Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

Hon. Mussa Bakari Mbarouk

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Tanga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge na Utawala na Serikali za Mitaa pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia afya njema na tukawezesha kuendelea na shughuli zetu za Bunge kama kawaida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na suala la TAMISEMI. Kwenye TAMISEMI kuna jambo ambalo limetokea katika jiji letu, hususan katika Halmashauri yetu ya Jiji la Tanga. Kuna Madiwani wamehama kutoka chama kimoja kwenda chama kingine. Ufahamu wangu unanielekeza kwamba moja ya sababu za kupoteza Udiwani ni ikiwa Diwani atahama kutoka chama chake alichochaguliwa nacho kwenda chama kingine; ikiwa Diwani atafungwa zaidi ya miezi sita; na labda akifanya biashara na Halmashauri bila kutangaza interest. Hizo ni baadhi ya sifa za kupoteza Udiwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Madiwani wamehama chama kutoka CUF kwenda Chama cha Mapinduzi, lakini cha kushangaza sasa, sheria haifuatwi. Madiwani wale bado wanaingia katika vikao vya Madiwani, wanalipwa posho na wanalipwa pesa ya mwisho wa mwezi na wanapitisha mpaka bajeti. Sasa je, wakitokea wasamaria wema, wakaenda wakafungua kesi kwamba bajeti hiyo iliyopitishwa siyo halali, si ina maana tutawaathiri wananchi wa Tanga? Kwa sababu itabidi Halmashauri isimamishwe? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka tu kuishauri Serikali. Hili jambo siyo mara ya kwanza. Kipindi cha nyuma kutoka mwaka 2014 kuja 2015 yupo Diwani alifanya mchezo huo huo na akatangazwa na Mkurugenzi kwamba ataendelea kuwa Diwani mpaka mwisho wa kipindi utakapofika na atapewa kiinua mgongo. Sasa najiuliza, sisi hapa kwa imani zetu tunaapishwa hapa…

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Tunaapishwa, tunashikishwa misaafu Waislamu, Wakristo wanashikishwa Biblia…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mussa, taarifa. Mheshimiwa Susan Lyimo.

T A A R I F A

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mussa, taarifa hiyo?

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa hii nimeipokea kwa mikono miwili. Nataka niseme kwamba, narudia tena; Wabunge wote humu ndani kila mtu ana imani yake ya dini. Tunapoapishwa kushika vitabu vya Mwenyezi Mungu, halafu kumbe tunamdhihaki Mwenyezi Mungu kwamba tutaiheshimu, kuitii na kuilinda Katiba ya Jamhuri ya Muungano pamoja na sheria zake, kumbe sisi ni waongo. Tunafikiri Mwenyezi Mungu atatuchukulia hatua gani kwa mambo… (Makofi)

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Mwacheni amalizie. Malizia Mheshimiwa.

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali, wale Madiwani kwa sababu wameshapoteza sifa kwa mujibu wa sheria na Katiba, basi wasihudhurie vikao vya Halmashauri na wasilipwe posho wala wasilipwe kiinua mgongo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ninalotaka kulisema ni uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Kuna mikoa mitano ilitangazwa isifanye uchaguzi wa Serikali za Mitaa kabisa, ukiwemo Mkoa wetu wa Tanga. Athari yake imeanza kujitokeza. Jana wakati tunaangalia taarifa ya habari huu Mkoa wa Dodoma, kipo kijiji wamemkataa Mwenyekiti, wanasema sio chaguo letu.

Sasa je, hatuoni kwamba tunakwenda kuitia hasara Serikali? Kama wananchi wamemkataa ina maana pale lazima uchaguzi urudiwe. Je, likifanyika jambo hilo nchi nzima itakuaje? (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali, ikibidi uchaguzi wote wa Serikali za Mitaa urudiwe, tutende haki tuwape Watanzania haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Waitara, nusu dakika. Haya, Mheshimiwa Waitara.

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

T A A R I F A

MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa yake mimi siipokei, lakini tu niseme kwamba majibu ya taarifa anayonipa ni kwamba waliharibu uchaguzi makusudi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema ina maana kwa maelezo ya Mheshimiwa Waitara wameharibu makusudi ili wananchi waje waandike barua sasa za kuomba eti ifanyike mikutano ya hadhara halafu waangalie asilimia. Huo siyo utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawashawishi Wabunge wenzangu, hasa wa Upinzani, tutakaporudi kwenye Majimbo yetu tuwahamasisheni wananchi wawakatae Wenyeviti wote waliopita bila kupingwa. Nami nawaambia, kama uchaguzi utafanyika haki bin haki, bila ya dhuluma, hakuna Mwenyekiti hata mmoja wa CCM atakayepatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu tufanyeni haki, tuwaache wananchi wachague Wenyeviti wanaowataka. Sasa hivi Wenyeviti hawajulikani na wengine wameanza kulalamika kwamba tumepewa nafasi ambazo wananchi hawatutambui. Huu siyo utaratibu.

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Mussa, umefahamika.