Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Kabla sijachangia niombe niseme maneno mawili, matatu, hasa ni shukurani. Nakushukuru wewe, Mheshimiwa Naibu Spika pamoja na Katibu wa Bunge na Wakurugenzi wote pamoja na Waheshimiwa Wabunge wote, kwa upendo ambao mlionesha wakati nikiwa hospitali ICU. Ni jambo kubwa sana limefanyika kuokoa maisha yangu. Kwa hiyo nawashukuruni sana kwa moyo wa ukunjufu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mambo mawili tu, la kwanza hili lililotokea na kukaa ICU. Tunazungumzia mipango hapa ukiniuliza sana nitakueleza labda ukiacha mkono wa Mungu ni vifaa pamoja na mabingwa walioweza kuokoa maisha yangu, sasa ni wakati muafaka Serikali imeshafanya mambo mengi sitaki kuyataja, imeshafanya mambo mengi, lakini sasa tujikite kuhakikisha watu wetu wanapata uhai. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini nasema, ukipelekwa Muhimbili ndugu zangu umepona. Muhimbili ya sasa sio kama zamani, wewe omba ufike emergency utaona jinsi gani madaktari mabingwa tena vijana watakapokufanyia kazi hapo mpaka ukafikishwa kama ni wa ICU au wa wodini unajua kabisa kwamba hiyo hospitali ina vifaa na ina wataalam, hivyo vitu ndio tunakosa mikoani. Badala ya kudhani kwamba kila siku… naogopa kidogo kuyataja mengine, tupeleke sasa pesa kwenye hospitali za mikoa ziwe na vifaa, ziwe na wataalamu ili watu waokolewe huko huko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake ni kwamba mimi ningeweza kupona nikiwa Tabora lakini kama tutategemea tu hospitali moja ya Muhimbili maana yake maeneo mengine yote kwa sababu ukiacha bima nani atakuwa na uwezo wa kusafiri mpaka Muhimbili ni tatizo, nadhani hata wanaotibiwa nje watapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa nadhani Serikali sasa iwe na uwamuzi tu wa makusudi, hizi MRI zikipelekwa kila mkoa watamalizana huko CT-Scan nini watu watapona. Kwa hiyo, naiomba sana Serikali na bwana Mipango jaribuni kuliona hilo ili kuokoa maisha ya watu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitaki kuchukua muda mrefu, la pili ni maji. Maji limekuwa tatizo na haya maji tunazungumzia maji ya Ziwa Victoria tu. Hivi wataalam wana mipango, wanashindwa kutupatia mbinu mbadala au vyanzo vya maji vingine, hivi kama tunaweza kukinga Rufiji tukapata umeme huku mikoa mingine hatuwezi kukinga maji. Kwa mfano Mkoa wa Tabora maji yako mbali sana chini, ndio maana shida ya maji ipo kila siku, matokeo yake tutazozana mimi hamjanipangia sijui lakini maji ni muhimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tumeweza kwenye umeme kwa nini maji tusiweze lakini shughuli ya maji inakwenda polepole sana. Kwa hiyo, nilikuwa nawashauri hebu na kwenye maji tujaribu kupaona pakoje ili watu wetu waweze kupata maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho tunapanga mipango hapa huku tukijua mapato yetu yatakuwaje. Leo hii tumbaku makampuni yanaondoka na kwa utaratibu wa kilimo cha tumbaku mpaka upewe makisio usipopewa makisio huruhusiwi kulima. Eneo kubwa kwa mfano tunakolima tumbaku Lyakulu wapi na wapi hawajapewa makisio na makampuni yanaondoka maana yake hiyo mipango tuliyopanga kama kulikuwa na pesa ya tumbaku hatutaipata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa nafikiri Serikali hivi imeshindwa na hawa wazungu wa tumbaku mbona wa korosho wanaweza. Tumbaku tu ndio imekuwa shida, hiyo mipango kama imepangwa na hela ya tumbaku imo nataka nikwambie kwamba tumbaku itakuwa kidogo sana na maeneo ambayo yanalima tumbaku sana hayatakuwa na tumbaku. Mojawapo huko Lyankulu kampuni zinaondoka lakini Serikali imeshindwa majadiliano na hawa watu! Lakini unasikia kabisa wanaenda jirani, wanaenda Zimbabwe manake sisi mipango yetu kwenye kilimo hiki cha tumbaku haiku vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie tena nakushukuru sana na uongozi mzima kwa yale mliyonifanyia na nina imani kabisa nisingeweza kutoka ICU kurudi Bungeni, ningekuja hapa nikiwa ndani ya sanduku ahsante. (Makofi)