Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Peter Joseph Serukamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati Kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, nami naomba niwapongeze Wenyeviti; Mwenyekiti wa Kamati ya Madini na Nishati kwa ripoti zao nzuri sana. Nawapongeza sana Wizara ya Nishati na Wizara ya Madini kwa kazi kubwa wanayofanya.

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema ndugu yangu Mheshimiwa Mzee Keissy kazi ya umeme inayofanyika Tanzania ni nzuri sana, naipongeza sana Serikali. Nataka niseme jambo moja ambalo nadhani kama Bunge lako, hatujalipa nafasi ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika na Waheshimiwa Wabunge wenzangu, kilichofanywa na Rais, kilichofanywa na Serikali kuingia makubaliano mapya na wawekezaji wakubwa wa madini, kwa vyovyote vile ni jambo ambalo sisi kama Bunge tunapaswa kuipongeza Serikali. Wako wanaosema ambao mimi naelewa kwa nini wanasema, lakini najaribu kuangalia tutakachopata kama nchi kwa makubaliano haya makubwa na kwa uchumi wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, cha kwanza ukisoma kwenye yale makubaliano ambacho watu wengine wanaweza wakaona ni kidogo, ofisi za Barrick London, ofisi za Barrick Johannesburg, zote zinafungwa, zinakuja Tanzania. Maana yake wafanyakazi wale watakaa kwenye nyumba za Watanzania, watalala kwenye hoteli za Watanzania, watakula kwa Watanzania. Maana yake uchumi mkubwa katika nchi utaongezeka sana. Bado hapa sijaongea habari ya ajira. Ninayo hakika, leo ukienda Dar es Salaam na mikoa ya Mwanza na Arusha bei ya nyumba zimeshuka, lakini unapopata Kampuni kubwa kama Barrick, wafanyakazi wake wanakuja kukaa Tanzania, maana yake nyumba zetu zitarudi bei kuwa juu, kwa sababu wale watu wana- income kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia ziko faida za kiuchumi. Moja ya faida kubwa, ukiangalia pale, Serikali ina asilimia 16, lakini Tanzania tutapata cooperate tax 30%. Tutapata karibia 3% kwa ajili ya Local Government. Maana yake kwa uchumi tunakwenda kupata kila mwaka mapato ya zaidi ya 50% kwa revenue ya kampuni hii. Kwa vyovyote vile Mtanzania yeyote ukisimama unalaumu jambo hili, then maana yake hufahamu uchumi mpana unavyofanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vile vile naangalia social responsibility ambapo kwa watu ambao wanazunguka na madini kule ambako madini yapo watafaidi zaidi kuliko Halmashauri nyingine za mbali ambazo sisi tunakaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nataka niwaambie wenzangu, mimi nimeangalia vizuri sana, tunaanzisha kampuni mpya ya Twiga, ukiingalia watu watasema unapata 16% lakini mkishakuwa na kampuni maana yake baadaye ikiishaanza kufanya biashara, tutaipeleka kwenye stock exchange, kwa sababu ni kampuni mpya hii. Tukiipeleka kwenye stock exchange, watakaofaidi ni mimi na wewe na sisi. Haya ni mageuzi makubwa ya kishujaa ya kimapinduzi. Tanzania tume-set tone Africa. Leo hii Waafrika wote wanakuja kujifunza tuliyoyafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, habari ya smelter, hata kama isipojengwa hapa, ambayo naamini baadaye itajengwa, bado kwa sababu tumeweza ku-identify a new company, watu wetu watakuwemo kwenye Bodi, ofisi zitakuwepo hapa, usimamizi bado kama nchi tutafaidi ndugu Wabunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naangalia, kwa mara ya kwanza, tutakuwa na Board Members kwenye kampuni hiyo Watanzania ambapo naamini jambo hili ni kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia kubwa zaidi ambalo wote hamlisemi, tulitunga sheria mwaka 2010 hapa; moja ya jambo kubwa tulilotunga, makampuni haya…

(Hapa Mhe. John W. Heche alisimama)

SPIKA: Mheshimiwa Heche, naomba utulie. Halafu wanaogeuza kiti nyuma kwa Spika wanakosea. Mnatakiwa wote muwe mnamwona Spika anavyopendeza. (Kicheko/Makofi)

Tusikilize shule inayoshushwa na Mheshimiwa Peter Selukamba.

MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, moja ya jambo kubwa lililofanyika, kuna maamuzi makubwa ambapo tulitunga Sheria ya Madini Mwaka 2010, kwamba makampuni yote ya madini fedha zao wataweka kwenye benki za Tanzania. Maana yake ni nini? Wakiweka fedha kwenye benki za Tanzania; NMB, CRDB na benki zote, fedha zile Watanzania wote tutazi- access kwenye mikopo. Maana yake fedha za Barrick, pamoja na kwamba zitafanya kazi ya kuchimba, zitafanya na kazi ya uchumi kwa Watanzania. Hili ni jambo kubwa, uncles wenzangu hatuelewi maana ya fedha kuja kwenye benki za Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu wakileta; kwa mfano, leo najua watu kama GGM fikiria fedha zao zote wanaweka kwenye benki moja ya Tanzania, Barrick; maana yake ni nini? Siyo kwamba fedha zile ni kwa ajili ya kumpa Barrick or Geita peke yake, maana yake fedha zile kwa sababu ziko kwenye benki zitatumika na masikini wa nchi hii kuwakopesha kufanyia biashara. Huu ndiyo uchumi mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, muhimu zaidi leo nataka niseme, kwa muda huu ambao walikuwa wamesimamisha biashara, nenda leo kaangalie Kahama, Shinyanga na Mwanza utaona tofauti. Tumefaidika kidogo baada ya Waziri wa Madini ambaye nami nampongeza sana ndugu yangu Mheshimiwa Doto kuhakikisha wachimbaji wadogo wanapewa nafasi ya kufanya kazi kubwa. Kama leo ingekuwa wachimbaji wadogo hawapo, tungekuwa na hali ngumu kiuchumi mikoa ile ya Kanda ya Ziwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, fikiria, tuna wachimbaji wadogo, tumewawekea regulation, tumewawekea masoko, wanaleta fedha, tunapata kodi na on top of it tunawaleta na wachimbaji wakubwa wanaanza kufanya biashara yao. Kwa vyovyote vile hili ni jambo kubwa. This is a game change of the economic Tanzania; na sisi kama Wabunge tunapaswa kuwa watu wa mwisho kuinyooshea kidole Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, rafiki yangu Mheshimiwa Heche amesema kwamba Wabunge wa CCM tunatakiwa kuona aibu. Nadhani kuna maeneo haelewi vizuri. Anasema tunabadilisha sheria. Wewe umekaa muda mrefu na wengine wachache wamekaa muda mrefu, kila mwaka tunabadilisha sheria. Miscellaneous maana yake nini? Miscellaneous tunaleta tubadilishe sheria ambazo aidha tulitunga tukakosea, tumefikiria, tunatunga upya. Suala la kubadilisha sheria halimaliziki leo. Mbona sheria nyingine hawasemi? Kazi ya Wabunge ni kutunga sheria. Ukitunga sheria leo, ukaanza kuitumia, ukaona haikuletei ulichokuwa unakitaka, prudence yoyote, unaleta unabadilisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumetunga sheria nyingi hapa za fedha, tunakwenda tunagundua haifai, tunaileta tunaibadilisha. Kwa nini Sheria ya Madini tukiibadilisha iwe nongwa? Ni nongwa! Mimi naelewa kwa nini ni nongwa. Ni kwa sababu wanaona Chama cha Mapinduzi kinafanikiwa sasa. Ni nongwa kwa sababu wanaona Chama cha Mapinduzi na Serikali yake kimeanza kuelewa na kuleta mageuzi makubwa ambayo kasi ya uchumi itakuwa kubwa, nafasi yao inazidi kupungua kadri siku zinavyoenda mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nawaomba watu wa Serikali, msiogope. Kama kuna maeneo tulifanya tukadhani hayatuletei faida, leteni tubadilishe, ndiyo kazi yetu. Nasema tuleteeni! Moja ya kazi kubwa tukibadilisha sheria hii, maana yake tuna-attract more investors. tuki-attract more investors, maana yake uchumi wa Tanzania utakua; na ile dream ya Mheshimiwa Rais Magufuli ya kwenda kwenye uchumi wa viwanda, kwenda uchumi wa kati, tutai-realize kwa kuandika sheria nzuri.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, naomba kuunga mkono hoja ripoti ya Kamati. (Makofi)