Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Mboni Mohamed Mhita

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Handeni Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Nilitamani sana niweze kumwelewesha ndugu yangu Mheshimiwa Salome. Sasa asiweze kunitoa kwenye reli na maelezo mazuri ambayo yamezungumzwa na mama yetu Mheshimiwa Jenista, naomba niendelee.

Mheshimiwa Spika, naomba kwa namna ya kipekee, kwanza kabisa nitumie fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Katika jarida la The Diplomat toleo la Januari, 2020 limetamka au limemwita
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni A Game Changer kwenye mining industry.

Sasa wenyewe tunaweza tukajipima na tukaona kama jarida kubwa kama hilo la The Diplomat limeweza kutambua wazi na kumwita An African Mining Game Changers, siyo Tanzania Game Changer kwenye mining sector, lakini African Game Changer kwenye Sekta nzima ya madini. Sisi tunajua na wao wanaanza kutambua hilo.

Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kuipongeza sana Wizara ya Mambo ya Nje kwa namna ya kipekee katika kipindi hiki cha miaka minne ya utekelezaji wa Ilani, kimefanikiwa au Wizara imefanikiwa kuongeza Balozi saba.

Mheshimiwa Spika, naomba nizitaje, ya kwanza ni Algeria, ya pili Israel, Sudan, South Korea, Quba, Namibia pamoja na Qatar. Hii inaonesha ni jinsi gani ambavyo Wizara inaendelea kujipambanua kwenye kukuza uhusiano wa kimataifa na diplomasia ya uchumi. Pia, ni jinsi gani ambavyo kupitia hizi Balozi zetu mpya itashughulika na watanzania ambao wako kwenye nchi hizo, nikiwa na maana ya diasporas lakini pia kupitia uchumi (economic diplomacy) itaendelea basi kushughulika na wawekezaji ambao wana interest ya kuja kuwekeza Tanzania. Vilevile kikubwa zaidi pia kuweza kuvutia utalii.

Mheshimiwa Spika, hapa niwe muwazi kabisa, kuna Balozi ambazo zimekuwa ni mfano wa kuigwa kwenye suala zima la watalii. Ubalozi wa kwanza ni China, Ubalozi wa pili ni Israel, Ubalozi wa tatu ni Urusi. Mabalozi hawa wamekuwa; natafuta neno sahihi la kuwaita; lakini wazalendo kupindukia kwa sababu wamejitoa kwa namna ya kipekee kwa kujiongeza kufanya marketing kwenye sekta nzima ya utalii, na tumeshuhudia watalii ambao wamekuja nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuna changamoto moja hapa; hawa mabalozi hawana fungu lolote la marketing, marketing funds ziko kwenye Wizara ya Maliasili na Utalii. Hivyo basi, naomba nitumie fursa hii kuwashauri wenzetu wa Wizara ya Mambo ya Nje ione ni jinsi gani itakuja na utaratibu wa kuweza kupata fedha kidogo za kuweza kuwasaidia Mabalozi wetu kwenye nchi hizo ili waendelee basi kujipambanua zaidi na kuja na njia latest au more ways za kuona ni jinsi ambavyo wanaweza kukuza utalii.

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii pia kuipongeza sana Wizara kwa namna ya kipekee. Katika kipindi hiki kifupi tumeshuhudia SADC ikipitisha Kiswahili kuwa ni an official and working language; na tunakumbuka wazi kwamba SADC ina nchi 16 lakini wakati huo huo na nchi za Maziwa Makuu (Great Lakes) ambayo imekusanya nchi 13 nao pia wamepitisha kuwa Kiswahili kuwa ni official language na official working language. Wizara haikuishia hapo, imeenda mbali zaidi kwa kushirikiana na Baraza la Kiswahili imeanza kuandaa mitaala ambayo itatumika sasa katika nchi hizo. Hapa tumeona kwamba Wizara imeamua kujipambanua na imeamua ku- champion hili suala zima la Lugha ya Kiswahili.

Mheshimiwa Spika, Wizara yetu ya Mambo ya Nje inamiliki nyumba 106 lakini wakati huohuo ina viwanja takribani 12. Naomba nitumie fursa hii kuishauri basi Wizara ione ni namna gani sahihi hivi viwanja 12 vitajengwa ili kuweza kupunguza gharama ambazo kwa sasa Serikali inapata lakini pia adha ambayo Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje wanayopata kupitia kutokuwepo kwa nyumba za kudumu katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, nimalizie sasa, na ninaomba nimalizie kwa kuzungumzia Chuo cha Diplomasia ambacho ni chuo sasa hivi, au kilianzishwa kupitia uhusiano kati ya Tanzania na Mozambique, Tanzania wakiwa na asilimia 50 na Mozambique wakiwa na asilimia 50. Kwa muda mrefu sana wenzetu wa Mozambique wamekuwa hawatoi mgao wao au hawachangii katika makubaliano yale; na kwa namna moja ama nyingine hiyo imekuwa inaturudisha nyuma. Nilikuwa naomba niishauri Wizara basi, kwa namna ya kipekee iangalie mfumo gani mzuri na wa kidiplomasia wa kuweza kuachana na wenzetu waweze kuendelea kwa sababu ni dhahiri kwamba hawana nia ya kuendelea na muungano huu na sisi tujiongeze. Tuna majengo ya kutosha Dar es Salaam sasa hivi Serikali imehamia Dodoma, tuna mitaala mipya katika sekta nzima ya diplomasia ya uchumi ambayo sasa; na ninaamini kupitia Wizara hii makini ikifanya hivyo kwa kutumia majengo yetu ambayo yako pale Dar es Salaam chuo kitaendelea kukua na kitasaidia vijana wengi ambao wanataka kujiongeza katika sekta nzima ya diplomasia.

Mheshimiwa Spika, niishie kabisa sasa kwa kuipongeza Wizara ya Mambo ya Nje kwa kuendelea kuimarisha uhusiano wa kimataifa na nchi mbalimbali, nchi zetu ambazo tunapakana nazo nchi za Afrika Mashariki, nchi za African Union, nchi za ACP, European Countries, American Countries. Tumeshuhudia juzi wenzetu wa EU tuko nao wamekuja kutusaidia hiyo Euro milioni sitini lakini pia tumeshuhudia wenzetu wa Marekani jana tu wametoa vifaa vya kijeshi kwa Wizara ya Mambo ya Ndani. Naomba kutumia nafasi hii Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Nje na kuwatakia kila la kheri.

Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii sasa kuishia hapa, nashukuru sana kwa kunipa fursa. (Makofi)