Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

Hon. Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2019

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kupata nafasi ya kuchangia kwenye hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu. Nichukue nafasi kuwapongeza sana Kamati yetu ya miundombinu kwa taarifa yao ambayo ni nzuri sana, taarifa ambayo kwa kweli kwa ujumla ilikuwa na maelekezo mazuri sana kwa upande wetu sisi Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaongelea kwa haraka sana suala la bandari nitaongelea kidogo na TASAC lakini pia nitaongelea masuala ya usajili wa line kwa alama za vidole. Ni kweli kwamba tumeendelea kufanya maboresho ya makusudi kabisa kwenye bandari yetu ili kuongeza mzigo na kuweza kuuhudumia kama ipasavyo. Tumeendelea kufanya mchakato wa kupanua bandari kwenye gati mbalimbali lakini pia tumeagiza vifaa mbalimbali vya kufanyia kazi ya kupakua mzigo wetu ili tuweze kufanya kazi usiku na mchana pia tuweze kupakua mzigo mwingi kama inavyopaswa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba changamoto za hapa na pale zipo na sisi kama Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari tumeendelea kuwasiliana na wadau mbalimbali na tumekuwa tukifanya vikao mbalimbali kuhakikisha kwamba changamoto za hapa na pale ambazo zipo zinatatuliwa kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kidogo kuhusu suala la TASAC; limezungumzwa sana na Waheshimiwa Wabunge. TASAC ilianzishwa kwa Sheria ya Bunge Na. 14 ya mwaka 2017 na katika sheria hiyo kipengele cha 7(1)(a) kinairuhusu TASAC kufanya kazi ya ku-clear na ku- forward mizigo ambayo ni mahususi exclusivity mandate. Ni kweli kwamba sio kila mzigo unaweza ukawa cleared na kila mtu au kila kampuni, kuna mizigo mbalimbali ambayo kwa kweli iko kiusalama zaidi, ni lazima ichukue wajibu wake wa kulinda hiyo mzigo kuweza kuisafirisha na kuigomboa. Pia ni lazima vilevile tutengeneze mazingira ambapo meli inayokuja ni lazima tujue imeleta mzigo gani kutoka huko ilikotoka na umefikaje hapa ili tuweze kutengeneza utaratibu wa kupeleka maelezo kwa taasisi zinazohusika na bandari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia ni lazima vilevile tutengeneze mazingira ambapo meli inayokuja ni lazima tujue imeleta mzigo gani kutoka huko ilikofika na umefikaje hapa, ili tuweze kutengeneza utaratibu wa kupeleka maelezo kwa taasisi zinazohusika na bandari. Hatuna nia mbaya na wala wale ma-shipping agency hatujawazuwia wanaendelea kufanya kazi zao kama kawaida, hata wale ma-clearing and forwarding wanaendelea kufanya kazi zao kama kawaida na shughuli bandarini zinzendelea kama kawaida. TASAC haijaja kuuwa sekta binafsi isipokuwa imekuja kuimarisha sekta binafsi, lakini pia kulinda rasilimali za Serikali ambazo ni muhimu zilindwe na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niongelee kwa harakaharaka suala la mawasiliano. Ni kweli kwamba, kuanzia tarehe 01Mei, 2019 Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano tulikubaliana kwamba, Watanzania sasa waanze kutumia line zao za simu kwa kusajili kwa alama ya kidole kupitia kitambulisho cha Taifa cha NIDA. Na kwa kweli, mpaka sasa hivi ninapoongea na Bunge lako Tukufu line milioni 31 kati ya line milioni 43 tayari zimekwishasajiliwa kwa alama za vidole kwa kutumia vitambulisho vya NIDA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia line ambazo tayari tumekwishazizima mpaka sasa hivi ni line 6,211,000 na tunaendelea kuzima kwa awamu. Awamu inayofuata wiki ijayo kuanzia Jumatatu ni kuzima line milioni 12 ambazo Watanzania walionazo bado hawajasajili kwa alama za vidole. Tunafanya hivyo kwa lengo zuri la kuhakikisha kwamba, tunawalinda watumiaji wa mawasiliano wawe salama wanapofanya mawasiliano yao au wanapofanya transactions mbalimbali kupitia mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshtushwa kidogo na maelezo yaliyotolewa na Mbunge mmojawapo wa Mtwara hapo kwamba, yeye ameibiwa kupitia Kampuni ya Simu ya Vodacom:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna maelezo kidogo; tunapotumia hizi simu janja za sasa hivi kuna vitu mbalimbali ambavyo vinatusaidia na vinatuletea manufaa katika kutumia hizo simu janja. Watu wanajifunza, watu wanapakuwa document mbalimbali, sasa unapofanya transactions hizo ujue kwamba, kama umeishiwa bundle halafu hujatoka kwenye download hicho kitu unapoweka bundle upya lazima litaendelea kuliwa. Wakati mwingine watu wanapata changamoto kutokana na hivyo, lakini watu wenye zile simu za kawaida walio wengi hatujawahi kusikia changamoto kama hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunawaomba sana Waheshimiwa Wabunge na Wananchi kwa ujumla unapotumia simu janja na unaweka bundle likiisha uhakikishe vile vitu ambavyo umeshaanza ku-download unaviondoa kwenye mfumo wa kuwa-downloaded, ili unapoweka bundle lingine lisiishe kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tunashukuru sana… ahsante sana.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Engineer Nditiye.