Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii kuchangia katika Mpango huu wa Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri na Menejimenti yote ya Wizara kwa kuleta huu Mpango ambao tunataka tuone ni dira ambayo inaweza ikatuondoa tulipo na kuelekea kwingine ambako tutakuwa na taswira mpya ya kuifanya Tanzania hii iwe ni nchi ya uchumi wa kati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi nataka nizungumzie maeneo yale ambayo tunayaita economic tools ambapo tukiyatumia tunaweza kufikia kwenye huo uchumi wa kati mbali na miundombinu na miradi ya kimkakati ambayo inatekelezwa na Taifa. Sina tatizo na miradi yote ya Serikali iliyokuwa imeipanga ya kimkakati, ile miradi mikubwa kwamba itakuwa ni sehemu ya kuifanya Taifa hili liweze kuelekea huko kwenye uchumi wa kati lakini napenda zaidi niishauri Serikali kwani kuna maeneo lazima tutoe lawama kwa kitu ambacho hakijafanyika ili Serikali wasikilize ushauri ambapo utasaidia kutoka kuliko kuendelea kubaki kama tulivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa sekta ya mifugo, Tanzania mbali ya kuwa ni nchi ya pili kwa mifugo lakini bado sekta hii haijafanikiwa. Nimepitia Mpango huu hapa sijaona maeneo thabiti ambayo tunaweza kufaidika na mifugo lakini na fursa ya ufugaji hapa nchini. Kuchunga tunakochunga hakutusaidii chochote hardly pengine tunakwenda kwenye 2% or 3%. Tunataka tuone Wizara ya Mifugo imejikita katika kuhakikisha kwamba inapeleka mfumo wa artificial insemination vijijini ili kubadilisha aina ya ufugaji kwanza, ili kubadilisha ng’ombe waliokuwepo kule ambao wana uwezo wa kutoa nusu lita na lita moja ya maziwa na waende kuwa ng’ombe ambao wanatoa zaidi ya lita 20 na kuendelea, hilo linawezekana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo, tunataka kuona maziwa haya ambayo yanaweza kuzalishwa ndani ya nchi yanafaidisha nchi. Biashara ya maziwa wenzetu wa Zimbabwe ni sehemu ya uchumi wao mkubwa sana na kwa kipindi kile ilikuwa unachangia zaidi ya asilimia 12 lakini sisi Watanzania tumekuwa ni sehemu ya wanunuzi wakubwa wa maziwa kutoka maeneo ya Zimbabwe na sehemu nyingine wakati ndani ya nchi hapa tunaweza kuzalisha maziwa na kuuza na kuyatumia kwa matumizi yetu nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niiombe Serikali na Wizara ya Mipango tuwe na Mpango madhubuti na maalum wa kuhakikisha kwamba tunaweza ku-handle maziwa ambayo yako zaidi ya lita milioni mbili kwa siku yanayozalishwa yageuzwe kuwa bidhaa ambazo zinatumika katika maeneo yetu mbalimbali. Mimi niseme wazi nasikitika sana na mfumo wa biashara ya kupokea maziwa mengi sana kutoka kwa majirani zetu kuingizwa ndani ya nchi kuliko maziwa yanayozalishwa hapa nchini. Ni kitu gani ambacho kinatushinda kuweza kuwa na viwanda ambavyo vinaweza kuchakata maziwa ambayo yako hapa nchini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu handling yake ni gharama, sasa Serikali pamoja na miradi mikubwa ambayo inaifanya ielekeze nguvu sasa katika eneo hili ambapo raw material yake ipo ndani ya nchi ya kutosha na tuache mfumo huu uliopo sasa. Nafikiri iwekwe kodi maalum kubwa ya kudhibiti uingizwaji wa maziwa kutoka nje ili watu waweze kutumia maziwa yaliyoko hapa nchini. Mkiwauliza watu wa Mifugo, hata jana nilionana na Profesa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo bado anasema hakujawa na engagement ya fedha ambazo zinakwenda kutengeneza mitamba ya kutosha ambapo tutaisambaza katika maeneo yetu mbalimbali na kubadilisha taswira ya ufugaji kuwa wa kisasa zaidi kuliko kuendelea kuchunga ambapo tunasababisha ugomvi wa wakulima na wafugaji uliokuwa hauna sababu wakati njia rahisi ya kutumia teknolojia ya kisasa ya ufugaji ipo na hatujaitumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, vilevile nilikuwa naangalia Mpango Mheshimiwa Dkt. Mpango kwa mara ya tatu niseme kwamba bado hatujatumia bahari iliyokuwepo ndani ya nchi hii. Katika dunia hii watu wote wanatushangaa, Mheshimiwa Dkt. Mpango kinachoniuma zaidi nilipata fursa ya kwenda Comoro kama miezi mitatu iliyopita. Comoro wao kama kisiwa wameanza kufaidika na blue sea sisi kwetu bado.

Tuna suffer na 0.4 imekimbiza meli zote, tuna fursa ya kuifanya SUMATRA iweze kukusanya karibu shilingi milioni 40 kwa kila meli iliyokuja kufanyiwa inspection ya kwenda kwenye uvuvi wa bahari kuu na zaidi ya meli 200 hapa duniani zinataka kuja kuchukua leseni lakini kuna kikwazo hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niombe Serikali badala ya kuelekeza nguvu zaidi katika maeneo ya uwekezaji wa reli, umeme na uwekezaji mwingine wowote mkubwa i- engage pesa maalum kwa ajili ya blue sea. I will promise Bunge hili ndani ya miaka miwili break even ambayo itapatikana kutoka katika bahari hakuna sehemu yoyote ya uchumi ambayo itaweza ku-compete. Fedha ziko nyingi na ziko nje nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tunachosema hapa demand inaendelea kuongezeka na kinachofanyika duniani tunatengenewa artificial fish siyo samaki halisi tunaoletewa kwenye makontena hapa na Watanzania tunakula wakati tuna bahari ya kutosha na bado tumeomba kuongezewa eneo la nautical miles 150 la nini sasa kama hatuwekezi? Kama tumeomba tuongezewe eneo basi tuiombe Serikali iwekeze katika bahari ile tuoneshe kwamba na sisi tunayo potential ya kuitumia bahari hii iliyokuwepo hapa na Mungu aliyotujalia tuweze kuleta mabadiliko chanya na tuende kwenye uchumi wa viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe sana kama wanavyoweza kufaidika watu wa Namibia kwa zaidi ya asilimia 11 ya uchumi wao GDP wanategemea samaki ambao wanapenya tu katika mlango mmoja wa Mozambique Current kwenda katika eneo la Namibia na wanaweza kupata fedha ambazo zinaweza kuongezea GDP zaidi ya asilimia 11. South Africa pamoja na uchumi wao mkubwa lakini 8% wanapata fedha kutoka bahari, tunachoshindwa Tanzania ni nini? Mimi nimeuona Mpango halisi huu hapa lakini sijaona mkakati ambao tunaelekea kwenye bahari kuu na kuifanya nchi hii ni sehemu ya nchi ambazo zinauza samaki nchi za nje. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala zima la kilimo. Nchi hii tumejaliwa kuwa na maeneo mengi mengi ya kilimo lakini pamoja na kuwepo na miradi ya SPDII ambayo mpaka sasa hivi hatujaona uendelezwaji wake na kufanya kazi katika maeneo ambayo yanaweza kuleta mabadiliko hayo chanya. Bado mwendo wake nauona unasuasua ingawaje mradi sasa hivi umeshafikia miaka miwili. Ushauri wangu uko hapa, Serikali inatakiwa iwekeze kwenye kilimo cha umwagiliaji maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile niombe Serikali kitu kimoja, mfumo uliopo hivi sasa wa kujenga canal irrigation hautusaidii kitu, unakula fedha nyingi na unachukua muda kumalizika na wakandarasi ndiyo sehemu ambayo wanaweza kupata pesa bila ya sababu.

Kwa ushauri wangu mimi tuzuie fedha zote zinazokwendwa kwenye canal irrigation ambapo tunaweza tuka-save zaidi ya asilimia 70 kwa kutumia pipe irrigation ambazo unaweza kuwekeza kwa muda mfupi tu. Wiki mbili tu unajenga zaidi ya hekta 200 au 100 kwa kutandika mabomba ukaweza kuhifadhi maji na akatumia maji ambayo hayawezi kupotea. Tukitumia mfumo huo tuaweza ku-control ile wanaita Evapo-transpiration lakini vilevile contamination ya wadudu, maradhi, magugu na vitu vingine vyote tutaepuka. Hiyo ndiyo teknolojia tunayotaka twende na dunia huko ndiko iliko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo kuendelea kujenga mitaro kwa mawe na saruji ambayo baada ya muda wakandarasi wanapiga hiyo pesa na hakuna kinachoendelea, niseme wazi kwamba huko sioni kama kuna tija na hakuwezi kutufikisha. Tutumie njia rahisi ambapo tutaweza kuzalisha na kuyatumia maji effectively kuliko hivi sasa. Kwa hiyo, niiombe sana Serikali katika mipango yetu yote hizi billions of money zinazokwenda kwa ajili ya kutengeneza canal za irrigation tuelekeze kwenye pipe irrigation ambacho ndicho kilimo cha kileo zaidi kuliko huku tunakokwenda.

MWENYEKITI: Muda wako umeisha Mheshimiwa.

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja. (Makofi)