Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. William Mganga Ngeleja

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

MHE. WILLIAM M. NGELEJA - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa niaba ya Mwenyekiti wetu wa Kamati ya Sheria Ndogo Mheshimiwa Mtemi Andrew Chenge ninaomba kuhitimisha hoja yetu iliyowasilishwa asubuhi ya leo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kukushukuru wewe kutuongoza vizuri siku ya leo kama ilivyosiku zote, lakini pili kuwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wenzangu waliochangia hizi taarifa tatu ambazo zimewasilishwa leo kwa upekee nawashukuru sana Waheshimiwa Naibu Mawaziri pamoja na Waziri kwa ujumla wake. Kwa kufafanua hoja ambalimbali ambazo ziliibuliwa na Waheshimiwa wachangiaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kamati ya Sheria Ndogo tunaendelea kupokea salamu hizi za upendo salamu za pongezi kwa kadri ambazo ambazo zimejitokeza kwenye mjadala huu na tunalihakikishia Bunge lako tukufu kwamba Kamati yetu ya Sheria Ndogo iko tayari itaendelea kuyatenda yaliyomema kwa maslahi ya Taifa letu na tunaendelea kumshukuru sana rafiki yangu Mheshimiwa Jenista Mhagama kwa coordination nzuri unayoifanya tupo tayari tulishawahi kujadili huko nyuma kwamba kwa kadri ambavyo Serikali na viongozi wetu wa Bunge mtakavyoona inafaa kwa sababu sheria ndogo zimekuwa nyingi leo umesikia habari ya sheria ya mia nane tisini na kitu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unaposikia kwamba kati ya sheria 897 zilizowasilishwa lakini zinaonekana zinadosari labda ni sheria ya 73 haimaanishi kwamba sheria zingine zote hazikuchambuliwa maana yake kwamba sheria zote kamati imezipitia kwa hiyo, inatumia muda mwingi. Kwa hiyo, tulishawahi kuweka wazo na tunaendelea kushauri kwamba kwa sababu kwamba kwa sababu katika mfumo wetu wa uendeshwaji Bunge kuna baadhi ya Kamati ambazo kwenye mikutano yetu ya kawaida huwa zinatangulia angala wiki moja kabla ili tuondoe tupunguze stress ya muda tunaotumia kuzichambua hizi Sheria Ndogo utawala, mtaangalia kama hilo linawezekana ili Kamati ya Sheria Ndogo pia ipate hiyo fursa hili tufanye kazi kwa utulivu zaidi kuliko tunavyofanya sasa pamoja na kwamba haijaathiri ubora wa kazi tunazozifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati tukiendelea kuhitimisha hoja yetu kuna mambo matatu tunataka tukumbushe na ninaikumbusha Serikali kwa sababu wenyewe wamekuwa wakiwasilisha hizi Sheria Ndogo kwetu. La kwanza ni jambo la ujumla kwamba tunauzoefu wa kuona kwamba kwenye taasisi nyingi za Serikali wanasheria hasa wenye taaluma ya ususi wa uandishi wa hizi sheria kimsingi kuna uhaba wake na tunahitaji kuongeza ajira katika eneo hili na kuboresha ama kuboresha mafunzo kwa waliopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo tunaomba Wizara ya Sheria kwa ujumla wake na hasa kitengo hiki cha Uwandishi wa Sheria legislative draft file tunaomba sana kipewe nafasi tupate kuongeza nguvu kazi pale kwa ajili ya kuboresha shughuli za uandishi wa Sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili ambalo tunakumbusha Serikali ni kwamba tumeshuhudia sisi kwenye Kamati zetu katika utendajiwetu wa kazi wa kila siku ziko baadhi ya Sheria Ndogo zinazokuja kwa namna ambavyo zimetungwa ni kama zinapoka mamlaka ya na madaraka ya Sheria ambazo zimeziazisha hizi Sheria Ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hii ni changamoto inawezekana si rahisi sana kuielewa tulivyozungumza lakini kwenye Kamati tunaweza kuelewa, tuna utungaji wa Sheria Ndogo na misingi yake sasa inapotokea kwamba Sheria Ndogo zile ambazo kimsingi zinatungwa kutokana na Sheria mama zenyewe tena zinakuwa na mamlaka na masharti ya kupoka sheria ya mama ambazo ndiyo kwanzo ndiyo zimetungwa kutokana na hizo Sheria mama tunakuwa na tabu kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo tunaiomba sana Serikali pamoja na vyombo vingine vinavyoshiriki katika utungaji wa sheria ndogo ili kupunguza muda wa kuzipitia hizi Sheria Ndogo lakini pia usumbufu wa kila wakati kukumbushana ili jambo pia lizingatiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho lakini siyo la umuhimu, tunaikumbusha Serikali kwamba katika utungaji wa hizi Sheria Ndogo na hasa tunapoanza kutunga Sheria mama, Sheria yake inamchakato wake kuna Muswada unajadiliwa sasa katika masharti ambayo yamekuwa nyakati nyingine inatokea masharti inayopendekezwa katika Muswada wa Sheria unaokuja kuzaa Sheria ambayo baadaye zinatungwa Sheria Ndogo. Wakati mwingine kunakuwa na baadhi ya masharti ama vifungu vya Sheria hizo mama yanakataliwa kwenye mjadala kama hapa bungeni ama hata upande wa Serikali kutokana na mashauriano ya Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hayo masharti hasi ambayo yanakataliwa mara nyingi huwa tunaona yanaibukia tena kwenye Sheria Ndogo sasa hili ni jambo ambalo limekuwa likitukwanza kidogo kama kamati lakini yote kwa yote ndiyo umuhimu wa kuwepo Kamati ya Sheria Ndogo ya Bunge lako Tukufu ndiyo ni sehemu yetu ya kazi yetu tunaamini kabisa kama haya yote yasingekuwepo bali isingekuwa na uhalali wa kuwepo. Lakini jambo jema kukumbusha kwamba kwa yale masharti ambayo yamekuwa yakikataliwa kwenye utungaji wa sheria mama yasije tena kupitia mlango wa nyuma yakaibukia huku kwa sababu huku milango imefungwa, ni jambo la kukumbusha ni jambo jema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo kwa mara nyingine niwashukuru sana Wabunge wenzangu ahsanteni sana tupo tayari kushirikiana na ninyi na kwahauta hii sasa kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Sheria Ndogo naomba kutoa hoja kwa mara nyingine tena ahsante sana. (Makofi)

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.