Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga na Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (The East Africa Community Protocol on Information and Communication Technology)

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Kuridhia Itifaki ya Kinga na Maslahi ya Kidiplomasia ya Jumuiya ya Afrika Mashariki pamoja na Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (The East Africa Community Protocol on Information and Communication Technology)

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi niweze kuchangia kidogo kwenye hii Protocol ya Afrika ya Mashariki. Maudhui yameshazungumzwa kwamba nini maudhui ya Itifaki hiyo, ninayo maeneo ambayo ningependa kupata ufafanuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kutatua migogoro tumesema tutaridhiana na kuzungumza na kama ikishindikana tunakwenda Mahakama Kuu ya Afrika Mashariki nauliza Je, kama tuna migogoro hao Ma-judge wa hiyo Mahakama hawatakuwa na allegiances na Nchi Wanachama na hivyo kutoweza kutatua tatizo ambalo linatukabili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa nafikiria hili ni jambo ambalo tunaweza kulifikiria na pengine kutafutia ufumbuzi mwingine. Vilevile kuna hili suala la wale waliokuwa wanafanya kazi East Africa ambalo limezungumzwa hapa ambao mpaka leo wanadai mafao yao, ningependa kupata kauli ya Serikali kwamba ina mpango gani kuhakikisha hao wanalipwa mafao yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu inahusu pia Itifaki ambayo imeasainiwa na nchi wanachama wote isipokuwa Sudani ya Kusini, yenyewe haijasaini hii Itifaki mpaka leo, na bado wanapta benefits zote za East Africa wakati wao hawajasaini Itifaki hii, pamoja na kwamba wamesaini Vienna Convection, hata sisi pia tumesaini Vienna Convection lakini tumeridhia Itifaki hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni Serikali yetu au Jumuiya ya Afrika Mashariki ina Mkakati gani kuhakikisha kwamba na wenyewe hawa wanasaini hiyo Itifaki Mheshimiwa Waziri, nafikiri ni hayo matatu ambayo nimeyaona na ningepata kupata kauli ya Serikali ahsante. (Makofi)