Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia Mpango huu wa bajeti. Michango hii watu wengi wameizungumza vizuri lakini nilikuwa naangalia katika nchi yetu hapa kwamba uchumi wake unakuwaje, unakuwa kwa 6.8 mpaka seven point. Wanauchumi wanasema uchumi ukikua lazima uendane na mipango ya wananchi katika maeneo yao. Nilikuwa naangalia maeneo mbalimbali sijui kwa nini nchi yetu haiendi kwenye vyanzo halisi vya kupata uchumi wetu unavyokwenda. Ukiangalia katika maziwa yetu, Ziwa Tanganyika na Ziwa Victoria, ukinda Norway, ukienda Algeria, nilikuwa naangalia hapa Algeria ni nchi kama ya tatu hivi kiuchumi, lakini maeneo mengi inayotegemea katika uchumi wake ni suala la samaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi uki-invest milioni 40 katika samaki unaweza ukapata samaki 200 na samaki 200 ukipata unaelekea kuzungumza habari ya bilioni mbili. Kwa hiyo nafikiri kwamba, sasa uchumi wetu uende sana kutafuta fedha za ku-invest katika maeneo ambayo tunaweza kupata faida kwa wakati muafaka. Vijana wetu wengi hawana ajira, lakini maeneo yetu mengi yana ajira. Tuna suala la kilimo, ukiangalia sasa Misri ndiyo nchi inaenda kwenye uchumi ambao uko juu kwenye uchumi wetu, lakini uchumi wao mwingi unatokana na hot culture, Kenya hivyo hivyo, Angola nayo imeenda kutuzidi kwenye uchumi ingawaje wana mafuta. Kwa hiyo, naomba Wachumi wetu waelekee sana kwenye namna ya kupata fedha ku-invest katika maeneo ambayo tunaweza tukapeleka vijana wetu wakafanya kazi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa naiona JKT kama ni eneo ambalo tungelitumia sana kupata uchumi wetu vizuri. Tuna maeneo mengi vijana wetu wanaenda JKT, tungetumia vijana hawa kuwapa mikopo katika maeneo, tuna maeneo mengi mazuri sana. Wale vijana wote wanaokwenda JKT wakitoka pale wameiva kwenye shughuli za kilimo, watu wote tume-invest kwenye shughuli za kazi za ofisini kazi ambazo sasa hazipo. Kwa hiyo tubadilishe mind set zetu twende kwenye maeneo ambayo tutanufaika nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo mengi yalikuwa yanazungumzwa hapa, watu wanazungumza good governance (utawala bora), lakini utawala bora haujajikita kwenye election peke yake, umejikita kwenye mambo mengi. Kuna effective, kuna transparency, kuna accountability, kuna mambo mengi yamejikita humo ndani lakini watu wameng’ang’ania mambo ya utawala bora utawala bora, kama vile ni uchaguzi. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi nyingi za Ulaya sasa zinaangalia uchumi wao, kuna watu wanafikiri kwamba Tanzania haiko kwenye mpango wa kwenda mbele. Sasa hivi tunaangalia kwamba uchumi wa China mwaka 2030 utakuwa umezidi Marekani mara mbili, kuna watu wanaangalia hata Mexico nchi maskini inapokwenda 2030 inakwenda kuikaribia Marekani. Kuna watu wanafikiri kwamba kila wakati sasa sijui ni kuzungumza mambo ya uchaguzi, mambo ya kugombana. Kuna wasomi wamesema haya mambo ya uchaguzi pia yaliletwa na watu ambao wameleta kuvurugana kwenye nchi za Kiafrika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia nchi nyingi nyingine zipo nchi za utawala wa kifalme hazina uchaguzi. Leo mtu anazungumza uchaguzi umekuwaje, uchaguzi umekuwaje ili mradi wapate msaada. Nataka niwaambie wenzetu nchi za Ulaya sasa hivi kila nchi inagombana, ukienda Marekani wanagombana juu ya utawala bora, sasa Marekani si nchi ya demokrasia, ni nchi ya utawala wa sheria. Ukienda Uingereza inagombana na Black City, ukienda kila mahali wanagombana kwa hiyo wasipokwenda kwenye uchaguzi wajue hakuna mtu atawasaidia, wao waende kwenye uchaguzi, tufanye uchaguzi mambo yaishe tuendelee na wakati wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna watu wanafikiri Mheshimiwa Magufuli amejiweka tu kuwa Rais, Mheshimiwa Magufuli ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyetokana na Chama cha Mapinduzi. Nilisikia siku moja mtu anasema ndege zimekuja nikaona mapambio, nikaona nini, nikamshangaa. Ukisoma Ilani ya Chama cha Mapinduzi ukurasa wa 70 inaeleza jinsi gani tumefanya mipango mikakati ya kuwa na viwanja vya ndege vingi na kupata ndege kwa ajili ya mambo yetu hapa. Sisi tunapoona…(Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Getere tatizo siyo uchaguzi, watu wanaangalia matokeo, wameshaangalia wanapigwa ile mbaya. (Kicheko/Makofi)

Sasa wanakamatia hapa chini lakini wanajua kimbembe kiko, si tarehe 24 Novemba wewe utaona matokeo tu! Mheshimiwa endelea. (Kicheko)

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwanza…

MWENYEKITI: Nilikuwa namchokoza Frank hapa!

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli! Kwanza mimi naona hiki Chama cha Upinzani ndani ya Tanzania kinaitwa CHADEMA, hiki chama kinakokwenda kwanza wanazungumza transparency, wao wenyewe wanapata mabilioni ya fedha hapa kutokana na ruzuku lakini mpaka today wameandikiwa barua mbili na Msajili wameshindwa kufanya uchaguzi. Sasa huu utawala bora wanaouzungumza ni upi? Utawala bora wa CCM peke yake au utawala bora mwingine? (Makofi)

T A A R I F A

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwakajoka, Mwakajoka ametoka pangoni. Jamani tumempa ruhusa Mwakajoka.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa mzungumzaji, kwanza anasema kwamba mambo ya uchaguzi haya hayafai na sisi pia tulishawaambia kwamba mko wengi ndani ya Bunge leteni Muswada hapa tufute vyama vingi vya siasa ili mbaki na chama kimoja. Mtakaotaka kubaki CCM mbaki na sisi wengine ambao tutakuwa hatutaki tuendelee na mambo yetu. Ahsante. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Kaa chini, kaa chini wewe!

MWENYEKITI: Jamani aliyepewa taarifa ni Mheshimiwa Mwita Getere, unaipokea taarifa Mheshimiwa Mwita!

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza vyama vyenyewe vitajifuta kama vinavyojifuta sasa hivi, kwa hiyo mimi sioni haja ya kuendelea na mambo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze, kuna watu wamezungumza hapa fedha haziendi kwenye maeneo yetu ya majimbo, fedha haziendi huko kwenye halmashauri, fedha haziendi wapi, sasa mimi najiuliza; fedha haziendi wapi? Ukienda sekta ya elimu tunatoa bilioni 24 kila mwezi zinakwenda shuleni, ukienda kwenye afya…(Makofi)

MWENYEKITI: Kila halmashauri inapata.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kila halmashauri inapata. Ukienda kwenye afya hospitali zinajengwa kila mahali hata Mwakajoka juzi alisema imejengwa kwake, ukienda kwenye reli fedha zinakwenda, ukienda kwenye barabara za changarawe na lami zinakwenda, ukienda kwenye shughuli za kila mahali zinakwenda. Kwenye madini wamezungumza hapa, watu wanasema Private Sector, tushirikiane na Private Sector kutengeneza uchumi, sasa mtu anasema tupeleke fedha kwenye madini. Badala ya kusema wale wa madini tuwape nafasi ili Private Sector zituletee fedha, yeye anataka tupeleke tena fedha kwenye madini. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwita na kwenye ruzuku ya CHADEMA zinaenda pia.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ruzuku ya CHADEMA pia zinaenda huko huko ndani. (Makofi/Kicheko/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyoona sasa hivi suala la hawa wenzetu wamejichanganya kuhusu Mheshimiwa Rais wetu. Rais wetu amejiongeza kukusanya mapato ya kutosha kwa ajili ya kupeleka maeneo mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano mmoja, siku moja tumekwenda pale Muhimbili, mtu anasema hapa panadaiwa bilioni nne hazijaja hapa, bajeti haijaja ya bilioni nne. Bilioni nne kabla ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuwa madarakani walikuwa wanakusanya bilioni tano, sasa hivi katika sekta ile ya Hospitali ya Muhimbili inakusanya bilioni 11, sasa kama zimeongezeka unapeleka za nini wakati hela zimeongezeka? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawajui kubana matumizi pia ni sehemu ya kuongeza fedha kwenye maeneo mbalimbali. Kwa hiyo nafikiri kwamba wenzetu wanajichanganya na hali halisi ilivyo na katika huo utawala bora wako watu wanasema ile Citizen, Watanzania wanategemea nini. Kama wameona Rais aliyepo na chama kilichopo kimebadilika kinaenda kuwaletea matumaini wawe na vyama vingine vya kufanya biashara gani! Leo hata mngepeleka Polisi Ngorongoro, hata mngepeleka polisi pale Monduli kuna maeneo hata ungepeleka fomu 300 hazichukuliwi. Maana pale hawachagui vyama, wazee ndiyo wanasema, ukienda Ngorongoro wao walishamaliza uchaguzi wanasema wewe ni Mwenyekiti, wewe utakuwa Diwani, wewe utakuwa Mbunge, sasa unaenda kufanya biashara gani kule ndani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona chama kinaitwa sijui ni NCCR Mageuzi, hakipo. Yule mzee naye ampumzike aende pole pole tulishampa na madaraka siku nyingi hapa ndani, naye anang’ang’ana kwenda kwenye sehemu ambayo haipo. Atulie mahali pake sisi tumuone bora hata tuweze kumpa Ubalozi, anaanza tena maneno ya kuleta matatizo kwenye nchi yetu hapa. Kwa hiyo tukubaliane kwamba CCM pamoja na kwamba Rais wake...

T A A R I F A

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwita kuna taarifa.

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimpe taarifa Mwita Getere kwamba hata kwangu Serengeti, nimeshangaa sijawahi kuona, vijiji vingi wamepita bila kupingwa hata kwenda kuchukua fomu imeshindikana, wametafuta wagombea wamekosa kabisa. Sijawahi kuona hii, sijawahi kuona kabisa. (Makofi/Kicheko)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwita unapewa taarifa hiyo, unaipokea?

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea taarifa kwa sababu mimi ninavyoona, labda kama tunataka, nakuomba, pengine tukae tukubaliane hawa wenzetu walioko humu ndani tunaweza kuwasaidia labda kajimbo kamoja, viwili wakarudi humu ndani. Maana yake hali ya hewa ni mbaya kuliko ilivyo kawaidia, kwa hiyo, ndiyo maana wamekuwa na hali hiyo (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme ukweli kama tunataka kuwa na upinzani tutengeneze mazingira ya kuwabakiza wenzetu, vinginevyo wote hawatarudi hapa ndani. Kwa hiyo, tukubaliane na mazingira hayo, vinginevyo tukubali sasa Tanzania imebadilika, watu wanataka Chama cha Mapinduzi, lakini wasimhusishe Mheshimiwa Rais na uchaguzi. Mheshimiwa Rais anafanya kazi za Serikali, Chama cha Mapinduzi kina viongozi wake, Chama cha Mapinduzi kina Katibu, kuna viongozi, kuna Wabunge sisi tupo tunapambana na mambo yetu. Wenzetu wameshindwa kwenda kupambana kule chini, wanapambana na hali ya hewa ya kwao humu ndani. Wameshindwa kwenda kupambana kwenye majimbo yao wameachia maeneo yameenda, watu wanaogopa. Kwa hiyo, naomba mazingira yatengenezwe, tuone namna gani tutaendelea na upinzani Tanzania, vinginevyo hautakuwepo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)