Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nianze na jambo moja hapa. Hakuna kanuni yoyote ya Bunge hili ambayo inamzuia Mbunge kuzungumza kuhusu Waziri yeyote kwenye hili Bunge. Kwa hiyo naomba tafadhali tanapokuja hapa tunalipwa pesa za walipakodi wa nchi hii ili tufanye kazi yao. Sasa haya mambo ya kusumbua watu wakati wanachangia sio mazuri. La kwanza hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, tumezungumza sana kuhusu kilimo, wazungu walipotaka kuanza kuendelea Agrarian Revolution ndio ilikuwa ya kwanza karne ya 16. Kati ya mambo makubwa mawili ambayo Serikali yenu kuyasabishwa yamedharaulika katika nchi hii ni kilimo na ualimu, ambayo ni mambo ya muhimu kweli kweli. Ukiangalia mwanafunzi anayekaribia kufeli shule utasikia familia yake inamwambia ameshindwa hata ualimu, ndipo mlipoufikisha ualimu wa nchi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo, mtu akikaribia kuonekana hawezi kusoma vizuri wanamwambia utarudi kupiga jembe, kilimo ndicho kinawatajirisha watu na ndicho kinachotoa chakula cha 100% kwa watu, kinatoa ajira 80%, kinatoa malighafi za viwandani na kilimo ndio kila kitu. Sasa wamefanya vice versa na ndio maana tukiwaacha kuendelea kuiongoza nchi hii hata miaka 1,000 hamuwezi kutuondoa hapa, hata miaka 1,000. Ndio maana mwaka 2015 wakati Serikali hii inayojiita ya wanyonge inaingia madarakani, bei ya kahawa pale Tarime ilikuwa Sh.2,200. Sasa hivi tunavyozungumza Mheshimiwa Hasunga bei ya kahawa ni Sh.800, are we moving forward au tunarudi nyuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama bei ya kahawa ni Sh.800 kwa wakulima ambao wameanza kujitegemea, kwa wakulima ambao alikuja Naibu Waziri Tarime, wamechukua kahawa ya wakulima watu maskini Kata za Muriba, Itiryo, Mbogi, kata nyingi tangu mwezi wa Saba mwaka jana hawajawalipa mpaka leo na wanasema wao ni Serikali ya wanyonge. Halafu wanasimama watu humu kwa sababu wao wanalipwa pesa za kodi ya watu maskini, wanafungiwa mikanda kwenye gari, wanajisahau wanajiona ma-queen na ma-king, wanasahau kwamba hizo ni pesa za walipakodi maskini, sasa wanasimama huku, wanawafanyia maudhi Watanzania waliowapa huo ukubwa wanaotamba nao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni aibu kwamba Waziri anaweza kusimama hapa akapinga kwamba Watanzania hawazidi kuumia kwa sababu ya aina ya jinsi mnavyochukulia Kilimo. Sasa leo mmechukua kahawa ya watu, mwezi wa saba. Nani angeambiwa hapa tangu mwezi wa saba hatulipwi posho au hatulipwi mshahara kama mngekanyaga hapa, hata hela za mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na Watanzania wajue, mpaka mafuta mnayokwenda nayo Bungeni na kurudi mnalipwa na Watanzania. You are being paid millions of money za walipa Kodi maskini; sasa tunaposimama hapa, hebu tuwafikirie pia waliotusababisha tukaja hapa, la kwanza hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuhusu Korosho. Katika hili naanza kwa kuweka mezani kwako hapo watu wako wachukue, gazeti la Daily Nation la Kenya la tarehe 12 lilisema Serikali ya Tanzania yaingizwa chaka na kampuni ya kihuni ya Indo power, ambayo leo mnataka mui-protect. Ninataka niwaambie, hamtai-protect mkii-protect humu tunazungumza nje. (Makofi) (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua, hiyo zabuni ya kuanza kuzungumza na hiyo Kampuni ilitangazwa wapi? La kwanza hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, nani aliyekuwa anafanya mazungumzo ya awali na hiyo Kampuni ya Indo power, ambayo gazeti hili la Daily National linasema halina hata ofisi kule Kenya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa na hili ni jambo la aibu, na tunakuja humu mambo makubwa tunayafanya mambo madogo kwa sababu ya mizaha. Sasa nataka mtuambie hivi kama gazeti mwandishi mmoja tu anaweza kufanya uchunguzi akajua hii Kampuni haina ofisi, ni Kampuni ya kitapeli, Serikali nzima mnampeleka Gavana wetu wa Benki Kuu pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mnapeleka Mawaziri watano, mko hapa kwenye picha, mlikuwa pale, akiwemo Profesa Palamagamba Kabudi, ambaye mnam-protect hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nani alianza kuzungumza na hiyo Kampuni? Nataka mtuambie je, hiyo Kampuni, yaani gazeti la Daily National la mwandishi lina uwezo wa kuchunguza kuliko Serikali yetu? Muwaambie Watanzania, muwaambie Watanzania na kama si hasara mtuambie; unakuja unatuambia hapa Kabudi anasema eti huyu mtu alikuja na ndege, so what? Mimi na Esther Matiko tunakodi helicopter tunaenda Tarime, kwa hiyo sisi ni wawekezeji? (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eti, kwani, yaani mawazo yenu, Waziri kabisa anasimama, eti hii ni Kampuni nzuri kwa sababu huyu mtu ni Mwekezaji, serious amekuja na ndege. Freeman Mbowe huyu anamiliki Caravan, Godbless Lema anamiliki Ndege ya watu 16, sasa na yeye ni Mwekezaji? (Makofi/Kicheko)

MBUNGE FULANI: Gwajima.

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Gwajima, amepaki pale Helicopter yake. (Kicheko/Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa Heche, Mheshimiwa Heche ongea na Kiti wewe, changia, changia. Jielekeze kwenye hoja sasa, mambo, jielekeze kwenye hoja. (Kicheko)

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hii Kampuni ilipatikanaje?

MBUNGE FULANI: Dakika za Heche….

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya ni mambo ya muhimu tunataja kujua, nani alianza kuzungumza nao? Tunataka kujua; common sense ya kawaida, ukimsikia Profesa Palamagamba Kabudi, na Gavana wa BOT Profesa common sense inakataa, kwamba hawawezi kufanya maamuzi ya vile, kama si rushwa basi hawawezi kuongoza hata kibanda cha kuuza nyanya hawapaswi kuongoza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawapaswi kabisa, na hili suala Watanzania maskini…

MWENYEKITI: Mheshimiwa Heche, hivi mnataka nifanye nini sasa? Nimeshaitolea uamuzi, you may not like my ruling lakini ndio uamuzi wangu.

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa. Kule Kusini kuna Watanzania wenzetu ambao ni wakulima wa korosho, na sisi Wabunge tuko hapa ku-protect watu wetu. Kuna Watanzania kule korosho ndio mshahara wao, kama ninyi mnavyolipwa kila mwisho wa mwezi. Korosho ndiyo karo ya watoto wao, Korosho ndiyo malipo ya benki wanayodaiwa wamekopa wamejenga. Kwa hiyo tunapozungumza haya masuala tuyazungumze kwa uzito huo. Ndiyo maana sisi tunasema, kama alivyosema mtu anayekaimu nafasi Waziri Mkuu; kama kweli Serikali nzima, mna collective responsibility na mnakubali kwamba kosa la kuingiza nchi kwenye aibu gazeti la Kenya linatuandika. Pamoja na mambo yote tunayoweza kufanya humu, Rais wa nchi, nje ya nchi ni Symbol ya nchi, na tutam-protect. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa gazeti hili limesema, pamoja na kwamba umesema hivyo, wewe tunaamini kauli yako ni ya Waziri Mkuu. Leo kama mna uadilifu wa kutosha, Serikali nzima resign kwa sababu mmeaibisha nchi yetu vya kutosha kwa kwenda kuingia na Kampuni…. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)