Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia. Nakubaliana na niishukuru Serikali kwa kuleta haya maazimio, maazimio yote matatu mimi nayaunga mkono.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wanazungumza viingereza virefu sana hapa, lakini ukweli ni kwamba dunia hapo inapokwenda sasa ni hatari zaidi. Na nchi yetu, ukiangalia katika zile nchi 10 za Afrika ambazo ziko, wanasema most likely to be destroyed by climate change, Tanzania ni nchi ya 10. Na kila nchi imepewa sababu zake za kutoweka; sisi tumepewa sababu za kutoweka kwa mambo ya mafuriko na ukame, floods and drought.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasa kama hivyo ndivyo ilivyo, sisi tumeshaambiwa kwamba climate change ni jambo la kidunia, na ozone layer 0.003% imeshaharibika na uwezo wa kuirudisha ni mgumu sana kwa sababu nchi za Ulaya ambazo zinatumia viwanda vingi vinavyosababisha mambo ya greenhouse gases zinakuwepo; carbon dioxide, nitrus, methane chlorophene zinakuepo. Sasa kama sisi hatuna uwezo wa kuzuia hizo maana yake wametupa sababu za nchi yetu kutoweka na nchi yetu kutoweka ni mafuriko na ukame.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama sisi hatuna uwezo wa kuzuia hizo, maana yake wametupa sababu za sisi nchi yetu kutoweka na mafuriko na ukame. Kama ndivyo ilivyo, basi, sisi hatuna namna yoyote ya mpango wowote makusudi zaidi ya kupanda miti, kwa sababu miti ni carbon sinker, inachukua carbon dioxide. Kwa hiyo, lazima tufanye kila namna, kwa kila eneo, kwa kila mkoa, kwa kila sehemu kupanda miti ili kuepuka janga ambalo wametupa sasa hivi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. (Makofi)