Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa FAO wa Kuzuia Uvuvi Haramu kupitia Bandari za Nchi Wanachama pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kuanzishwa kwa Ushirikiano wa Kimataifa wa Nishati ya Jua (The Framework Agreement on the Establishment of International Solar Alliance)

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa FAO wa Kuzuia Uvuvi Haramu kupitia Bandari za Nchi Wanachama pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kuanzishwa kwa Ushirikiano wa Kimataifa wa Nishati ya Jua (The Framework Agreement on the Establishment of International Solar Alliance)

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mimi nitabaki katika hili suala la solar power agreement ambayo imesainiwa miaka michache tuliyopita, lakini nimefurahi kwamba nchi yangu ilikuwa katika nchi za mwanzo na leo hata muda haujapita sana linaletwa Bungeni turidhie. Kwa kweli tumekuwa tukipitwa na maazimio mengi ya kimataifa lakini hili limekuja haraka sana. Nitafurahi spirit hii ya kukipitisha maazimio haraka inavyowezekana ikiendelea.

Mheshimiwa Spika, la pili ni kwamba jana na juzi nilisema kwamba Mungu ameiweka Tanzania kwa makusudi yake. Katika mfano huu wa solar ni kwamba ametuweka katika maeneo kati ya tropical of cancer na tropical of Capricorn ambayo inatajwa katika mkataba huo na katikati inapita IKweta. Kwa maana tumewekwa kwenye sunshine state kama inavyotajwa, na kama anavyosema Narendra Modi wa India. Kwamba tuko katika eneo ambalo jua ni 12 seven, lakini tunalitumiaje? Jua liko wakati wote na liko takriban nchi nzima; sasa tunalitumiaje ndiyo muhimu; kwa hivyo tumekuwa katika pahala ambapo sasa hivi tuna fursa nzuri sana. Nchi ambazo jua si wakati wote kama Ujerumani bado ni katika nchi 10 duniani ambazo zinaongoza kwa solar.

Mheshimiwa Spika, nchi kama ya Norway jua ambalo si siku zote lakini bado inaongoza kwa solar, sembuse sisi ambapo asubuhi mpaka jioni jua.

Mheshimiwa Spika, kikundi hiki cha International Solar Power Agreement sasa hivi ni kundi kubwa la pili la nchi za Kimataifa zinazokutana baada ya Umoja wa Mataifa. Kwa hivyo ni eneo ambalo linakua haraka sana na nafikiri takwimu za mwisho labda kama signatories kama 121 tayari mpaka hivi sasa, kwa hivyo ni kundi kubwa. Hata hivyo si kundi kubwa kwa jina tu, ni kundi kubwa kwa dhamira; kwa sababu kuna mipango mingi ya kufanya ili kuiokoa dunia, linalofanywa hapa ni kujaribu kuiokoa dunia. Ndiyo maana wanataka tufanye kila njia ili tuache kutumia fossil energy badala yake tutumie energy ambayo ni renewable, kwa hivyo sisi tusiiache fursa hii.

Mheshimiwa Spika, nasema tusiiache kwa sababu nina experience, kwamba labda pengine kwa hii sasa kutakuwa na mabadiliko; na ningependa Mheshimiwa Waziri wa Uwekezaji anisikilize katika hili.

Mheshimiwa Spika, na narudia tena hapa Bungeni niwahi kupata ofa ya wawekezaji ambao wako tayari kuwekeza three billion dollar’s kwa ajili ya three thousands megawati za umeme nikataabishwa, nikasumbuliwa mpaka yule muwekezaji akakata tamaa. Hivi sasa nasema, pengine Mheshimiwa Waziri ananisikia, kwamba nina offer nyingine ya mtu ambaye yuko tayari kuwekeza vituo zaidi ya 50 vya solar kwa ajili ya magari, kwa ajili ya vyombo vya umeme, kwa pesa zake; I mean ni self financing. Kwa hiyo kama Serikali watakuwa tayari huu ndio mwanzo mzuri, tunaanza kidogo kidogo ku-phase kwenye petroleum tunaingia katika vitu vingine. Kwa hiyo ningependa baadaye nikae nizungumze na Mheshimiwa Waziri tuone tatafanya kitu gani.

Mheshimiwa Spika, lakini pia ni njia nzuri ya energy mix tunalalamika kila siku juu ya energy mix. Wengine tulisema sana hapa juu ya umeme wa Julius Nyerere; lakini kusema kweli tulikuwa na ushindani. Wengine tunasema kwamba umeme wa solar ni rahisi zaidi, wengine wanasema umeme wa maji rahisi zaidi, lakini namna ya uwekezaji wenyewe. Sasa hivi kumepatakana solution, hawa walioko mbele, kwa mfano India, wao wametenga three fifty billion dollar’s kwa ajili ya kuzisaidia nchi kufanya kazi hii. Pia World Bank wao wanatarajia kuhamasisha uwekezaji wa takriban bilioni 1000 mpaka kufikia 2030 ili nchi zote ambazo zina fursa zipo katika sunshine area ziweze kunufaika. Kwa hiyo sisi tusikae nyuma sasa maadam tulishaingia katika uwanachama huu na tuna fursa.

Mheshimiwa Spika, Dodoma peke yake hapa ikitumika, maeneo ambayo hayafai kwa kilimo, maeneo ambayo hayaoti miti basi tunaweza tukatoa megawati kwa mamia kabisa sembuse nchi nzima, kwa hiyo tutumie fursa hiyo kwa vizuri.

Mheshimiwa Spika, lakini pia sasa hivi kuna nchi; kwa mgano Venezuela, ambazo tayari zinaweza kufikia 100 percent sasa ya mahitaji yao. Kwa hivyo sisi tusiona kwamba Julius Nyerere kama tumefika kwa zile megawati 2000 na ushehe. Bado nchi hii kama tunataka kweli kwenda kwenye viwanda tuondokane na dhana, kama alivyosema Mheshimiwa Mbarouk, ya kuona umeme wa jua si umeme kitu. Umeme wa jua ni umeme kama umeme mwingine na unaweza kuuzalisha viwandani na unaweza ukatumika sehemu nyingine nyingi hata hapa Bungeni.

Mheshimiwa Spika, imagine hapa jua linalopiga kutwa nzima katika paa la nyumba hii na namna paa yaliyopo humu ndani kiasi ambacho pengine tukiweka solar tu humu ndani ya Bunge tunaweza tukakoa mamilioni ya fedha. Kama vile ambavyo tumeokoa karatasi kwa kwenda kwenye tablets na huku tunaweza tukaokoa pesa tukatumia renewable energy lakini pia tukaokoa fedha nyingi kwa kuitandika solar power eneo lote la Bunge au eneo lolote lingine ambalo umeme wake utakuja mpaka Bungeni. Kwa hiyo mimi nasema katika hili Tanzania tusikae nyuma…

SPIKA: Mheshimiwa Ally Saleh nilitaka kukubaliana na wewe katika eneo la Bunge kutumia solar power. Niliwahai kutembelea Bunge la Israel wanatumia 1005 umeme wao kwenye Bunge la Israel solar power. Endelea tu Mheshimiwa. (Makofi)

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Spika, fahari kubwa kukubaliwa wazo langu. Kwa hivyo mimi nafikiri Bunge lioneshe mfano kwamba hiki kinawezekana na taasisi za Kiserikalia kwa mfano Mji wetu wa Mtumba utandikwe solar, inawezekana kufanya, ili Serikali iwe mfano na ili tuwe tunaweza kujiendesha wenyewe kidogo mpaka hapo ambapo wakubwa wa dunia watakapotuona na kuwekeza katika maeneo haya; kwa sababu umeme utaendelea kuhitajika kwa sababu tunasema tunataka Tanzania ya viwanda ahsante sana. (Makofi)