Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Hon. Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti nikushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii niweze kuchangia kidogo kuhusiana na mapendekezo ya mpango wa maendeleo ya Taifa kwa mwaka 2020/2021 ambao ndio utakuwa umefika ukomo wa kipindi cha miaka mitano kwa huu mpango wa pili ambao tumeanza kuutekeleza tangu 2016/2017.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha na timu yake kwa kutuletea mapendekezo haya na wewe umesema sasa hivi vizuri sana huu ni mwendelezo katika utekelezaji wa mpango wa pili wa maendeleo ya Taifa ambao tumeingia sasa huu mwaka wa nne. Ni kweli lazima tu-take stock na ndio maana Serikali inakuja hapa na mapendekezo haya. Sisi kama wadau kama sehemu ya uongozi wa Taifa hili ambao tumeaminiwa na watanzania wema katika nyumba yao hii tuweze kuona namna ya kuboresha, kuishauri Serikali ndio kazi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru sana Waheshimiwa Wabunge waliotangulia katika kuchangia tuisaidie Serikali maana nikilalamika nikishamaliza kulalamika kwani itakuwa imesaidia? Saidia kuonyesha njia, mimi nadhani tukienda hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa haya makubwa inayoyafanya sasa unaweza usione muunganiko wa moja kwa moja kwa maendeleo ya mwananchi mmoja mmoja kwa Bwawa la Nyerere la kufua umeme. SGR inayojengwa hata ndege hizi zinazonunuliwa lakini nawaambieni miradi hii itakapokamilika suala tunalosema la tija, ufanisi kwenye viwanda vyetu, umeme ndio kichocheo kikubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia reli hii ambayo nitaisemea sasa hivi reli ya kati ndio kiini ni injini ya ukuaji wa uchumi wa mataifa yote na ndege hizi utalii watanzania Mwenyezi Mungu ametujalia kitu ambacho lazima tuendelee kukinufaika, tunufaike nacho sasa na kesho na kesho kutwa. Pesa hiyo ndio inayoenda kusaidia kuboresha huduma za jamii kama afya, maji yote haya ambayo tunayaongelea kwa faida ya watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sitaki kuchukua muda mwingi kwa hilo lakini sisi kazi yetu tuishauri Serikali katika maeneo ambayo tunadhani tunaweza tukafanya vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na hili la kilimo, limesemwa vizuri sana kwenye taarifa ya waziri aliyowasilisha; niseme pia ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti tumeyasema sana lakini nashukuru taarifa ya Kamati ya Bajeti. Waheshimiwa Wabunge isomeni lakini tumeongea sana na Serikali kwenye kamati kusaidia haya mawazo na sisi tunabaliana na wengi mnaosema kwenye kilimo, kwenye uvuvi, kwenye mifugo huko tukiweza kuboresha hayo maana ndio sekta ambazo ukinyanyua hizo ndio zinaunganisha na zinachochea ukuaji wa sekta nyingine ifanywe vizuri kwenye kilimo nasema kilimo cha Tanzania kama tutafanikiwa kikuwe kwa kasi asilimia sita na tukawa persisted kwa kipindi kirefu miaka 10, 20 utaona mchango wake kwa Pato la Taifa tulikuwa kubwa sana na ndio itabeba wananchi wengi kuwaondoa katika lindi la umasikini, mipango ndio hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimia naomba sana katika vipaumbele vya mwaka kesho tuweke intervention kubwa tupeleke kwenye kilimo pia kwenye mifugo, kwenye uvuvi ionekane kwenye bajeti yetu kwenye sekta hizo kupitia mpango huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naelewa Serikali maana tunamaliza mpango huu wa pili mwakani ndio tutakuwa Bunge litakuwa karibu linakaribia kuvunjwa lakini Tanania ipo itaendelea kuwepo wananchi wa Tanzania watakuwepo na Serikali itaendelea kuwepo na Bunge la Tanzania litaendelea kuwepo, kwa hiyo watakaorejea tunataka tuje tuone angalau ifanyike tathimini ya kipindi tuone mpango wa pili wa miaka mitano ambao tulikuwa tumemaliza kuutekeleza kipindi hicho tunapoenda kwenye mpango wa tatu wa maendeleo ya Taifa letu tuone ni nini ambacho tumefanikiwa sana, nini maeneo gani hatukufanikiwa sana, nini kifanyike ili tunapoenda kwenye mpango huo wa tatu na wa mwisho tuwe kweli confidence.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali hata katika hatua hii kwa sababu kupanga mwalimu alikuwa anatukumbusha kupanga ni kuchagua tungekuwa na rasilimali nyingi ambayo unaweza kutekeleza yote haya kwa wakati mmoja tungeweza kufanya hivyo lakini hatuna lazima kile kidogo ambacho tumekubaliana kukifanya tukifanye kwa ufanisi na ndio maana mimi nasema naelewa baadhi yetu tungependa tuone mambo tunasema haya ni mengi mno tuliyoyabeba, lakini utafanyaje Tanzania hii nchi ni kubwa tuna wananchi milioni karibu 53,000,000 lazima uende hivyo unaumia hapa kidogo lakini huko mbele wengine panaenda vizri, ukifanya stock nzima unasema Tanzania inasonga mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa reli concern yangu iko kwenye taarifa ya bajeti kama ripoti ya taarifa ya bajeti Kamati ya Bajeti tunafanya vizuri tumetumia pesa ya ndani jasho la Watanzania kutoka Dar es Salaam mpaka Morogoro heshima kubwa kwa nchi hii heshima ehee! Tujivunie wananchi pesa ya ndani tumekopa kutoka Morogoro kuja Makutupora ndio lakini ni mkopo wetu wa Watanzania. Na tunajiandaa sasa tutafute pesa nyingine kutoka Makutupora kwenda Tabora, kwenda Isaka, kwenda Mwanza na baadae kwenda Tabora, kwenda Kigoma, Uvinza Msongati tutatoka Kaliuwa, Mpanda tuende mpaka Kalema, ndio mipango yetu hii kalema kwenye Lake Tanganyika tuna mipango tunaiona Tanzania na majirani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nini concern yetu na ndio imo kwenye taarifa ni kwamba tunachukua mikopo hii bahati mbaya ni ya muda mfupi, masharti yake ingependeza kama tungeshambulia reli hii, ujenzi wa reli hii kwa wakati mmoja kwa sababu tunajua pesa hizi kwa kupata mkopo wa muda mrefu itakuwa ni ngumu sana lakini tukiweza vipande hivi tukavishambulia kwa wakati mmoja tutakuwa tumekamilisha ujenzi wa reli hii na matawi yake muhimu haraka sana na ndio tutaona faida, ndio ushauri wetu huo kwa Serikali. Naelewa misaada imepungua sana, mikopo ya masharti nafuu imepungua sana, eneo ambalo tunaweza tukapiga hodi na nadhani tumekaa vizuri ni kwenye export credits iwe ni ya Waingereza ya Wafaransa ya Wajerumani angalau ukipata mkopo ule mpaka miaka 21 window hiyo ipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri naiomba Serikali tuangalie option hizo tutafanya vizuri na kwenye reli nasema reli hii tuikamilishe naomba sana Serikali reli hii ya Kati tuikamilishe na ningependa sana ndoto aliyonayo Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli aikamilishe reli hii wakati wa uongozi wake heshima kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho tuna miradi mikubwa kwanza nipongeze kazi nzuri ya Dar es Salaam Bandari Port Gati moja mpaka namba 7 ile kazi inaenda vizuri, tunapanua lango pale kuingilia kazi nzuri. Mtwara inaenda vizuri sana is the natural Port Mtwara is the deep sea Port ehee nashukuru sana Magati yale yanaongezeka. Tanga ya sasa na sawa tunawekeza kwenda toka mita depth ya mita
4 kwenda 15 lakini Mwambani ndio yenyewe Tanga Mwambani ndio kwenyewe eehe tuangalie huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini narudia kama kwa Bagamoyo tumeona muwekezaji huyo hafai haimaanishi kwamba mradi wa Bandari ya Bagamoyo haufai hapana, tutafute muwekezaji mwingine ambaye ataendana na matakwa yetu ili bandari ya Bagamoyo ijengwe ndio matumaini ya Taifa hili Dar es Salaam pamoja na maboresho yanayoendelea hatutaweza kupata meli zile kubwa za tani kuanzia 50,600 yale yanaitwa ports kwanama yale hayawezi kuingia kwenye lango la Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho naomba Liganga na Mchuchuma tukamilishe mazungumzo kama imeshindikana na muwekezaji huyo tutafute mwingine lakini hii taarifa hii kila mwaka tunarudi nayo mpaka tunataka kumaliza miaka mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, najua muda wangu ndio huo lakini mimi naipongeza sana Serikali Mheshimiwa Waziri wa Fedha na timu yako hongereni sana tuwaunge mkono najua changamoto ni mapato tuwasaidie ni maeneo yapi tunadhani tunaweza tukaongeza to argument mapato ya Serikali ya ndani hasa mapato ya ndani ya kodi ya siyo ya kodi mnaona tangu tuanze matumizi ya ufanisi wa electroniki, mapato yanaongezeka ya kodi lakini pia na yasiyo ya kodi. Nadhani likisimamiwa vizuri tutaweza kupanda kutoka kwenye trilioni 1.2 ambao tumegota kidogo sasa na tukaweza kuongeza mapato yetu. Tuangalie maeneo mengine ameyasema vizuri Mheshimiwa Masoud eeh! Bahari ya Hindi tutumie, blue economy ya Tanzania hiyo hiyo tuichukue vizuri tufanye mambo makubwa, inawezekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umenipa heshima umenivumilia mchango wangu ni huo tuhimize tufanye maamuzi ya haraka katika maeneo ya vipaumbele ambayo tumejiwekea sisi wenyewe nakushukuru sana ubarikiwe sana. (Makofi)