Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

Hon. Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa utendaji uliotukuka kwa kipindi cha miaka minne ya Uongozi wake

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii. Niseme tu kwamba, umetumia Busara sana sana kutujumuisha sisi Wabunge ili tumpongeze Mheshimiwa Rais kwa kazi nzuri sana anayofanya. Nimemsikiliza mtoa mada kwa kweli mambo ambayo ameyasema ni mengi sana, sitaki niyarudie, lakini endapo kuna Mtanzania au Mbunge hatayaona haya au hayasikii haya kule porini, kuna mnyama mmoja anaitwa ngiri, ngiri hana kumbukumbu hata kidogo, hata ukimfaa namna gani hana kumbukumbu na ndiyo maaana wawindaji kule porini, anapotoka porini akienda kwenye shamba la mahindi au la mihogo, kuna mwindaji atamkosa kosa risasi lakini speed yake atakayotokanayo hapa ni kama kilomita mia moja kwa saa, atafunga break. Akifungu break atasema hili nilipokoswa koswa ilikuwa jana au juzi. Atasema ilikuwa juzi, anarudi tena kwenye shamba, atakoswakoswa tena atakimbia mbio, atasimama, atasema hii ilikuwa jana au juzi. Ni kwa sababu mnyama huyu ngiri hana kumbukumbu.

Mheshimiwa Spika, haya yote na ndiyo maana Bunge lako Tukufu kwa kazi nzuri sana inayofanywa na Mheshimiwa Rais wetu na kila mtu ana macho na masikio, lakini hata kama hujui kusoma basi hata kuangalia picha inakushinda. Niombe sana Watanzania tumpe moyo Rais wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu, niwaombe watendaji wa Serikali kwamba ni lazima tukimbie na spidi ya Mheshimiwa Rais wetu ili matarajio yake aliyonayo kwa Watanzania yaweze kufikia hapo anapotaka. Haipendezi sana Mheshimiwa Rais mpaka anafikia mahali aseme hivi ninyi haya hamyaoni mpaka mimi niingilie kati? Kwa hiyo, ili tufike huko tunakotaka kwenda, niwaombe sana watendaji, spidi ambayo wewe unayo na Bunge lako, na watendaji wa Serikali nao lazima wafanye hivyo ili tufikie malengo yetu ambayo tunayataka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho; niombe sana wenzangu, Wabunge wa upande wa pili, nchi hii ni yetu sote, na Rais huyu ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hatuna sababu ya kuanza kufika mahali na kuanza labda kumbeza, vinginevyo utakuwa unajibeza wewe mwenyewe uliyeko humu ndani. Lakini wananchi walio wengi wa Tanzania kwa sasa wameshamuelewa Rais wetu kwamba anataka kuwafanya nini, hasa wanyonge wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja azimio hili. Ahsante sana. (Makofi)