Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kabla ya yote kwanza nichukue nafasi hii kupongeza Serikali kwa kuleta maazimio haya yote, na naunga mkono maazimio yote haya matatu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuzungumzia Azimio la Montreal; kuna mashirika ya ndege sio chini ya 25 mpaka 30 yanatumia anga la Tanzania, na kila abiria anatakiwa alipe kodi ya carbon emission (carbon emission tax). Nataka kuuliza Serikali, wamejipanga vipi katika kudai pesa hizi ziweze kurudi nchini na kuboresha mazingira ya Mlima Kilimanjaro, tukapanda miti zaidi ya bilioni moja, kwa sababu ndege hizi zinaharibu mazingira yetu hapa nchini. Kwa hiyo, naomba Serikali walione hilo; kama tunalipa kodi na ndege zinatumia anga zetu ni bora tukatafuta namna ya kudai pesa hizi ili zirudi hapa nchini mwetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kuhusu depreciation ya ozone; depreciation ya ozone inatokana na mambo mengi, pamoja na friji. Nchi nyingi zilizoendelea sasa hivi wamepiga marufuku kutumia friji aina ya Freon; hizi friji zimepigwa marufuku nchini mwao lakini zinaletwa nchini mwetu, na zikija kwetu zinaharibu mazingira yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kuelimisha wananchi wetu waelewe; hivi sindano ambayo imetumika Ulaya utakubalije Tanzania itumike kama sindano mtumba? Na sasa hivi magari mengi yataacha kutumia petroli na fossil fuels, wataanza kutumia umeme na gesi, magari haya yana hatari ya kuja katika Bara la Afrika na kuharibu mazingira yetu. Kwa hiyo, naomba kama wenzetu Ulaya wamekubali sasa kutumia HFC 134a, tetphoroicine, na sisi tukubali kuacha kutumia freon gas kulinda mazingira ya Taifa letu na Bara la Afrika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono. (Makofi)