Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nami nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na ardhi, aliyetujalia sote hapa uhai na uzima na kutuwezesha kufanya hili tunalolifanya. Baada ya hapo nitoe shukrani za kipekee kwa wazazi wangu wawili Mwenyezi Mungu awarehemu huko waliko na awahurumie kama wao walivyonihurumia mimi nilipokuwa mdogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna ya kipekee kabisa naomba niyatambue, niyashukuru na niyaenzi malezi ya Walimu wangu wa darasa la kwanza mpaka la saba kama ifuatavyo:-
Mama Clara wa darasa la kwanza na la pili; Mrs Mganga wa darasa la tatu; Mrs. Makundi wa darasa la nne; Mrs Matata wa darasa la tano; Miss Komba wa darasa la sita; na Mr. Mabula wa darasa la saba waliongozwa na ma-head waaminifu, mama Kehemere, Mzee Mwamugunda na Mzee Lukoo. Naomba kwa namna ya kipekee niwaenzi Walimu wangu Wakuu wa Kisutu sekondari 1974-1977 marehemu mama Chale, mpenzi wangu mama Tegisa, Mama yangu Mrs. Munuo na Miss Kassim. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaenzi pia Walimu wangu Wakuu wa Korogwe Sekondari mama Msemakweli na Mwalimu Chisongela, kwa malezi yenu nimefika hapa, nawashukuru sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nianze kuzungumzia mada hii kwa kuangalia Taasisi zilizomo na nianze na NECTA. Katika mambo yanayotia uchungu kwenye Taasisi hii ni credibility yake. Hii ni Taasisi ambayo it makes or destroys Mtanzania. NECTA inatoa maamuzi mwanafunzi anapotoa mitihani yake lakini je, kweli Taasisi hii ina uadilifu wa kutosha kuweza kufanya kazi hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwa ruhusa yako niwasome watoto hawa halafu nitakwambia kwa nini. Kuna hafidhi Hassan Arkam Salum, Nassoro Shaban, Ali Alhabi, Abdulhamid Ahmed, Zamha Abdallah Rashid, Damtu Mohamed Tahir, Fatma Vuai Muhidini, Mwanaharusi Ally, Sabrina Suleiman Ally, Ruwaida Ally Ahmed. Hawa watoto walidhalilishwa mbele ya umma wa Tanzania katika watoto waliofutiwa matokeo yao, hawakufanya vizuri, wamekopia mitihani.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mwenyezi Mungu alichowajalia watoto hawa ni kwamba wazazi wao wana uwezo. Walichofanya wazazi wa watoto hawa, waliwapeleka Arusha Modern na pale wakaamua wafanyiwe mitihani ya Cambridge, mtoto Hafidhi Hassan Ali, alitoka na distinction lakini kama vile haitoshi, ule mtihani wake wa Kiswahili ulipewa A* na A* kwa Cambridge ni kwamba iko beyond 89. Hasa ni Global wise na hiyo A* yake ya Kiswahili ni globaly, worldwide huyu mtoto alitoka Arusha modern, lakini kwa mfumo wetu kwa assessment ya NECTA huyu mtoto kama mzazi wake asingekuwa na uwezo tungeshamsahau sasa hizi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, na hawa wote waliomfuatia katika orodha hii walipata merit. Kwa hiyo, ni watoto na naombeni m-google muangalie how Cambridge wanaweka hizo classification zake, distinction, merit na pass halafu muone sisi tunaingia wapi pale. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama hilo halitoshi kwa NECTA, lingine ni kwamba hawa NECTA wakishakufelisha ukitaka kukata rufaa ukate kwao, mlisikia wapi? Mahakama ya Mwanzo, hiyo hiyo Mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Rufaa ni hiyo hiyo, tunafanyaje haya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nina kesi mbili ambazo walifelishwa niseme na wakakata rufaa. Uzuri hawa walipata msaada wa Walimu wao wenyewe, kama huyu kijana mmoja yeye alipofanya mitihani ya A-level pale Benjamin Mkapa, wazazi wake wakasema haiwezekani Abdulkarim afeli, kupata division III ni Walimu wake waliomsimamia na ziliposahihishwa akapata division one, sasa hivi ni Mhasibu, yuko Arusha Municipality, hiyo ndio NECTA yetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa NECTA katika kasoro nyingine wasifanye kazi kwa uzoefu. Nimepata bahati mbaya ya kupoteza vyeti vyangu, vya O-Level na A-Level, lakini baadaye nikapa hamu ya kwenda kujiendeleza nifanye PhD nilipokwenda shuleni Vietnam, Taasisi zetu za elimu ya juu na NECTA, chuo kikuu wananidai mimi vyeti vyangu vya form IV na Form VI nikawaambia ninyi mnisamehe kwa sababu degree yangu ya kwanza niliipata hapa chuoni kwenu na mlini-admit kwa credential zangu za O-level na A-level, lakini wakaniambia tunakuweka lakini hutopata cheti, huto-graduate mpaka utuletee.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilipokwenda NECTA wananiambia niende shule yangu ya O-level, niende na shule yangu ya A-level wakathibitishe kama mimi nilikuwa mwanafunzi wao pale. Mimi nimeondoka Kisutu 1977, nimeondoka Korogwe Girls 1980. Mwalimu gani ambaye ataweza kuthibitisha zaidi kuwepo kwangu mimi kuliko NECTA ambao wao waliitambua shule, wakanitambua mimi, wakanipa examination number. Haya mambo gani ya kufanya kazi kwa uzoefu? NECTA wabadilike katika utendaji kazi wao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine ambalo linaingia kwenye Wizara hii pia ni suala la Mheshimiwa Kuchauka alichangia siku moja akasema, uwekwe msisitizo katika kufundisha jiografia na historia, lakini nimekuwa nikisema mara kadhaa hapa kwamba, watendaji wetu wanatakiwa wapate dozi ya know your country. Hii nairudia tena leo hapa kwa mfano mdogo kwamba, watu hawa watakapoijua nchi yao, watajua makundi maalum yaliko yanayotengeneza ile jamii kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo watakapofikiria kupanga shughuli maalum kama hizi za michezo kwa mfano, UMISHUMTA sijui, UMISETA na hata SHIMIWI, hawawezi wakayapanga mwezi wa Ramadhani kwa sababu wanajua kuna kundi kubwa la jamii ya Watanzania kushiriki kwao michezo ile itakuwa muhali, basi hata hili nalo jamani tuambiwe, wakati kalenda tunaZIpata mwezi Januari au hata kabla tukaona mle na huwa wanaweka star kabisa kwamba tarehe hizi inaweza ikawa Idd el fitri, kwa hiyo maana yake mwezi before ndiYo Ramadhani, sasa mambo kama hayo yazingatiwe. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba pia nichangie katika, mimi nimeliita the big scandle in town, hili tuliloambiwa hapa, la TCU na Saint Joseph. Hili limetokea kwa haya ambayo Wabunge wengi wamesema na kaka yangu Mheshimiwa Mbatia amemalizia kusema na amekuwa akilisema miaka mingi ya kuchezea elimu yetu na mfumo wetu wa mafunzo katika nchi hii, mahodari wa kuunda Taasisi, kuzipa majina, halafu tukakoroga yale majukumu yake, mwisho wa yote hatupati chochote. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Waziri na kwa namna alivyom-introduce best half wake jana mimi nakuwa wifi, kwa hiyo, nisikilize kwa umakini zaidi, siyo tu Mbunge lakini wifi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ajijulishe kuhusu kitu kilitwa NAMDEC ilikuwepo huko, National Managament Development something ikaundwa HEAC, lakini baadaye nikadhani baada ya kuunda TCU na NECTA na VETA, nikajua sasa ule mkorogo tuliokuwa nao kwenye NAMDEC na ile HEAC kwa maana ya Higher Education Accreditation Council yatakwisha, kwa nini? Kwa sababu zile Taasisi za mwanzo zilikuwa zinachanganya chuo kikuu kimo, kisichokuwa chuo kikuu kimo, lakini ukishasema TCU (Tanzania Commission For Unviversity) ukasema NACTE sijui National Technical Edecucation something; VETA Vocational Education yashajulikana, lakini tunafanya nini?
Mheshimiwa Naibu Spika, Taasisi zilizokuwa chini ya NACTE na zenyewe zinakwenda zinataka kutoa degree zijiite chuo kikuu; Taasisi zile za chuo kikuu zenyewe nazo zinashuka mpaka chini zinataka kutoa vyeti, sasa ni nini? NACTE kwa mfumo wao wanasema wao ni competency based kwa maana nyingine wanatutengenezea hawa watu wa hands on, wale wataoshughulika practically na wao ndio maana kwao…
MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, basi nakushukuru.