Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza napenda kukushukuru kwa kupata nafasi hii na pia napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kupata fursa hii ya kuchangia katika Wizara hii ya Elimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja ya Kambi ya Upinzani kwa asilimia 100. Ninavyounga mkono, naomba ninukuu maneno ya Hayati Baba wa Taifa katika kitabu chake cha Binadamu na Maendeleo alipokuwa akizungumzia faida ya elimu katika nchi. Naomba ninukuu baadhi ya mistari, anasema:- “Tunatumia fedha nyingi sana zisizolingana na uwezo wetu kuwasomesha watu wachache ili baadaye na wao walete faida kubwa kiasi hicho hicho katika nchi. Tunatumia fedha nyingi kutafuta faida katika akili ya mwanadamu kama vilevile tunavyotumia fedha kununua trekta na kama vilevile ambavyo tukinunua trekta tunatarajia kufanya kazi kubwa zaidi kuliko kazi ya mtu na jembe la mkono”. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama tunaona elimu ni gharama tujaribu ujinga, walikwishazungumza watu wengi. Elimu ya nchi hii imewekwa rehani. Watanzania walio wengi hawaoni umuhimu wa kupeleka watoto wao katika shule zetu za Serikali kwa sababu ya matokeo ambayo tunayaona sasa hivi. Watoto wengi wamekuwa wakimaliza shule bila hata kujua kusoma na kuandika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Waziri wa Elimu aweze kunisikiliza kwa makini. Hakuna elimu bora bila kujali Walimu. Walimu ndiyo wanaofanya elimu hii ikawa bora zaidi hata kama shule ikiwa haina madawati mengi, haina miundombinu mizuri zaidi lakini Walimu wakawa wameboreshwa vizuri wanaweza wakafanya elimu hii ikawa bora hivyo vingine vinasaidia kuwa bora zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi hii imewatelekeza Walimu. Tumesema tunahitaji Walimu wa Sayansi katika nchi hii lakini tuna vyuo vya ualimu visivyo na maabara. Nitavitaja baadhi muone kama vyuo vya ualimu ambavyo vinafundisha Walimu wa Sayansi havina maabara unategemea nini huko? Kuna Chuo cha Ualimu Vikindu, Chuo cha Ualimu Singa Chini, Chuo cha Ualimu Mpuguso, Chuo cha Ualimu Kitangali na vinginevyo hivi navitaja ni baadhi havina maabara na hakuna vifaa vya maabara. Sasa tunatarajia nini na tunajenga maabara nchi nzima tukitarajia kwamba tutapata Walimu bora ambao watakuja kufundisha watoto wetu lakini kule tunakoandaa Walimu wetu hakuna maabara. Serikali hii inafanya masihara na elimu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Walimu hao hao wa Sayansi waliahidiwa kupewa mikopo, hapa ninavyozungumza Walimu hao wa Sayansi hawajapata fedha za mikopo mpaka dakika hii. Nina ushahidi nitakuletea orodha ya Walimu Mheshimiwa Waziri kama utahitaji, wengi hawajapata mikopo katika sekta hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niende kuzungumzia katika suala la mitaala. Naomba ni declare interest mimi ni Mwalimu na pia nilikuwa mkuzaji wa mitaala kabla sijaacha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kabisa tunapozungumzia elimu bora tunahitaji mitaala iliyo bora na mitaala ili iwe bora ina process zake za uandaaji. Zile hatua zikipindishwa ndiyo tunapata matokeo haya sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunatakiwa tufanye research ili kujua Serikali yetu au nchi yetu inataka Watanzania wawe na elimu ya namna gani ili kuwanufaisha hao Watanzania, ile sera kwanza haipo vizuri. Tulikuwa tuna falsafa ya elimu ya kujitegemea huko nyuma lakini sasa hivi haieleweki na haitafsiriki vizuri kwenye mitaala kwamba tunakwenda na falsafa ipi sasa hivi. Je, bado ni elimu ya kujitegemea mpaka sasa hivi ama tuna nini ambacho kipo?
Mheshimiwa Naibu Spika, baadhi ya process nyingine zinarukwa, tunatakiwa tuite wadau ili tukubaliane nao ni yapi ambayo tunatakiwa kuyaweka kwenye mitaala. Mheshimiwa Waziri alikuwa ni Mjumbe wa Bodi katika Taasisi ya Elimu Tanzania anaelewa matatizo yaliyopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mara nyingi tulikuwa tukiomba fedha Wizara ya Elimu lakini fedha za kufanyia mambo hayo mengi zinakuwa hakuna, unatarajia upate nini? Unatakiwa ufanye utafiti, uitishe wadau lakini kwa kiasi kikubwa wadau wa nchi nzima unaweza ukaita wadau 60 au 100, hao watasaidia kuweza kujua kwamba nchi hii inahitaji twende katika mrengo upi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile katika suala hilohilo kuna masuala ya vitabu. Mheshimiwa Waziri amezungumza katika hotuba yake, amezungumzia masuala mengi yanayohusu masuala ya vitabu. Kulikuwa na bodi iliyokuwa inaitwa EMAC ambayo walikuwa wanashughulikia vitabu vyetu, ilivunjwa wakarudisha Taasisi ya Elimu Tanzania iweze kufanya kazi hiyo. Hivi ninavyozungumza hapa shule zetu kule hazina vitabu, Wizara imeandaa masuala ya KKK lakini sijui huo usambazaji TAMISEMI unakwenda vipi. Walimu wanakwenda wanafundisha bila vitabu na vitabu vyenyewe vilivyokuwa vimetolewa kwa masomo mengine vinatofautiana, hii ni changamoto kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, miaka ya 80 kulikuwa na ushindani baina ya shule za Serikali na shule za watu binafsi. Leo hii mnaleta bei elekezi, hivi hawa wenye shule binafsi wangekuwa hawakuweza kuwekeza hivyo wale watoto wetu waliokuwa wanaachwa wangekwenda wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, badala ya kukaa tukaboresha elimu yetu katika shule zetu za Serikali ndipo sasa tuanze kuona kwamba tunaweka bei elekezi baadaye, kwa nini tunaanza kubana watoto wetu wasiweze kusoma katika hizo shule kwa sababu huku waliachwa katika nafasi ya shule za Serikali?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu shule za Serikali zinawachukua wale ambao ni bora na hawa shule binafsi zinawachukua wale ambao siyo bora ilivyokuwa zamani. Sasa hivi hata wazazi hawaoni umuhimu huo kwa sababu kule shuleni tunakuta hakuna Walimu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe mfano katika Mkoa wangu wa Iringa kuna baadhi ya shule ina Mwalimu mmoja shule nyingine zina Walimu wawili, shule ya sekondari wanatakiwa wafundishwe masomo yote.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kimoja Mheshimiwa Waziri lazima mtambue utahini wa mitihani. Shule X ambayo ina Walimu wa masomo yote na shule Y ambayo kwa mfano ina Mwalimu mmoja au wawili lakini mwishoni mwa utahini mnatahini mitihani sawa. Hii siyo sawa hata kidogo!
Mheshimiwa Naibu Spika, tuwaangalie wale ambao wamefundishwa na Mwalimu mmoja somo moja tutahini kwa kile walichofundishwa! Kwa nini mnawafelisha watoto wetu wakati mwingine wakati siyo makosa yao kwa sababu…