Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili name niweze kuchangia hoja zilizopo mezani za Kamati ya Ardhi Maliasili na Utalii pamoja na kamati ya Kilimo Mifugo na Maji.

Mheshimiwa Spika nitumie fursa hii kuwapongeza Kamati kwa kazi kubwa walizozifanya na Wizara husika kwa kazi kubwa wanaoifanya kupeleka mbele maendeleo ya watanzani.

Mheshimiwa Spika, naomba nitoe dondoo chache katika sekta ya ardhi, maliasili na mifugo; na kama muda utaniruhusu nitaongelea pia suala la maji kwa kifupi sana.

Mheshimiwa Spika, kuhusu ardhi; napenda kuipongeza Serikali kwa dhana nzuri muhimu sana ya kupanga kupima na kuradhimisha kila kipande cha ardhi ya nchi yetu; kwakweli hii dhana ni muhimu sana. Ninachelea kusema kwamba kwa ufinyu wa bajeti ambayo mapato ya ndani inatenga kila mwaka kuwapa Wizara, na kwa uhaba wa fedha za wafadhili na hata za mikopo tunayopata hatutakaa tufanikishe zoezi hili. Ningependa kuishauri Serikali kwamba twende sasa kwenye hatua ya kujiongeza, twende nje ya box kidogo. Tutafute namna nyingine ya kuongeza mapato ili tuweze kukamilisha zoezi hili kwa sababu migogoro ya ardhi haitakaa iishe kama kasi tutakayoendelea kwenda nayo ni hii ya kuhangaika ya urasimishaji wa makazi ambayo yalishazuka kiholelea katika sehemu mbalimbali za nchi yetu. Badala yake twende proactively mbele na kupima ardhi yote ya Tanzania na kumilikisha; tuwahi maeneo kabla hayajavamiwa na watu ambao nao wanazidi kuongezeka na kila siku wanahitaji kujenga.

Mheshimiwa Spika, ingependeza kama ambavyo imeshawahi kufanywa na Bunge hili tukaongeza hata tozo zingine katika baadhi huduma za kijamii na mazao au bidhaa mbalimbali kwa ajili tu ya kuongeza mfuko wa upangaji umimaji na urasimishaji wa ardhi ya nchi yetu .

Mheshimiwa Spika, mimi nilikuwa napenda kuishauri Serikali kwamba Mpango wa Matumizi Bora ya Ardhi ambao unahitajika kwa kasi zaidi kuliko inavyokwenda sasa usipofanya kwa kuweka fedha za ziada katika Wizara hatutafika na migogoro haitapungua. Ndiyo maana migogoro iko kila siku kati ya vijiji na vijiji kata na kata wilaya na wilaya, mkoa na mkoa na hata nchi na nchi.

Mheshimiwa Spika, kwahiyo naomba sana Serikali iende hatua ya ziada ya kutafuta fedha hata katika kuongeza kodi katika baadhi ya bidhaa zinazotengenezwa au kuuzwa au kuletwa nje ili tuweke kodi kama ile ya TDL ambayo iko katika mazao mengine ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, kwenye sekta ya maliasili. Ninapenda kuipongeza kwa kweli wizara hii kwa kazi kubwa wanayoifanya na kwa kuongezeka utalii nchini na kuimarika kwa hifadhi ya wanyamapori; na ndiyo maana hata sasa wanyama wamezidi mpaka wanakuja kurandaranda kwenye makazi ya watu na adha inazidi kuongezeka na kuwa kubwa katika mgongano unaotokea kati ya wanyama na binadamu.

Mheshimiwa Spika, mimi naomba, kwa sababu Wizara sasa hivi inafanya marejeo ya kanuni mbalimbali, katika marejeo inayohusika na suala la kifuta machozi pamoja na suala la kifuta jasho; pamoja na kwamba tunaamini package itaongezeka ili itie matumaini kuna kipengele muhimu ambacho hakipo; suala la majeruhi. Mtu anaweza akajeruhiwa akalipwa laki mbili na nusu lakini majeraha aliyopata anahitaji matibabu ya gharama kubwa na ambayo kile kifuta machozi hakiwezi kugharamia. Kwa mfano katika jimbo langu la Longido mtoto wa darasa la nne aliyekuwa anachunga tu wakati wa likizo aliparamiwa na tembo akaaribiwa mfumo wa mzima wa sehemu zake za siri katika ya miguu. Yule mtoto angekufa, lakini Wizara ya Maliasili na Utalii ilimpeleka Hospitali ya Rufaa ya Seriani; akatibiwa takribani miezi mitatu, gharama ikapanda mpaka ikafika milioni kumi na sita. Mtoto yule angezuiliwa pale mpaka alipe lile deni, lakini kwa sababu ya ubinadamu uliotumika na penda kuishukuru wizara ili bidi wamzamini mtoto akatoka na wizara ikatafuta kila namna tukasaidiana ili yule mtoto alipiwe ile bill.

Mheshimiwa Spika, sasa kwa sababu hakuna sheria na wala haiko kwenye kanuni, ningeomba kanuni ya mafao ya kumtimu majeruhi iongezwe kwenye zili kanuni ili mtoto au mtu anapojeruhiwa lakini hajafa ile 250 tu ya kumfuta machozi haitoshi; ahudumiwe na Wizara wananchi waweze kuthamini hifadhi ya wanyamapori kwa sababu unalipa.

Mheshimiwa Spika, lingine ni kwa upande wa sekta ya mifugo. Sekta ya mifugo kwa kweli; nimeona kwenye ripoti yao; wametia mkazo zaidi kwenye suala la kuaharakisha uwekezaji kwenye viwanda. Tukiwekeza kwenye viwanda ilhali hatujawekeza kwenye malisho, maji, majosho, dawa za tiba na za chanjo pamoja na kuimarisha bei ya masoko ya mifugo tutakuwa hatujafanya kitu. Sawa, viwanda vinaweza vikajengwa lakini, je, kama hatujaweka mbele maslai ya ubora wa mifugo tunayofuga haijawekewa mkazo tutafika kweli? Ninaomba kwamba Serikali ijitahidi kuweka mkazo katika uboreshaji wa afya ya mifugo kwa kuwekeza kwenye maji, malisho tiba na vitu kama hivyo ili tuweze kufanikisha kuvipatia viwanda hivyo rasilimali inayostahili. Ikitokea kwamba viwanda vimekwisha na hatuna ng‟ombe wenye tija ambao viwanda vile vinahitaji wafugaji wetu wataendelea kuwa na adha kubwa ya sehemu ya kuuza mazao yao ya mifugo.

Mheshimiwa Spika, na sambamba na hilo pia niombe Wizara hii ya Mifugo, zile tozo ambazo sisi Wabunge wafugaji tumelalamikia kila wakati ni kubwa. Kabla hatujapata soko la ndani hizo tozo zipunguzwe ili hawa wafugaji waendelee kuuza hata nchi ya jirani wapate hela ya kuendelea ku-support familia zao.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, hivi viwanda vitakavyomalizika na vikaanza kuwa ndio watumiaji wakubwa wa bidhaa ya mifugo tunayozalisha hapa nchini ningeomba bei yenye ushindani itolewe; tusije tukaweka bei bei chini hao wawekezaji wa viwanda wakalaza bei ikawa ni kichocheo cha watu kuendelea kutamani kupekeka mifugo nje ya nchi Tanzania. Tuangalie masoko ya nje, nchi za jirani, tuweke bei ambayo ni sawia ili tuweze kutumia rasilimali ya mifugo kwa utaratibu huo na sisi tukapata faida.

Mheshimiwa Spika, kwenye sekta ya maji mimi nilikuwa nimeona kero moja kubwa sana ambayo iko katika miradi ya maji inayoanzishwa na Serikali; katika wilaya yangu kuna ile ya World bank; unakuta visima virefu vimechimbwa, watu wamewekewa miundombinu stahiki na mashine kubwa za kusukuma maji ku-pump maji lakini wanaachwa wananchi wasio na ujuzi wakaendesha zile mashine; na ndani ya miaka michache generator la milioni 20 unakuta limekufa kwa sababu hawajuwi ni lini oil inabadilishwa.

Mheshimiwa Spika, ningeomba Serikali iwe makini kukaribia hiyo miradi ambayo imeanzishwa waendelee kuwapeleka wataalamu na wawasimamie wanakijiji kamati zile za majizisiachiwe jukumu la kuendasha mitambo ambayo hawana ujuzi nayo maana wanaingia hasara. Sasa hivi sisi katika wilaya yangu tuna visima vingi mwaka huu na mvua imearibu mabwawa yote. Watu watakaa bila maji kwa sababu mashine zimearibika na hakuna utaalamu wa kuzitengeneza na wananchi hawana uwezo wa kununua mashine kama zile zilizowekezwa na Serikali mara ya kwanza.

Mheshimiwa Spika, sambamba hili na mwisho kabisa nipende pia kusema kwamba sisi jamii ya Wana Longido ni wafugaji na asilimia 99 ya maji ya mifugo ni yanatokana na mabwawa, na mabwawa yetu yote; tulikuwa na mabwawa 25 takriban yote ama yamejaa udongo ama yamepasuka. Wizara ya Maji na Wizara ya Mifugo kwa sababu sisi tukipata maji ya mifugo binadamu watatumia hayo hayo…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana…

MHE. DKT. STEPHEN L. KIRUSWA: …tukipata maji ya binadamu mifugo watatumia maji hayo hayo wafanye bidii warudi Longido watusaidie kurekebisha miundombinu ya maji maana hali ni mbaya kweli kweli.

Mheshimiwa Spika ninakushukuru kwa kunipa nafasi, ninaunga mkono hoja zote za Kamati zote.