Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Mohamed Omary Mchengerwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rufiji

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA - MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwanza kwa kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote waliochangia taarifa yetu ya mwaka lakini kipekee kabisa niwapongeze sana Waheshimiwa Mawaziri ambao kimsingi wamejibu hoja nyingi ambazo kamati yangu ya katiba na sheria imeziibua. Nimpongeze sana Mheshimiwa Mzee Mkuchika kwa kutoa darasa zuri kwa Waheshimiwa Wabunge ambalo kwa kweli limeeleweka kweli kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimpongeze Mheshimiwa Dkt. Mahiga kwa majibu mazuri Mheshimiwa Kairuki ambaye ametoa ufafanuzi mzuri kuhusu suala nzima la uwekezaji lakini pia Mheshimiwa Jenista Mhagama ambaye amefafanua kwa kina kabisa kwa hiyo hoja nyingi ambazo, zimeongelewa na Waheshimiwa tayari zimeshajibiwa na waheshimiwa Mawaziri hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lazima niseme kwamba tatizo kubwa ambalo nimeligundua kwa baadhi ya waheshimiwa Wabunge si hoja ya kulalamika bali ni hoja ya kutofahamu sheria na taratibu ambazo zinaongoza Taifa letu. Ni kuombe sana wewe kupitia nafasi yako umshauri Mheshimiwa Spika basi pale ambapo Wabunge wapya wanakuja katika Bunge hili kwa kupitia legislative support programme awamu ya pili, atumie fursa hiyo kutoa elimu ya ufahamu wa Sheria kwa Wabunge eneo hili iwapo litatimia vizuri hoja nyingi zitakuwa zimejibiwa na hakutakuwa na malalamiko yoyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu nimegundua kwa mfano Mheshimiwa Lema analalamikia malaka ya mkurugenzi ya mashitaka na Waheshimiwa wengine ukiangalia, Bunge hili halina mamlaka kwa Bunge hili kwa taarifa halina mamlaka ya kuoji vipengele vya Katiba Bunge hili halina mamlaka nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tatizo kubwa tulilonalo ambalo nimeligundua ni waheshimiwa Wabunge wengi kutokuwa na ufahamu wa Sheria kutokuwa na knowledge ya sheria kwahiyo pengine Mheshimiwa Spika kwa kupitia legislative support programme awamu ya pili aweze kutoa elimu ya ufahamu na nina amini iwapo eneo hili likitekelezwa basi maswali kama yale ambayo yalikuwa yanaulizwa ambayo yalikuwa yanaulizwa na Mheshimiwa Lema hayataulizwa tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na eneo la pili unapo hoji mamlaka ya DPP Mkurugenzi wa Mashitaka maana yake unaoji ibara ya 59 ya katiba zipo taratibu za kuoji katiba, zipo taratibu za kuoji sheria ambazo Bunge hili imezitunga. Kwa hiyo, kwa kutumia utaalamu ule ule ambao Mheshimiwa Spika atatusaidia Waheshimiwa Wabunge itatusaidia san asana kufahamu ni kanuni zipi ambazo kama wabunge tunapaswa kuzitumia pale ambapo tunaona sheria fulani ina mapungufu au kipengele fulani kina itilafu kidogo namna gani Mbunge anapaswa kuja na hoja hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo mengi kama nilivyosema yamejibiwa niendelee kukumbusha tu Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Kairuki basi kwa kuwa Serikali hii ni ya Viwanda kama ambavyo imesisitizwa sana kwenye Bunge lako hili tukufu tumuombe Mheshimiwa anayetekeleza eneo hili la uwekezaji basi kuharakisha mchakato wa utengenezaji wa mapendekezo ya sheria ya uwekezaji. Sheria ya uharakishwaji ya uwezeshaji ya biashara ili sasa iwe raisi kwa utekelezaji wa yale ambayo malengo ya ilani yetu ya Chama Cha Mapinduzi imekuwa ikiwa meendelea kusisitiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pili Mheshimiwa Jitu Soni ameniandikia akioji kuhusu utekelezaji wa sheria ya Finance Art, ya mwaka 2019 ambayo imetoa exemption kwa baaadhi ya utekelezaji wa misamaha ya VAT katika eneo la Serikali Kuu na Serikali za Mitaa nimuombe Mheshimiwa Waziri wa Fedha basi eneo hili liweze kushughulikiwa kwa haraka ili kuondoa mapungufu yaliyopo kwa sasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni kuhusu vibali vya kazi ambao kimsingi Mheshimiwa Jenistar Waziri wa Nchi ametoa ufafanunuzi wa kina kabisa. Lakini Mheshimiwa Ruth Mollel amesisitiza kwa kina sana kuhusu ucheleweshwaji wa mashauri, nimuombe Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria kwa kuwa jupo hapa kusisitiza mahakimu wetu wote nchini na kutumia kifungu cha 225 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai ili kuweza kuharakisha katika mashauri ambayo yanachelewa ili mashauri yale ambayo yamevuka siku 60 basi kuona uwezekano wa mahakimu kuyaondoa mashauri yale ambayo iwapo Serikali basi itaona kwamba iko tayari kuendelea na mashitaka hayo inaweza kuleta kwa kupitia kifungu hicho hicho kifungu kidogo cha tano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ambalo limesisitizwa kwa kina ni kuhusu mamlaka ya mkurugenzi wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa niwaombe waheshimiwa Wabunge watambue kwamba katiba yetu lakini pia sheria ya kupambana na kuzuia rushwa sura ya 7 sheria hii inatoa ufafanuzi kifungu cha 7 kinatoa ufafanuzi wa kazi ambazo taasisi hii inafanya kwa kina kabisa sina haya ya kurudia niwaombe Waheshimiwa Wabunge tujielekeze pengine tukisoma sheria hii maswali kama haya ambayo ni mepesi yanaweza yasiulizwe kwenye Bunge lako tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine ambalo Mheshimiwa Lema alioji ni kuhusu mamlaka ya Mkurugenzi wa Mashitaka kuliondoa shitaka pale ambapo anapoona yeye anapendezwa nalo kuliondoa na kulirejesha wakati wowote niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge kwamba tukisoma mwenendo wa makosa ya jinai kifungu cha 91 kinampa mamlaka mkurugenzi wa mashitaka na mamlaka yake hayahojiwi sehemu yoyote ukisoma Ibara ya 59 ya katiba mamlaka ya mkurugenzi wa mashitaka haojiwi wakati wowote pale ambapo wataona inafaa anauwezo wa kuliondoa shitaka wakati wowote kabla ya hukumu kutolewa na mahakama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ili jukumu ni la mkurugenzi wa mashitaka na nijukumu la Bunge hili iwapo inaona kwamba kipengele hiki hakifai basi Bunge hili linaweza kujiongeza ili kuona uwezekano wa kurekebisha kifungu hiki. Lakini kwa sasa hatuna mamlaka ya kuhoji mamlaka ya mkurugenzi wa mashitaka ambaye yanapatikana katika ibara ya 59 ya katiba yetu lakini mamlaka ya kufuta shitaka wakati wowote kabla ya hukumu kutolewa yapo kwa mujibu ya kifungu 91 cha sheria hii kwa hiyo niwaombe Waheshimiwa Wabunge kujielekeza katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hoja nyingi zimejibiwa na Waheshimiwa Mawaziri na mimi naomba kutoa hoja kwa taarifa yangu kama ambavyo nimesema hapo ahsante.

MHE. YAHAYA Y. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naafiki.