Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuendesha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo

Hon. Agnes Mathew Marwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuendesha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo

MHE. AGNESS M. MARWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia hoja hii.

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC. Hii ni heshima kubwa kwetu kama Wabunge, lakini ni heshima kubwa kwa Watanzania na nchi kwa ujumla. Mimi niseme hii nafasi sasa imempata mkunaji maana sasa imefika mahali pake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa sababu ameanza vizuri. Ukweli ni kwamba Watanzania bado lugha ya kigeni Kiingereza na lugha nyingine, zilikuwa ni lugha ambazo zilikuwa zinaleta shida sana kwenye mikutano na sehemu mbalimbali kutokana na kwamba ni lugha ambazo tulikuwa hatuzijui vizuri, tulikuwa hatufundishwi tangu utotoni. Kwa hiyo, nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, niungane na Mbunge mwenzangu kusema kwamba ni kweli atakuwa ameacha legacy katika Jumuiya hii ya SADC.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia kwa Tanzania tumekuwa mstari wa mbele chini ya uongozi wa Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika harakati za kutafuta uhuru wa baadhi ya nchi za SADC. Kwa kweli tumewasaidia nchi nyingi sana kiasi kwamba Uenyekiti ulipofikia umefikia mahali pake, kwamba nasi sasa tuonekane kwa yale tuliyoyafanya, kwamba sasa hivi tunaweza kufanya kitu gani.

Mheshimiwa Spika, sina shaka sana na Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa uongozi alioupata wa SADC, kwa sababu Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli naamini kabisa ataondoa ukiritimba katika masoko ya biashara. Kwa mfano, kule kwangu Mkoani Mara unaweza ukafanya biashara ama za nafaka au biashara ya dagaa niliyokuwa naifanya mimi kutoka nchini kwetu kuvuka mpakani kunakuwa na ukiritimba lakini kunakuwa pia na masuala ya rushwa. Sasa naamini kabisa chini ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli rushwa itakoma na hizo nchi washirika naamini kabisa watamtambua kwamba huyu ndiyo Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba Mheshimiwa Rais wetu ni kati ya vivutio na hasa katika nyanja ya uongozi, kwa sababu ni kiongozi bora, ana uongozi uliotukuka, Wabunge pia tumeiga kutoka kwake, mfano; Kama unakumbuka safari hii likizo ya Bunge lililopita kila Mbunge amekuwa akifanya kazi na hii yote ni kutokana na uongozi wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, kwamba asiyefanya kazi na asile na ambaye hajafanya kazi kwa kweli kuliona hili Bunge mwaka 2020 asahau. Kwa hiyo, huu uongozi safari hii umempata mwenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia nimpongeze sana Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa hili suala la viwanda maana yeye alipochaguliwa tu alisema kaulimbiu yake ni Tanzania ya Viwanda, lakini kumbe ni Rais ambaye ana maono makubwa na ndiyo maana tunasema tumepewa Rais ambaye ametoka kwa Mwenyezi Mungu kwa sababu hapohapo ukiangalia imeunganishwa kwamba sasa SADC pia wameongelea suala la viwanda na kukubaliana. Hivyo, naamini kabisa viwanda sasa vitakuwa vingi sana, mfano wake nimwambie hata Mheshimiwa Neema Mgaya kile kiwanda chake cha vyerehani Kumi sasa akianzishe kwa sababu haya mambo yote yanafanyika kutokana na makubaliano ya SADC.

(Maneno hayo yalifanyiwa marekebisho na Mheshimiwa Neema W. Mgaya na kusomeka Vyerehani 370 na siyo Vyerehani Kumi)

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Wabunge wenzangu au wapiga kura wangu wa NEC ambao ndiyo Wabunge, pamoja na wananchi wangu wa Mkoa wa Mara, na hasa Wabunge wa CCM, napongeza sana kwa kweli uongozi huu wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, imani yangu ni kwamba sasa atafanya mabadiliko makubwa na watauona uongozi wake uliotukuka ambao Tanzania tunajivunia.(Makofi)
Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, ahsante.