Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020 Pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli Zilizotekelezwa na Kamati Hiyo Katika Kipindi cha Mwezi Februari, 2019 Hadi Januari, 2020

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa nami nichangie kwenye hoja iliyotolewa leo asubuhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimelisikia suala la Star Times likiongelewa hapa nikaona ni muhimu sana nilitolee ufafanuzi angalau kwa kifupi kwa sababu tutakuja na ufafanuzi wa kina katika Bunge hili na kwa kutumia njia nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Star Media ambayo ni kampuni ya ubia kati ya Star Times ya China na Shirika letu la Utangazaji la TBC ni suala ambalo liliibuliwa ndani ya Serikali na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano mwenyewe, baada ya kuhoji kwa nini ubia uliodumu zaidi ya miaka saba usioneshe faida?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na kauli ya Mheshimiwa Rais, Bodi ya Wakurugenzi ya TBC ikamwomba CAG afanye special audit, lakini nami vile vile kwa nafasi yangu ya Uwaziri nikaunda Kamati Maalum ambayo iliongozwa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Mkurugenzi wa Maelezo, Dkt. Abbass pamoja na Mtendaji kutoka Star Times nao wafanye uchunguzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliogopa kwamba pengine uchunguzi wa CAG ungechukua muda mrefu sana. Taarifa zote mbili zimetoka na tumeweza kubaini madudu mengi sana katika ubia huo. Madudu yale yenye mwelekeo wa kijinai, tumeyawasilisha kwenye vyombo husika vya Serikali vya masuala hayo. Yale ya kiutendaji tumeyafanyia marekebisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kulitaarifu Bunge hili, kwa mara ya kwanza hata sisi wenyewe tumeanza kuona vitu vimeanza kuonekana positive. Mwaka huu Star Media imeweza kuchangia shilingi milioni 500 Hazina kwa mara ya kwanza. Siyo hivyo tu, mimi nina barua hapa sasa, Star Media imekubali kwa ule upungufu uliojitokeza uliosababishwa na baadhi ya watendaji wake, kulipa TBC shilingi bilioni tatu kuanzia mwezi wa tatu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mambo yanaenda vizuri na tumeyafanyia kazi na taarifa ndefu itatolewa katika Bunge hili na kwa kutumia njia nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)