Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubali turidhie hizi itifaki zote tatu na ninapongeza Serikali kwa kuja nazo ili iweze kurahisisha katika utekelezaji wa majukumu yetu yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba katika eneo lile la kwanza la Montreal, ni vizuri sana, nashukuru kwamba turidhie hiyo itifaki, lakini muhimu ni Serikali iweke mkakati wa kuhakikisha kwamba tunaendelea kuzuia na tunaendelea kuzingatia sheria zilizowekwa kwa manufaa yetu sisi Watanzania. Tusije tukawa dumping ground, yaani eneo la kutupa taka ambazo baadaye itakuwa ni sumu kwetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye hilo pia kuna Mjumbe mmoja alichangia kwamba sheria za kodi ndiyo zinafanya sisi tununue vitu chakavu; hiyo sio sahihi. Sahihi ni kwamba tumeweka kodi kubwa kwenye bidhaa ambazo ni used, yaani bidhaa chakavu ina kodi 20% extra ili tusinunue bidhaa chakavu, kwa hiyo hiyo record ikae vizuri; Serikali imefanya vizuri sana, bidhaa zilizotumika zina kodi ya 20% ili kulinda mazingira yetu, kwa hiyo hiyo record ikae vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kwa upande wa WTO, naomba pia itifaki hii Wabunge wote turidhie ili iweze kufanya kazi. Lakini muhimu kuliko yote, tutakaporidhia hizi itifaki za kimataifa ni vizuri sisi kama ndani ya nchi pia tuhakikishe kwamba tunatenda yale ambayo tumekubaliana huko kimataifa. Kwa mfano kwenye hii ya ufanyaji biashara, ease of doing business, ni vizuri yale yote ambayo tumekubali tutafanya kimataifa huku ndani ndiyo tuwe na dirisha na tuwe tunafanya vizuri zaidi ili huko nje tuwe wa mfano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwenye hizo bring business naomba Serikali ije na hiyo Sheria ya Blueprint itekelezwe kwa asilimia 100, bidhaa zetu ziwe na gharama ndogo ya uzalishaji kutokana na regulatory bodies nyingi. Na pia kuingia kwenye mfumo mzima wa kufanya kazi kwa kupitia internet na urahisi wa kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kwa Itifaki ile ya SADC, naunga mkono sana kwa sababu changamoto hizi zote ambazo zinahusiana na masuala ya mazingira hakuna namna tunaweza kujitenga kama kisiwa. Kwa hiyo, tufanye kazi kwa pamoja. Sheria zote za nchi za SADC zikiwa zinafanana na itifaki tukikubaliana nayo naamini kabisa tutaweza kusaidia nchi yetu kufanya kazi kwa pamoja kwa sababu tunashirikiana katika mambo mengi. Kwa hiyo, itifaki hizi zote naomba Wabunge wote tuunge mkono ili ziweze kutekelezwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ombi langu pia; zile itifaki zingine ambazo tuliwekewa kwenye orodha ya ratiba kwamba zitakuja, basi ziletwe, kwa mfano International Solar Alliance na itifaki nyingine. Basi na hizo zenyewe zije zote turidhie ile tuweze kusonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naunga mkono hoja itifaki zote. (Makofi)