Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa FAO wa Kuzuia Uvuvi Haramu kupitia Bandari za Nchi Wanachama pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kuanzishwa kwa Ushirikiano wa Kimataifa wa Nishati ya Jua (The Framework Agreement on the Establishment of International Solar Alliance)

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa FAO wa Kuzuia Uvuvi Haramu kupitia Bandari za Nchi Wanachama pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kuanzishwa kwa Ushirikiano wa Kimataifa wa Nishati ya Jua (The Framework Agreement on the Establishment of International Solar Alliance)

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru nami kupata nafasi hii ya kuchangia kwenye itifaki hii. Kwanza niseme kwamba naunga mkono na ninaomba Wajumbe mbalimbali tuweze kuiridhia itifaki hii ya FAO ambayo sasa inatupeleka na sisi kutuunga miongoni mwa nchi ambazo zinanufaika katika itifaki hii kwa wale waliokuwa wameanza kuridhia. Sisi tumechelewa.

Mheshimiwa Spika, hasara ya mwanzo ambayo inatokana na kutokuridhia kwetu, Tanzania imekosa siyo chini ya dola za Marekani 184,000 ambazo zilikuwa ni fedha maalum za nchi ambazo zinapitiwa na bahari upande wa mashariki na hasa zile ambazo zinatumika kupitishia meli kubwa zinazomwaga dawa na sumu mbalimbali katika eneo letu. Kwa hiyo, eneo letu limekuwa linaathirika sana na watu ambao wanafanya biashara ya kutupa uchafu mbalimbali hasa wa sumu katika eneo letu, lakini sisi kwa kutokuridhia mkataba huu, tumeshindwa kutetewa au kulindwa kwa pamoja na wale waliokuwa wameridhia mkataba huu.

Mheshimiwa Spika, la pili, tunaingia miongoni mwa nchi ambazo zitakuwa zina ule mpango, routine research na monitoring ya meli zile ambazo zinaingia katika mkumbo wa meli ambazo zinaitwa za eneo la Indian Ocean and Pacific, ambapo tutakuwa tunapata takwimu sasa za fish stock karibu kila baada ya miaka mitatu katika eneo letu hili la bahari kuu.

Mheshimiwa Spika, lingine mabalo linanufaisha; Tanzania pamoja na kuwa na ukubwa wa eneo la mita za mraba laki mbili, tulizoziongeza hizo la uvuvi wa uvuvi wa bahari kuu, lakini tumeomba tena eneo lingine tuongezewe la zaidi ya nautical miles 150,000. Kwa hiyo, tunakwenda kuwa na eneo kubwa zaidi la uvuvi wa bahari kuu au eneo la bahari kuu ambalo tunatakiwa sisi wenyewe tuweze kulilinda, tuweze kulitumia na litunufaishe kama ni sehemu ya rasilimali.

Mheshimiwa Spika, sasa huwezi kuwa na eneo kubwa kama hili halafu ukasema kwamba wewe huungi mkono wenzako ambao wanatumia vyombo mbalimbali kuweza kulilinda eneo hilo. Kwa hiyo, tukiridhia, hizo ni moja kati ya faida ambazo tutazipata.

Mheshimiwa Spika, lingine ambalo linakwenda kutupeleka sasa hivi, ni kwamba Serikali na mtazamo wa watu mbalimbali, tumeomba hapa kwamba, nchi hii iwekeze kwenye uvuvi wa bahari kuu. Tukiwekeza kwenye uvuvi wa bahari kuu na sisi sasa tunakuwa miongoni mwa nchi ambazo zinaingia kwenye ile wanaita Tuna World Market; Soko lile la Japani, kuna Soko la China na Soko lile la Norway, ambapo nasi tutapata fursa ya kuweza kuuza samaki wetu katika masoko ya nje.

Mheshimiwa Spika, faida nyingine ambayo imejitokeza hapa, ni kwamba zile meli ambazo tutazikamata zikichafua mazingira katika eneo letu la bahari kuu, tutaweza kupiga faini au kuweza kuzilipisha faini za uchafuzi wa mazingira pale kisheria, kuliko kusema kwamba tunatumia sheria zetu za ndani, kitu ambacho wale wanaotumia sheria za nje, hatuwezi kuwabana na baada ya kufanya huo uchafuzi wanakwenda zao, kwa sababu hakuna kitu au hakuna mkono wa sheria unaowakamata na kuweza kuwaadhibu kwa vitendo ambavyo wanatufanyia.

Mheshimiwa Spika, la mwisho katika faida ambazo zinapatikana, ni kulindwa katika ile wanaita Ocean Biological Weapons, ambapo katika eneo letu la bahari kuu huweza kutumika kwa uhalifu wa kibiolojia. Katika njia mbalimbali ambazo wenzetu nchi za nje zinatumia uharamia huo, eneo letu litakuwa linalindwa na vifaa maalum, zile VMS, maalum za Kimataifa kupita satellites na chochote kitakachopita katika eneo hilo kwa nia ya kufanya uhalifu wa kibiolojia, kisheria zitaweza kuchukua mkondo wake.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nawamba Waheshimiwa Wabunge wa Bunge hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, turidhie, kwa sababu tukiridhia na sisi tutapata faida ya kuwemo miongoni mwa hao watu ambao ni wanufaika wa mkataba huu.

Mheshimiwa Spika, mwisho kabisa, nawaomba Serikali kwa upande mwingine, tuweze kushiriki baadhi ya mikutano na makongamano ambayo yanakwenda kutunufaisha na miradi mbalimbali ya kimazingira katika eneo letu. Bado tu tuendelee kuwakumbusha Watanzania kwamba, asilimia 67 ya tuna ambao wanaliwa duniani au wanaoingia katika Soko la Dunia, wanatoka katika belt hii ya Tanzania ambapo ni eneo lile la Kizimkazi mpaka Kitutio kule Mafya.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, fursa hii iliyokuweko duniani mwote, tunaweza kusambaza samaki duniani, tuweze kuilinda na kuitunza. Ni kitu ambacho kwa kweli hakiwezi kupatikana, yaani faida yake haiwezi kupatikana kwa miradi mingine yoyote. Bado tuikumbushe Serikali kwamba eneo hili tukiwekeza, hakuna cha dhahabu, hakuna cha bidhaa nyingine yoyote itakayoweza kuishinda hii blue sea kwa kipato. Kwa hiyo, nawataka wadau mbaimbali, wawekezaji mbalimbali, waje tukae na Serikali, tuangalie uwezekano wa kuwekeza katika eneo hili la uvuvi wa bahari kuu.

Mheshimiwa Spika, siyo hilo tu, fursa nyingine ambayo tunaipata sasa Tanzania, baada ya kuondoa ile 0.4, nampongeza sana Mheshimiwa Waziri kwa hatua kubwa aliyoifanya na kuridhiana na wenzie wa Zanzibar na kuweza kumaliza tatizo lile la 0.4, sasa tunakwenda kurudisha leseni za uvuvi wa bahari kuu, na kuifanya Mamlaka ile ya Uvuvi wa Bahari Kuu kuwa na kipato cha ajabu sasa hivi. Kwa sababu, pending ya meli ambazo zinakaa zinagoja kufanya uvuvi wa bahari kuu ni zaidi ya 200 zinangoja leseni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, issue ilikuwa ni 0.4, Serikali imesikia kilio cha wadau, imekiondoa kwa muda hivi. Nami nasema kwamba, tukiweke pembeni, ili tuweze kupata faida ya meli zile ku-land katika maeneo yetu au kubaki katika maeneo yetu, ambapo kila meli itaweza kuacha zaidi ya shilingi milioni 40, ikija kutua katika maeneo yetu.

Mheshimiwa Spika, vilevile tusisahau; tujiandae sasa na kufaidika na by-catch ambazo zitakuja katika maeneo yetu, ambazo zitaziba gap lile la upungufu wa samaki, ambao wanahitajika kwa kupunguza lishe na utapia mlo uliokuweko hapa nchini. Ahsante sana. (Makofi)