Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuendesha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo

Hon. Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuendesha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo

MHE. MUSSA A. ZUNGU – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA: Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kukushukuru tena na kuwashukuru Wabunge Sita waliochangia ambao ni Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha, Mheshimiwa Ally Saleh Ally, Mheshimiwa Amina N. Makilagi, Mheshimiwa Victor K. Mwambalaswa, Mheshimiwa Peter Serukamba, tumemalizia na Mheshimiwa Agness Marwa.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha ameunga mkono na ametoa history ya namna Frontline States ilivyoanzishwa, ni kweli zilikuwa ni nchi Tano ni kama vile alivyozisema Tanzania, Botswana, Angola, Msumbuji na Zambia. Ameunga mkono na ameendelea kusema kuwa nchi hizi sasa zikumbuke namna Tanzania ilivyojitoa na tuendeleze kujitoa kuhakikisha sasa tunajitoa kwenye masuala ya uchumi. Mheshimiwa Makilagi nae ameunga mkono, amezungumzia namna Mheshimiwa Rais alivyozungumza kwenye hotuba yake tujitegemee. Mheshimiwa Victor Mwambalaswa ameendelea kutoa history kabisa ya namna Mwalimu alivyopambana na kuzungumza utawala wa kibeberu Afrika uondoke.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Ally Saleh naye amepongeza, amezungumza kuhusu namna ushiriki wa Tanzania kwenye Mabunge haya. Hata hivyo, nataka nimkumbushe Mheshimiwa Ally Saleh Wabunge wetu wanashiriki kwenye mikutano ya Bunge la Afrika na hata Makamu wa Rais wa Bunge hilo la Afrika anatoka Tanzania, kwa hiyo hii inaonesha Wabunge wetu wanakwenda na wanashiriki.

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Peter Serukamba ameunga mkono, amezungumzia masuala ya uchumi, amepongeza na suala la utulivu wa nchini mwetu, amesisitiza kwa suala la sekta binafsi nayo itiwe mkazo na amezungumzia, amekumbusha kuwa legacy ya Mheshimiwa Rais katika SADC katika mambo yote lakini haitasahahulika kwa Kiswahili kimeweza kuwa kitatumika na kitaweza kukua.

Mheshimiwa Spika, watu lazima wakumbuke Tanzania tunapotoka. Kama mtakumbuka tarehe 11 Novemba, 1965 Rhodesia chini ya Ian Smith walitangaza UDI (Unilateral Declaration of Independence), Tanzania ilikuwa ni nchi ya kwanza kupinga utawala huu dhalimu na Tanzania wakaomba Uingereza wasiitambue Serikali ya Ian Smith ya Rhodesia, lakini Harold Wilson wakati ule akiwa ni Waziri Mkuu wa Uingereza walikataa na palepale Mwalimu Nyerere akavunja uhusiano na Uingereza. Kuonesha namna gani gani Rais Nyerere alikuwa na uchungu na ukombozi wa Afrika, tulikataa misaada kutoka Uingereza. Hii inaonesha namna Tanzania ilivyokuwa mstari wa mbele katika kupambana na udhalimu wa nchi hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Tanzania ilichelewesha maendeleo yake ili kuhakikisha nchi za Afrika zipate uhuru wake, kwa hiyo damu ilimwagika na watu wengi walipoteza maisha yao. Sasa tunaliagiza kwenye Azimio letu na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kufuatilia hasa maelekezo ya Mheshimiwa Rais kuhakikisha trading within block ya SADC inafanywa na tuna-trade kwa kiwango kikubwa sana.

Mheshimiwa Spika, takwimu zinaonesha sasa hivi ndani ya Afrika tuna-trade kwa asilimia 16 tu, tofauti na nchi za Ulaya zina-trade kwa asilimia 70 wenyewe kwa wenyewe. Ili tujikomboe lazima tuanze kutafuta masoko ya ndani ya kujikomboa na kuhakikisha bidhaa zetu za kilimo na bidhaa zetu nyingine zinanunuliwa na Waafrika wenyewe.

Mheshimiwa Spika, nichukue nafasi hii kukushukuru, na sasa niwaombe Wabunge wote kwa pamoja kwa Kambi zote ambazo ziko ndani tuunge mkono azimio hili na tumpongeze Rais wetu kuchukua nafasi ya kijiti hiki na inawezekana akaendelea tena kuchukua kijiti hiki kwa mwaka mwingine unaokuja kutokana na kazi nzuri anayoifanya na kutokana na nchi za Afrika kumkubali na kumtegemea yeye kutuongoza wote. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. SHAMSI VUAI NAHODHA: Mheshimiwa Spika, naafiki.