Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA - MAKAMU MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI YA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushuru kwa kunipa nafasi ya kuhitimisha hoja yangu. Wabunge waliochangia hoja yetu ni Wabunge 14, na kiujumla hoja zao zilikuwa zinalenga katika kutoa msisitizo wa yale ambayo kamati iliwasilisha kama mapendekezo ili baadaye yalidhiwe kuwa maazimio ya Bunge. Kwa muhtasari nitapita hiyo michango yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya kwanza ilikuwa malipo kwa Waheshimiwa Madiwani. Na hii imechwangiwa na Mheshimiwa Lubeleje, Mheshimiwa Msuha na Mheshimiwa Sikudhani Chikambo.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile Mheshimiwa Jafo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI ametoa ufafanuzi jinsi gani ametoa maagizo kwa mamlaka ya Serikali za Mitaa. Lakini Kamati inaendelea kusisitiza kwamba pamoja na maagizo hayo TAMISEMI iendelee kufuatilia ili Waheshimiwa Madiwani walipe kabla ya mabaraza ya kuvunja hayo mabaraza yao. Kwa hiyo, naomba sana TAMISEMI mfuatilie ili ifikapo Juni Waheshimiwa Madiwani hawa wawe wameshalipwa stahili zao zote, posho za mwezi na posho za vikao vyao.

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya pili ambayo wachangiaji wengi wamechangia na imechangiwa vizuri na Mheshimiwa Msuha ni hoja ya dosari katika kanuni ambayo imetolewa na hivi karibu na Ofisi ya Rais TAMISEMI ambayo inasimamia uendeshaji wa mfuko wa wanawake, vijana na walemavu. Hapa kuna changamoto zimeshaanza kujitokeza kwanza kipindi cha kuanza malipo uundaji wa vikundi. Lakini je, mamlaka ya serikali za mitaa zitachangia fedha hizi 10% kwa muda gani?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kuna mamlaka za Serikali za Mitaa zina uwezo mkubwa, kwa mfano juzi tulikuwa Jiji la Dodoma wao wanatenga takribani bilioni 6 kila mwaka. Je watachangia bilioni 6 kila mwaka kwa muda gani? Kwa hiyo, nafikiri Wizara yenye zamana itafanya marekebisha kuhusu kanuni hii kwa sababu ya hii sio Quran au Bible wanaweza kurekebisha kulinga na mapato ya halmashauri husika. Kuna halmashauri zina kipato kikubwa na kuna halmashauri ambazo uwezo wao ni mdogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, Waheshimiwa Wabunge wengi wamechangia kuhusu mashine hizi ya kieletroniki kwa ajili ya kuchangia mapato POS Mheshimiwa Chatanda, Mheshimiwa Msuha, Mheshimiwa Komanya na Mheshimiwa Wambura wamechangia kuhusu hili. Na wameelezea changamoto ambazo zimejitokeza kuhusu PoS ambazo zimenunuliwa huko nyuma kwanza zilikuwa zinachezewa lakini zimenunuliwa kwa bei ya juu. Nichukue nafasi hii kuipongeza Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa tendo la hivi karibu la kutoa bure mashine hizi 7,200 kwa mamlaka ya Serikali za Mitaa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunawaomba sasa TAMISEMI wafuatilie matumizi ya POS hizi na kutatua changamoto ambazo zitajitokeza. Naomba Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi iimarishe mitandao katika mamlaka ya Serikali za Mitaa zilizopo pembezoni ili basi mashine hizi ziweze kutumika kwa ufanisi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna suala lingine ambao Wabunge wengi wamelichangia suala la Forces Account. Wachangiaji wote wamekubaiana na maoni ya kamati kwamba Force Account imeonyesha mafanikio makubwa sana tunajenga vituo vya afya, hospitali za wilaya kwa gharama nafuu na kwa ubora ambao ukubalika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ambayo hata sisi kwenye kamati yetu tumeisisiza kwamba kuna upungufu wa wataalam wa ujenzi (waandisi). Kwa hiyo, kama huko nyuma ilivyofanya ajira maalum kwa wahasibu basi kwa kuwa ma-engineer wengi wamehamia TARURA naomba Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais Utumishi watoe kibali cha ajira maalum kwa ajili ya watumishi hawa wa kitengo cha ujenzi ili miradi hii isimamiwe ipasavyo. Lakini kwa ujumla force account ni mkombozi kwa fedha za umma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya tano ambayo Wabunge wengi wamechangia ni kuhusu miradi ya kimkakati, na kipekee nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Rais na Wizara wa Fedha na Mipango kwa ubunifu huu mkubwa kwa kuzianzishia mamlaka ya Serikali za Mitaa miradi ya kimkakati. Miradi hii ikikamilika itapunguza utegemezi wa halmashauri kwa Serikali Kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, ushauri wa kamati kama tulivyotoa kwenye Kamati yetu, kwanza Ofisi ya Rais, TAMISEMI miradi hii inakaribia kukamika sasa hivi, tumetembelea Soko la Job Ndugai hapa Dodoma, tumetembelea Dodoma Bus Terminal. Lakini kuna soko kubwa linajengwa pale Morogoro, miradi hii sasa naomba Ofisi ya Rais, TAMISEMI iweke utaratibu maalum wa kuikabidhi kwenye Serikali za Mitaa na namna yakuziendesha ili ilete tija. Tumeambiwa hapa soko la Ndugai na ile Dodoma Bus Terminal miradi hii ikikamilika itakusanya bilioni 18 kwa mwaka. Huu ni ukombozi mkubwa kwa mamlaka ya Serikali za Mitaa na itapunguza utegemezi kwa Serikali Kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ombi letu la pili kwenye kamati tumezungumzia suala la viwango kwa sababu suala hili la kimkakati fedha zimetoka hazina kama ruzuku. Basi tuhakikishe viwango tutakavyoviweka vya tozo viwe rafiki kwa wananchi wetu tusiweke viwango vikubwa na miradi hii ikakimbiwa na wafanyabiashara. Tujifunze lile funzo ambalo limetokea soko la Mwanjelwa kule Mbeya wameweka viwango vikubwa na wafanyabisha wadogo wamekimbilia lile soko. Ni matarajio yetu Ofisi ya Rais, TAMISEMI itasimamia vizuri na miradi hii ya kimkakati ikawa na manufaa kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema wachagiaji wote hakuna aliyepinga hoja ya kamati, walikuwa walikuwa-qualify au wanasisitiza kile ambacho kamati imekifanya. Kwa hiyo, nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa jinsi anavyosimamia Mamlaka ya Serikali za Mitaa na jinsi alivyoongeza usimamizi wa fedha za umma na jinsi anavyoelekeza matumizi ya fedha za Umma kwa Mamlaka ya Serikali za Mitaa. Ni matarajio yetu kwamba speed hii itaendelea na mwenye macho haambiwi tazama kuna mabadiliko makubwa sana kwenye mamlaka ya Serikali za Mitaa sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maelezo hayo sasa nikushukuru wewe kwa jinsi ulivyoendesha mjadala wa Kamati yetu. Niombe sasa maapendekezo yetu tisa ya kamati ambayo tumewasilisha naomba sasa yawe maazimio ya Bunge lako tukufu yote tisa tuliyowasilisha yapitishwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, naafiki.