.

Mheshimiwa Maige kuna jamno amelibua la utozaji wa loyalty katika mawe lakini vilevile katika dhahabu. Hili tunalichukua, nikuahidi Kamati itali-persue tuone tunatokaje katika mkwamo huu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba kutoa hoja, ahsante sana. (Makofi)

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Spika, naafiki.