Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuendesha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo

Hon. Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa SADC na kuendesha vyema Mkutano wa 39 wa Jumuiya hiyo

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Nami kama wenzangu waliotangulia, naunga mkono azimio hili lililowekwa mezani. Azimio hili linatukumbusha historia ya ukombozi katika Afrika. Tanzania iliongoza nchi za Kusini mwa Afrika ili nchi ambazo hazijapata uhuru zipate uhuru Mwalimu Nyerere akiwaongoza. Tulianza na Mlungushi Club ambayo alikuwa anaiongoza Mwalimu Nyerere, lakini Mabeberu wakaipiga vita nchi nyingine zikawa zinajipendekeza kwa mabeberu, ndiyo Mwalimu akaanzisha nchi za mstari wa mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, bahati mbaya nchi za mstari wa mbele zipo nchi zilikuwa zinajitegemea Afrika Kusini kiuchumi. Kwa hiyo, Mwalimu akaona afadhali aache mstari wa mbele, ndiyo ikaazishwa Southern African Development Coordination Conference ili hizi nchi za Kusini mwa Afrika zisianze kujitegemea kijuchumi, ziachane na Afrika Kusini. Baada ya kuanzisha hii Southern African Development Coordination Conference, nchi za Ulaya na Marekani zikaanza kutambua kundi hili, likaanza kumpa pressure Afrika Kusini iachane na ubaguzi. Ndiyo ikakua ikaanza Southern African Development Community yote hii ikiongozwa na Mwalimu Nyerere. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vijana wa sasa wakitaka kuelewa Mwalimu Nyerere alikuwa champion wa uhuru katika Afrika, wasome kitabu chake cha Crusade for Liberation, utaona Mwalimu alivyojitoa ili Afrika yote ipate uhuru. Kuwepo kwa Southern African Development Community ndiyo kumeleta ukombozi Zimbambwe na Afrika Kusini.

Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Rais. Marais hawa waliokuja kwenye mkutano wa juzi, Rais Cyril Ramaphosa na Rais Mnangagwa angalau wanatambua umuhimu wa Tanzania kuleta mkombozi Kusini mwa Afrika.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, bado kwenye mkutano huo Tanzania ikiongozwa na Rais wetu pamoja na Waziri wa Mambo ya nchi za Nje inaendeleza mapambano ya kuikomboa Zimbabwe ili vikwazo viondolewe na Zimbambwe. Bado Tanzania iko… (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Azimio hili ni nzuri sana linatukumbusha Champion wa Tanzania katika kuikomboa Afrika. Yote haya ni mazuri, naunga sana mkono, nasema, boseaga maswano muno muno munze yetu. Muaha yalumbwe. Sendenyi. (Makofi/Kicheko)