Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai kwa Uamuzi wake wa Kulifanya Bunge Kutekeleza kwa Vitendo Dhana na Bunge Mtandao (e-Parliament)

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Yustino Ndugai kwa Uamuzi wake wa Kulifanya Bunge Kutekeleza kwa Vitendo Dhana na Bunge Mtandao (e-Parliament)

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nachukua nafasi hii kukushuru, lakini vilevile kumpongeza Mheshimiwa Spika, kwa uthubutu aliouleta ndani ya Bunge hili na Taifa letu kwa kukubali sasa Bunge liwe Bunge Mtandao kwa jina lingine e-Parliament. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika dunia kuna tathmini zilizofanywa na audit ya World Bank, Tanzania ni nchi ya tano kwa kasi ya kukata miti; na hii ni hatari sana kwa nchi yetu. Miti inayokatwa Tanzania sasa hivi ni kiwango cha kilometa za mraba 15,000 na kwa hatua hii ya Mheshimiwa Spika na hatua ya Serikali na wao vilevile kuingia katika Mtandao e- Government, tutapunguza athari ya mazingira kwenye Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru mtoaji taarifa, ametupa taarifa kwamba, sasa hivi Serikali itaokoa zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa mwaka katika nyaraka mbalimbali zinazotumika na Serikali kuja Bungeni. Hii ni hatua kubwa sana ya kupongezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Spika, naomba vilevile kutoa wazo kwa Bunge hili na mamlaka zinazohusika, kwa kutumia fursa hii ya e-Parliament tunaweza sasa vile vile tukapata fursa ya kutumia maswali kwa online questions za Wabunge wakajibiwa online na Wabunge wakaweza kutumia maswali haya kupeleka kwa wapigakura wao kwenye Majimbo, kwenye ma-group ili nao wakajua kazi anayofanya Mbunge Bungeni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo kila mtu anapata fursa ya kuuliza maswali ndani ya Bunge. Kwa hatua hii na kwa siku za mbele, lazima Bunge litakuwa live katika masuala ya mitandao na wananchi watajua wawakilishi wao ndani ya Bunge wanafanya nini na kutekeleza majukumu yao ya Kibunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii tena kumpongeza Mheshimiwa Spika kwa kazi nzuri aliyoifanya. Hongera Mheshimiwa Spika, hongera Serikali, hongereni Bunge. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naunga mkono hoja. (Makofi)