Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kunipa nafasi kuchangia kwenye mpango huu kwanza nimshukuru Mwenyezi Mungu kunipa uhai na nguvu kuendelea kuwatumikia wananchi wangu wa Jimbo la Kyerwa pia nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri kutuletea mpango huu pia kwa ujasiri ambao ameendelea nao kusimama imara kuhakikisha anaisimamia wizara yetu inafanya vizuri kwa kweli tunampongeza hajatetereka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa maamuzi magumu ambayo amekuwa akiyachukua kwenye mambo mbalimbali ambayo ameyafanya na watanzania wanaona kwa kweli tunampongeza sana tunaendelea kumwombea afya njema, Mwenyezi Mungu amlinde aweze kutimiza majukumu yake ya kuwatumikia watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kuchangia kwenye mpango huu kuna mambo ambayo nitaishauri Serikali, nishauri upande wa miundombinu. Maeneo mengi ya uzalishaji ni vijijini tunaposema tunaingia kwenye Tanzania ya viwanda lazima tuangalie kule vijijini ambako tunategemea kuzalisha ambako kuna wakulima wengi zaidi ya asilimia 70 lakini ukija kwa upande wa miundombinu kama barabara kwa kweli Serikali pamoja na jitihada ambazo imekuwa ikionyesha lakini bado kuna maeneo mengi ambayo hayajafikiwa vizuri, mimi nitoe mfano kama kule kwangu Kyerwa, Kyerwa tunazalisha sana kwa mwaka sisi tunalima zaidi ya mara tatu lakini ukija kuangalia barabara zetu kwa kweli sio nzuri na ukienda upande wa pili kwa kweli ukaangalia barabara za wenzetu na ukaja kidogo kwenye upande wa Kyerwa kwa kweli inasikitisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sana Mheshimiwa Waziri tuwekeze nguvu sana kwenye miundombinu ili hawa wakulima wanapozalisha mazao yao yaweze kufika sokoni kirahisi ndipo tutaweza kuinua kwanza kipato cha mkulima pia kuinua kipato cha Serikali. Kwa hiyo, niombe hilo Mheshimiwa Waziri uliangalie tunazo barabara zetu za Mgakorongo kwenda Murongo mpaka Uganda lakini tunayo barabara ya Mulushaka kwenda Nkwenda Murongo hizi ni barabara ambazo ni muhimu ukilinganisha na uzalishaji ambao tunaupata kule Kyerwa kwa hiyo niombe sana hilo tuliangalie hatuwezi tukasema tunaingia kwenye uchumi wa viwanda wakati miundombinu ambayo tunategemea kupata mazao yaje kwenye viwanda vyetu kama sio mizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine nilizungumzie tunayo mazao yetu ya kimkakati tunategemea kuwa viwanda vingi lakini hivi viwanda lazima tuhakikishe malighafi zinatoka hapa ndani kama tunataka kuinua uchumi wa Taifa lakini tukitegemea malighafi zinazotoka nje tutakuwa tunawanufaisha wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niombe sana nchi yetu Mungu ameibariki tunaweza kulima maeneo mengine kama nilivyosema kule kwetu tunalima mara tatu kwa mwaka sasa niombe sana tuwekeze sana kwenye kilimo. Tumekuwa tukiongelea suala la mazao ya kimkakati, kahawa na haya mazao mengine lakini hatuoni jitihada za Serikali kuongeza uzalishaji wa hizi kahawa. Kwa hiyo, niombe sana kwenye haya mazao ambayo ni ya kimkakati ambayo tunategemea yeweze kuleta malighafi kwenye viwanda vyetu kama hatujawekeza nguvu. Kwa hiyo, niombe sana Mheshimiwa Waziri hili uliangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine lisemee ni kwa upande wa afya, Pamoja na jitihada za Serikali kuwekeza kwenye vituo vya afya, kuwekeza kwenye hospitali lakini bado hatuna madaktari wa kutosha, tunategemea tuwe na madaktari tuwe na wataalam wa kutosha ili watanzania wawe na afya nzuri ndipo tutaweza kuwa na uzalishaji ambao ni mzuri. Kwa hiyo, niliombe sana Mheshimiwa Waziri hili mliangalie na muwekeze nguvu lakini pia pamoja na jitihada za Serikali tuna vituo vingi vya afya ambavyo vimeongezeka nchini pamoja na hospitali za Wilaya lakini bado vifaa havitoshi. Kwa hiyo, niombe sana hili la lenyewe tuliangalie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ili tuweze kufika kwenye uchumi wa viwanda lazima tuwe na maji safi na salama kwa wananchi wetu. Wananchi wetu wanatumia muda mwingi kwenda kutafuta maji wakati mwingine masaa hata mawili, matatu lakini hakuna maji ambayo yanaweza kuwasaidia wananchi wetu waweze kuzalisha. Mwananchi ameondoka saa 11 ameenda kutafuta maji halafu unategemea atarudi saa nne aweze kwenda shambani kulima, na hao wakulima ndio tunaowategemea waweze kuzalisha sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyeiti, kwa hiyo, niombe sana Serikali pamoja na jitihada zake niombe sana muendelee kuwekeza upatikanaji wa maji safi na salama na nimwombe sana Mheshimiwa Waziri nimekuwa nikikusumbua sana kwenye miradi ambayo iko kule Kyerwa tunao mradi wa vijiji 57 niombe sana miradi hii iangaliwe ili wananchi wetu ambao hawa tunategemea ndio wawe wazalishaji wakubwa kuinua uchumia wa Taifa letu waweze kuwa na muda mwingi wa kwenda kuzalisha kuliko kuwa na muda mwingi wa kwenda kutafuta maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona sana huu mpango ni mzuri lakini haya mengine tukiyazingatia nimeongelea suala la maji, miundombinu, kilimo hivi vitu vikiangaliwa vizuri ninaamini tutapiga hatua kutoka hapa tulipo na uchumi wa Taifa letu utaongezeka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo ninakushukuru asante sana. (Makofi)