Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi naomba niwape hongera sana wenzetu wa Serikali kwa mpango wao huu waliotuletea hapa. Nianze kwa kuwapongeza watu wa Wizara ya Kilimo na biashara, leo tarehe 11 yale madai yote ya korosho yamelipwa na wakulima sisi; na mimi mkulima; kupitia cashew nut payments code 704 imelipwa, kwa hiyo, ahadi ya Mheshimiwa Rais Magufuli imetekelezeka hongereni sana na sisi wakulima tunaendelea kukaza mwendo, Hasunga hongereni sana kwa kazi ilikuwa ni kitu kabisa kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nina mambo machache, nina mawili tu. Kwanza nilitaka nirejee maneno yako uliyoyasema asubuhi kuhusu China; ulivyosema nimekusikia vizuri. Kama nimekuelewa vizuri nadhani Mbunge yeyote mwenye maarifa amekuelewa vizuri, na bila shaka Serikali imeelewa vizuri. Kwasababu China inapaswa iwe ndicho chanzo chetu cha mtaji wa miradi mikubwa ya maendeleo. Lakini ni kwanini mpaka sasa, tunapozungumza, hata TAZARA iliyojengwa na Mwalimu Nyerere ina mgogoro mkubwa sana. Ni mahali gani tumeshindwa kuzungumza na Wachina hawa tukaelewana wakati wachina hawa kihistoria kwa kweli ni ndugu zetu na kuna maelewano ya kihistoria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwasababu wewe pia ni kiongozi wetu humu mimi napata hisia kwamba tuwashawishi viongozi wetu wakubwa wakatembelee China, ili kama kuna kitu hakieleweki wakakifungue wakubwa hawa. Wachina hawa tunaweza tukawatumia vizuri na wangeweza kutusaidia kwa mambo mengi, hasa masuala haya ya kimtaji kwa sababu uchumi wetu ndio unajijenga, unahitaji ku-stabilize, vinginevyo naona kama tutapata shida. Hii kukopa kwenye benki, fanya hiki inatuletea shida kubwa sana. Ni vyema twende China tukazungumze nao, tukakope mkopo mkubwa na wamuda mrefu ili kuweza kukwamua masuala haya tunayotaka kuyafanya katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nafikiri hoja yako ya asubuhi imenikuna sana; nawe kwasababu mnakaa na wakubwa mnakunywa kahawa nadhani kuna haja ya kuipeleka na kwao kule waweze kuielewa vizuri; umetueleza kitu kizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili ambalo ningependa niliseme pia amelizunguza ndugu yangu Mwakajoka hapa. Waziri wa Fedha fursa hazitusubiri, fursa zipo kesho hazipo. Nasema hivi kwa sababu; nizungumzie suala ya reli ya kati kwa mfano, SGR inayojengwa ni kitu chema sana, Rais Dkt. John Pombe Magufuli huyu ameamua uwamuzi wa busara kabisa kutujengea reli ya kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini reli hii ni mradi mkubwa na manufaa yake ni ya muda mrefu kidogo. Hii reli itakuwa na manufaa ya kiuchumi kama itafika Kigoma kwa ajili ya kuchukuwa mzigo mzito uliopo mashariki mwa DRC. Reli hii itakuwa na faida tawi lake hili la kutoka Tabora Kaliua kwende Kalema mpaka Kasanga Port kwa ajili ya kutape mzigo uliopo kusini mashariki ya DRC.

Mhimiwa Mwenyekiti, majirani zetu wote fursa wanayoitazama ni hiyo hiyo. Utasikia ooo! leo hii mzigo mkubwa unaopita bandari ya Dar es Salaam ni wa nchi ya Uganda! Zipo taarifa ambazo ninauhakika nazo kabisa; asilimia 60 wa ule mzigo unatoka Mashariki Kaskazini ya DRC ambao wangeweza kuja kutumia Bandari yetu ya Kigoma na wakaja kutumia Bandari yetu ya Kasanga kwenye Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu yangu Mheshimiwa Keissy amezungumza Bandari ya Kigoma leo tunachozungumza, na Waziri wa Fedha unajua; kwamba Bandari ya Kigoma Modernization ya Kigoma pot kuna pakeji ya msaada kutoka Jamhuri ya watu wa Japan. Hata hivyo mradi ule umekwama na sababu zake za kukwama ni vikwazo eti! Wanadaiwa mitambo yao walipe kodi za TRA. Wale wajapani walikuwa negotiation na Serikali huu ni mwezi wa saba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi ningependa kujua kwakweli, on a serious note, ni kitu gani kimekwamisha modernization ya Port ya Kigoma ilhali wenzetu Wajapani wapo tayari kutusaidia ku-modernization bandari ile kwa maslahi mapana ya uchumi wa nchi yetu. Kwamba mzigo sasa utoke ngambo ya pili ya DRC uje Bandari ya Kigoma uje kwenye reli ya SGR itakayojengwa kupeleka mzigo nchi za China na mashariki ya mbali; hilo ni jambo ambalo ningependa tuendelee kulizungumza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii zana ya majirani zetu, sina haya ya kuwataja, kujenga barabara kujenga reli na matawi yake wanakuja kudhohofisha, maana tutakuwa tunapokea mizigo kutoka nchi ya tatu. Origin, nchi ya pili na sisi tunakuwa nchi ya tatu ilhali tuna fursa ya kuja moja kwa moja sisi kutoka DRC na kuja katika nchi ya Tanzania; fursa hizi mziangalie. Nina matumaini kule hazina mtakaa chini na wataalamu mliangalie kwa mapana na marefu haya; mumshauri Mheshimiwa Rais juu ya jambo hili sasa, jambo hili maslahi yake ni mapana sana kwa taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni kuhusu ndege. Tulikuwa wote wakati tunapokea Dreamliner, nadhani wewe ni shahidi na wote mliokuwepo, kwamba kilikuwa ni kitu chema mno, kitu ambacho kila mmoja alifurahi. Dreamliner inatoka Marekani inatumia masaa 16 kufika Dar es Salaam, non stop na kila kitu kinafanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu iko hivi; Mheshimiwa Waziri wa Fedha ununuzi wa ndege ni jambo jema mno, jambo jema sana. Hata hivyo ndege hizi lazima tuzifungamanishe mambo mengine, ndege hizi lazima tuzifungamanishe na wenzetu wa utalii ili ndege hizi ziweze kuwa na faida. Vinginevyo ndege peke yake hizi zitafika mahali itakwenda Mumbai haina abiria wa kutosha, itakwenda Guangzhou haina abiria wa kutosha. Kwa hiyo kuna haja wenzetu wa Serikali hasa Wizara ya Fedha wazungumze na mashirika rafiki kama vile Precision Air, Rwanda Air, na zimbambwe Airway, na sisi Dar es Salaam iwe hub katika International travel, vinginevyo ndege hizi zitakosa biashara inayotarajiwa.

Mheshimiwe Mwenyekiti, ndege tuliyopanda siku ile ukiiangalia inabeba abiria 260 non stop Dar es Salaam Guangzhou, non stop Dar es Salaam mpaka Mombai. Sasa ndege hizi sisi wenyewe hatuwezi lazima tufikiri kibiashara; kwamba abiria kutoka Lubumbashi, Lusaka, Lilongwe, Bunjumbura na Entebe wanakuja Dar es Salaam halafu Dar es Salaam, halafu Dar es Salaam ndiyo inakuwa ndiyo kitivo na eneo la hub. Kama ilivyo Dubai, sisi lazima tuwe Dubai nyingine katika nchi za maziwa makubwa ili ndege zetu ziweze kuwa na faida kubwa hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho kabisa na li-link na hili hiliā€¦

MWENYEKITI: Pia katika hilo hili hawa Lubumbashi Waziri wa Uchukuzi akumbuke kujenga hoteli ya watu wa transit haraka sana, endelea Mheshimiwa.

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa kabisa, ahsante sana; na hilo unalolisema, ukiangalia tulichowekeza kwenye ujenzi wa rada tuna rada nne zinafanya kazi. Viwanja vya ndege vyetu vingi havina taa za usiku na matokeo yake ndege zetu nyingi zinafanya kazi mchana usiku hazifanyi kazi; na abiria kutoka Goma Congo kutoka Bukavu; na kwa wale wasiojua, Mji wa Bukavu ni mkubwa kama Dar es Salaam, ni miji mikubwa sana hii. Hawa watu wangeweza kuwa wanakuja kwa ndege za kusafiri mpaka usiku. Tafsiri yake ni kwamba Bandari ya Kigoma sasa ijengewe facility ya ndege kutua usiku ili ndege zifanye usiku na mchana ili ndege zetu kubwa zile ziweze kuwa na faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa rada, ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Julius Kambarage Nyerere, terminal III uweke na ndege hizi tumetumia takribani tirioni 2.7. Sasa lazima wenzetu wa hazina mfikiri kibiashara, muwe na mpango wa muda mfupi, muda wa kati na hakika tuwe na mpango wa muda mrefu kwa sababu hizi ni fursa, Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kafungua fursa, hizi ndege wenzetu wanashangaa. Juzi nilikuwa nazungumza nabalozi mmoja wa nchi jirani akawa ananiuliza ninyi mmewezaje; nikamwambia hiyo ni Magulification of Africa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo haya ni makubwa, na wenzetu wa Wizara ya Fedha, Wizara ya Uchukuzi, Mama Kairuki, wa uwekezaji, muanze kufikiri kibiashara. Juzi nimefurahi kusikia Waziri wetu wa biashara alikuwa China, nimefurahi sana, alikuwa anatueleza mambo ya kule China. Mawaziri msafiri msikae ndani. Ndege asiposafiri hawezi kujua mtama umekomaa wapi; na kadiri Mawaziri mnavyosafiri mnakuwa wa kisasa zaidi na namnakuwa mnaifahamu dunia zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi kwa leo nilifikiri nizungumze hayo, nakushukuru, ahsante sana.