Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia katika taarifa ambazo zimewasilishwa kuhusu TAMISEMI, Utawala Bora. Nami napenda kujielekeza zaidi kwenye taarifa ya TAMISEMI na Utawala Bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kuipongeza Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa ushindi mkubwa ambao tumeupata katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambao haujawahi kutokea. Nina uhakika kabisa kwamba Uchaguzi Mkuu tutashinda kwa asilimia nadhani zile zile au zaidi ya pale. Kinachofanya chama kushinda siyo Tume Huru, ni maandalizi ya Chama na jinsi gani chama kinakubalika ndani ya wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge tuliomo humu ndani tumeshinda kupitia Wakurugenzi hao hao ambao leo tunawaona hawafai. Kwa hiyo, mimi naomba tu tujiandae kwa uchaguzi wa mwaka 2020 kwa Tume yetu ile ile ambayo ndiyo imewaingiza humu ndani ya Bunge na nina uhakika wale wenye sifa watashinda na wale wengine ndio hivyo tena. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na kuipongeza TAMISEMI kwa jinsi ilivyosimamia ujenzi wa Hospitali za Wilaya pamoja na Vituo vya Afya kupitia force account. Gharama ambazo tumezitumia kujenga hospitali moja kwa tulivyozoea nadhani hata robo ya hospitali isingeweza kufikiwa. Naishukuru TAMISEMI kwamba tumepata hospitali ya Wilaya, Vituo vya Afya huko Kilambo, Mahurunga kimekarabatiwa, Mkunwa kinaendelea kujengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado tunayo maombi ambayo yako TAMISEMI ya Kituo cha Afya Mango Pachanne na pia kutokea Msimbati, Madimba, Ziwani, Nalingu mpaka Msangamkuu tunahitaji kupata Kituo cha Afya kingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwa kuamua kutupatia zaidi ya shilingi bilioni 15 kumalizia Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini. Sikupata nafasi kuchangia Wizara ya Afya, nachukua fursa hii kuishukuru sana Wizara ya Afya kwa jinsi inavyosimamia ujenzi ule kupitia National Housing. Nina imani kabisa baada ya mwaka mmoja Mtwara kwa maana ya Mkoa Kanda ya Kusini, Wilaya zetu zitakuwa zimeboresha kwa kiasi kikubwa huduma za afya. Ndiyo maana nasema sina wasiwasi hata kidogo kwamba tutashinda kwa kishindo katika Uchaguzi Mkuu unaokuja, kwa sababu Serikali ya Chama cha Mapinduzi imetekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi, imetatua kero za wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza tena Serikali kwa kutoa mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Kwa kweli imekuwa ni chachu na imeweza sana kuongezea mitaji wanawake wetu, vijana wetu pamoja na watu wenye ulemavu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kutoa mapendekezo kidogo kwa upande wa wenzetu wenye ulemavu hasa maeneo ya vijijini. Tunasema ili wawe na kikundi, wanahitajika wawe angalau 10. Kijiji kingine unakuta labda walemavu wako watatu, wanne kwa hiyo, inakuwa ni ngumu hasa ukizingatia wao ni walemavu. Kwa hiyo, hawezi yeye akasema aungane na mlemavu labda wa Kata nyingine au wa Tarafa nyingine na mara nyingi kikundi ni lazima muwe ni watu mnaofahamiana, mnaoleweana. Kwa hiyo, nawaomba wenzetu TAMISEMI waingalie hiyo Kanuni ili waweze kuirekebisha iweze kupunguza idadi ya wanakikundi hasa kwa wenzetu wenye ulemavu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, TARURA naiomba Serikali iongeze kiwango ambacho TARURA wanapewa kwa ajili ya ujenzi wa barabara. Asilimia 30 wanayoipata kwa kweli ukilinganisha na mtandao wa barabara ambao uko katika maeneo yao ni kidogo sana. Kwa hiyo, tunaomba waongeze kama haiwezekani 50 kwa 50, basi angalau asilimia 40. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na ninarudia tena kusema tutashinda Chama cha Mapinduzi kwa kishindo kikubwa sana. (Makofi)