Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kwa Mwaka 2019 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kwa Mwaka 2019

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuchangia katika taarifa iliyowasilishwa ya LAAC pamoja na PAC kwanza naziunga mkono. Nampongeza Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kwa namna alivyofanya kazi ya kuboresha na kuzisambaza PoS za kukusanyia mapato ambayo PoS hizi zinaweza kuzisaidia sana Halmashauri zetu kudhibiti wizi wa mapato katika halmashauri zetu, amefanya kazi kubwa tunamshukuru sana na tunakusudia sasa kuona kwamba kwenye halmashauri zetu mapato yataongezeka kutokana na vitendea kazi ambavyo vimepatikana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yapo mambo mengi ambayo tumeyazungumza na wenzangu wameshayazungumza katika Kamati yetu ni pamoja na suala zima la ajira za watumishi. Tumejenga vituo vya afya, tunajenga zahanati, lakini kumekuwa na upungufu mkubwa wa watumishi katika vituo hivyo vya afya na zahanati. Jambo ni jema sana na tunaishukuru sana Serikali kwa kazi kubwa ambayo imeifanya kwa ajili ya kujenga hizo hospitali tunazojenga, tunajenga hivi vituo vya afya, tunajenga hizi zahanati lakini sasa tuna uhitaji mkubwa watumishi katika maeneo hayo. Kwa hiyo tuiombe sana Serikali angalau basi waweze sasa kutoa ajira ili kusudi hospitali hizi na zahanati hizi ziweze kufanya kazi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yako mambo mengi ambayo yamezungumzwa ni pamoja na suala zima la kutumia hii force account, ni jambo jema sana na linaisaidia sana Serikali katika kubana matumizi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa, vituo vya afya na hospitali zetu na mambo mengi ya maendeleo. Hata hivyo, kama walivyosema wenzangu kwamba tunahitaji sasa Wahandisi katika halmashauri zetu maana Wahandisi waliokuwepo wakati huo wote wamechukuliwa, wako asilimia kubwa wamekwenda sasa TANROADS, wamekwenda TARURA. Sasa mara nyingine wanaenda kuwachukua TARURA au kuwaomba waje kuwasaidia kazi, inakuwa ni kazi kubwa sana katika kusimamia hii miradi ambayo tunatumia force account. Mradi wenyewe wa force account ni mzuri lakini tunahitaji watendaji angalau wale watakaokuwa wapo muda wote kuhakikisha kwamba wanasimamia hii miradi katika halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka nilizungumzie ni suala la watumishi. Tumegundua kwamba watumishi wanapandishwa madaraja lakini wanapopandishwa madaraja hawaendi sambamba na maslahi yao. Wakishapandishwa tu basi mtu anaweza akakaa mwaka mzima, miaka miwili haongezewi yale maslahi ambayo yanahusiana na kule kupandishwa kwake daraja. Kwa hiyo, naiomba sana Serikali, ili kuwapa motisha wafanyakazi hawa anapopandishwa basi aende sasa na maslahi yake kwa nafasi ile ambayo amepandishwa nayo daraja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu mengi yamezungumzwa nilikuwa nafikiri ni vizuri nikasema haya machache kwa sababu wenzangu wengi waliotangulia ambao tuko kwenye Kamati hii ya LAAC wamekwishayasema, hivyo nishukuru na niendelee kuipongeza sana Serikali kwa juhudi kubwa ambazo wameendelea kuzifanya katika kuyaletea maendeleo nchi yetu. Ahsante sana. (Makofi)