Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Ally Abdulla Ally Saleh

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Malindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwanza kabla ya yote napenda kwa mara nyingine tena ku-register kwamba bado sioni mantiki ya kutengeneza mpango wetu bila ya kuwa na connectivity yoyote ile na Zanzibar, bado akilini mwangu nataabika. Unawezaje kutengeneza uchumi wa nchi pasiwe na connectivity, hiyo bado najiuliza, na kwanini kila mara hili halifanyiki? Napenda iwepo on record.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili na katika mpango umezungumza…

SPIKA: Connectivity gani Mheshimiwa Ally Saleh, kwa dakika moja tu ili akupate vizuri.

MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano wakati ule wa mpango wa mwanzo kulikuwa kuna miradi kielekezi, na tulisema angalau mradi mmoja ukiwekwa Zanzibar utasaidia kazi, utasaidia ajira, utasaidia kila kitu. Si kila kitu kiwekwe huku, hata kama cha muungano kikiwekwa kule kinaweza kikasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano Bandari ya Bagamoyo.Unaweza ukawa na Bandari ya Bagamoyo lakini kuweko na connectivity; kazi fulani inaweza kufanywa Zanzibar; kwa mfano namna ya ku-repair au ya kufanya vitu gani hiyo ndiyo connectivity ambayo nazungumzia lakini huu mpango tunachoambiwa ni kwamba Zanzibar wanampango wao lakini at the end of the day hii ni nchi moja hakuna connectivity, hilo la kwanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kuhusu dhima; dhima nimeipenda kwasababu inaelezea juu ya kuongeza mauzo ya nje na uwezo wa ushindani, hii ni dhima nzuri sana kwa nchi kujiwekea kwasababu hapa nikieleza itaonekana kwambanaiunga mkono kwasababu gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevie tumechagua maeneo matano ya mkakati ambayo mimi nitataja matatu ambayo yamenipendeza; nayo ni uchumi wa viwanda, uchumi wa watu na uwezeshaji biashara na uwekezaji, na ninataka nianzie hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ningependa kuungana na Mheshimiwa Ally Keissy, Mheshimiwa Wilfredy Lwakatare na Mheshimiwa PeterSelukamba,nafikiri na mmoja mwingine yoyote ambaye amesema. Kwamba kuwepo sisi hapa kama nchi coordinance kadhaa mpaka coordinace kadhaa Mwenyezi Mungu ametaka tuwepo na fursa zimetuzunguka. Kwa mfano amezungumza Mheshimiwa Lwakatare juzi, wanasema walipo wao kuna fursa mpaka South Sudan; leo Mheshimiwa Ally Keissy anasema kwamba tunapakana na moja katika nchi tajiri Afrika ingawa per capitalyake ni dollar 627 lakini wana strength ya watu na pia wanautajiri wanchi.

Kigoma tunapakana na nchi nyingine nyingi pale, pamoja na Kongo je tunazitumia vipi fursa ya uwepo wetu katika maeneo hayo? Kama nchi tunajielekeza vipi maeneo yaliyo pembezoni kwa jina tu lakini ndiyo ambayo yalitu- open up.Kwahivyo bado nahisi hata kama tutatekeleza maeneo ya kilimo, maeneo ya deep sea, uwekezaji, biashara elimu, nishati na LNG inparticularna energy mix, kama alivyosema Mheshimiwa Selukamba bado tunataka outs tunataka tutoe vitu vyetu. Umesema hapa China, lakini it is not only China, kuna nchi nyingi. Urusi per capital yao 24 thousand per person, Uchina yenyewe ni per capital yao 16,000 lakini Uturuki per capital yao ni 26. So, it is not only China. Nakubaliana na mtu aliyesema nikutafuta new markets; kama tunavyotafuta new market kwenye utalii, basi tutafute new market kwenye uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uturukiis so strategicallylocatedkwa Asia na Europe. Ni njia ya kuingia Europe kirahisi, ni eighthoursfrom Dar es Salaam. Uturuki wanaleta ndege mbili kila wiki, wanaleta ndege tatu kila wiki lakini almost nothing leaves here to go to Turkey kwasababu hatujajitayarisha kibiashara. Pia Uturuki na kama viletunavyokaribisha Urusi, wanauwezo mkubwa sana wa kuwekeza,the money is there forthem wanachotafuta wao ni waziweke wapi. Ssasa mimi nafikiri kuna haja ya kutazama hili hapa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine; kwamfano tumezungukwa na bahari, kila siku tunasema; tunaambiwa kutakuwa na bandari ya utalii, bandari ya uvuvi.Issue si bandari ya uvuvi,issue ni kuwa na mipango kwanza kabla hujajenga bandari, watu hao wanaokuja kutuvulia ndio watakaotupa pesa ya kujenga bandari. Una uvuvi unaotoza kilo moja unaotoza dola 0.4 kwa kilo moja ya samaki, unawavunja moyo wanaokuja kutaka kuwekeza kwenye habari ya uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo issue si kuwa na mipango, lakini ni kupanuka, ni kutazama fursa mpya. Kila siku fursa mpya zinakuja,kila siku watu uchumi wao unaongezeka duniani; soko la Arabuni Qatar, Dubai pamoja na Oman. Tumefanya nini kama nchi? Kwahiyo mimi nafikiri kama ilikuwa mpango ule upo sasa haupo, kwamba pale mwanzo wa awamu hii walikuwa Mawaziri au safari za nje zilikuwa kidogo kwa watendaji mimi nahisi ni wakati sasa tupanue safari kwa watendaji ili waende wakatafute masoko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu gani utapeleka India kirudi, kitu gani utapeleka India kirudi kitu gani utapaleka China kirudi, kitu gani utapeleka Qatar kirudi, kwasababu wao hawalimi as such.Lakini bado, nchi kama Oman pamoja na kwamba wana utajiri mkubwa na wana gesi wana kitu gani lakini bado hawana kilimo cha kutosha na sisi tunaweza tukajazia mazao yao huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kuzungumza hayo, kuna jambo moja ambalo limo katika mpango lakini limetajwa just in passing; kidogo tu limetajwa, nalo ni utawala bora. Dunia ya leo ni wazi kabisa huwezi kuwa na uchumi mzuri kama hujawa na utawala bora, nchi chache tu zimepenya; labda Indonesia zamani, zilizokuwa Tiger zile, walikuwa na ukandamizaji kandamizaji lakini bado wakapenya. Hata hivyo bado, ukiwa na utawala bora ndiyo unakusaidia kwenye uchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la utawala bora bado mimi nina wasiwasi nalo katika nchi yetu. Public space inazidi ku-shrink kila siku, fursa za maoni zinazidi kupotea. Tumetunga AccessTo InformationAct miaka kama 10 nyuma huko au saba nyuma mpaka leo hatujatunga kanuni. Kwa hiyo bado mwananchi hawezi ku-access information ambayo anaitaka kutoka Serikalini. Vilevile uhuru wa vyombo vya habari ambao umekuwa ukilalamikiwa sana. Kwamba vyombo vya habari vinaogopa kuandika, ingawa unaweza ukasema uhuru upo lakini watu wanaogopa. Pia mfumo wa mahakama; tuna mashekhe leo miaka saba wako jela hata kesi haijaanza. Kwahiyo hii inatutia doa kwa watu wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hivi sasa imekuja hii issue ya Serikali za Mitaa; mimi nahisi hii ni aibu kwa taifa, kwasababu huwezekani unakata asilimia 96 ya wagombea;at least kwa chama cha ACT na CHADEMA asilimia tano; halafu anakuja Waziri na simple statement ambaye kabla yake alisema hakuna kilichobadilika…

SPIKA: Mheshimiwa Ally Saleh naambiwa muda hauko upande wako

MHE. ALLY SALEH ALLY: Ulinipa dakika 10 Mheshimiwa?

SPIKA: Yuko katibu anaangalia

MHE. ALLY SALEH ALLY: Nitaziona katika clip in shaa allah. (Makofi)

SPIKA: Anaangalia hapa maneno; ahsante sana Mheshimiwa Ally Saleh.