Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa FAO wa Kuzuia Uvuvi Haramu kupitia Bandari za Nchi Wanachama pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kuanzishwa kwa Ushirikiano wa Kimataifa wa Nishati ya Jua (The Framework Agreement on the Establishment of International Solar Alliance)

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kimataifa wa FAO wa Kuzuia Uvuvi Haramu kupitia Bandari za Nchi Wanachama pamoja na Azimio la Bunge la Kuridhia Mkataba wa Kuanzishwa kwa Ushirikiano wa Kimataifa wa Nishati ya Jua (The Framework Agreement on the Establishment of International Solar Alliance)

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii, nami niweze kuchangia katika itifaki hizi mbili. Moja, nitachangia ya solar energy na pia nitagusia kidogo kwenye hii ya PSMA ya FAO.

Mheshimiwa Spika, hii itifaki ya International Solar Alliances, tuliisaini mwaka 2015, tukiwa na ule Mkutano wa Climate Change, Paris, mwaka 2015 na sasa imeletwa turidhie. Tumeona kwamba baadhi ya nchi, kwa mfano India ambao pia waliridhia mkataba huu, wao wamefika mbali sana katika kutekeleza huu mkataba na kuanza kutumia energy hii ya solar ambayo ni muhimu sana; kwa sababu kwanza inafika vijijini, ambako energy nyingine ya umeme haifiki na vilevile ni energy ambayo ni safi kuliko tunavyoona kwenye energy nyingine ambazo zinaleta carbon monoxide katika mazingira.

Mheshimiwa Spika, sasa napendekeza kwamba, huu mkataba tumeusaini na ingekuwa ni vizuri vilevile kuhakikisha kwamba tunakuwa na mpango mkakati. Tumepitisha itifaki nyingi hapa na sijui Bunge lako Tukufu ni kwa jinsi gani linafuatilia hizi itifaki ambazo tunazipitisha hapa kuona kwamba zinatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, vilevile mradi huu utaongeza tija kwa wanavijiji na kuboresha maisha yao na kuwa na umeme wa kuwasaidia kuzalisha na kuongeza pato lao la nchi. Kwa hiyo, napendekeza kwamba, kuwepo na mpango mkakati na Waziri atueleze utakuwa vipi, ni kwa jinsi gani sasa, tuna solar energy na tuna REA? Tuone ni jinsi gani atajipanga, aweze kutekeleza hizi energy zote kwa pamoja; ya REA na Solar.

Mheshimiwa Spika, nitafurahi sana kama atakapokuja atatupa tu taarifa ni kwa jinsi gani hizi energy zote zitakwenda kwa pamoja? Kwa sababu tunajua REA nayo inakwenda vijijini na hii solar pia inakwenda vijijini; na solar ni rahisi zaidi kwa sababu haihitaji miundombinu mikubwa other than hizi solar panels na miundombinu mingine midogo midogo na jua tunalo kila siku. Kwa hiyo, nilikuwa nafikiri kwa mawazo yangu, itakuwa ni gharama nafuu zaidi kutekeleza hili la solar energy, sambamba na REA vilevile.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye suala ya ile itifaki nyingine ya kuzuia uvuvi haramu kwenye deep seas; ni vizuri tukaridhia huu mkataba, kwa sababu, kwanza kutakuwa na msaada, kwa sababu, bajeti yetu kama tunavyojua haikidhi mahitaji. Tutakuwa na bajeti ya msaada ambayo tutaitumia kwa ajili ya kujenga uwezo wa watu wetu na vilevile kulinda rasilimali yetu ambayo ni muhimu kama Wabunge wengine wengi walivyochangia. Siyo hivyo, kulinda rasilimali pia. Hata meli zinazokuja, zita-generate income ambayo itaingia katika mzunguko wa fedha.

Mheshimiwa Spika, tunajua jinsi ambavyo uvuvi haramu umekithiri. Kwa hiyo, kwa kuridhia huu mkataba, tutasaidia kulinda rasilimali zetu zisiweze kupotea na badala yake tuweze kupata fedha zika-generate revenue ambayo tutaweza kuendelea katika maisha yetu na kujenga uchumi wetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hayo machache, ninaipongeza Serikali kwa kuleta hizi itifaki hapa mbili tuziridhie na tuwe na monitoring system; hiyo ndiyo concern yangu kubwa. Tuna-monitor vipi sisi Bunge, kwamba hizi itifaki tunazopitisha hapa kila siku, zinafuatiliwa na zinafikia wapi? Maana yake, tunapimaje utekelezaji wa hizi itifaki? Ahsante. (Makofi)