Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

Hon. Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Kilimo

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nizungumze mambo mawili. Jambo la kwanza ni kuhusu kilimo cha parachichi; naomba niishauri Serikali, Nyanda za Juu, hasa Iringa ni corridor ya parachichi duniani na naomba tafiti zilizofanyika wahakikishe wanazifanyia kazi kubwa kwa ajili ya kuhakikisha wakazi wa Iringa na maeneo mengine wananufaika na zao la parachichi. Naomba sana wasifanye business as usual kwa sababu wanatumia methods zilezile, ulimwengu ume-change, wanafikiri vilevile, change namna ya kufikiri kulingana na ulimwengu unavyokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, katika kitabu cha hotuba yetu ukurasa wa 24 tumezungumza jinsi ambavyo Mheshimiwa Profesa Kabudi na Gavana wa Benki walisimamia kwenye kuandika ule mkataba wa wanunuzi wa korosho. Profesa ni authority, profesa ni mtu ambaye inatarajiwa kwamba anajua mambo mengi, anajua namna ya kufikiri na Mheshimiwa Rais katika Serikali ya Awamu ya Tano amefanya kazi nzuri sana ya kuwaleta wasomi, Maprofesa na Madaktari, tunategemea Madaktari na Maprofesa wanapofanya maamuzi lazima wanakuwa wamepanuka sana ili wasilipotoshe Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo la kutia aibu mahali ambapo mtu kama Mheshimiwa Profesa Kabudi amekaa, wamekuja na ile kampuni ya kitapeli kabisa, Rais amewaamini kampuni ya kihuni wanalitangazia Taifa kwamba kila kitu kitakuwa safi, korosho itanunuliwa, halafu korosho haijanunuliwa. Hili ni jambo la aibu, hatuwezi kulifumbua macho, lazima Mheshimiwa Profesa Kabudi ajiuzulu kwa kulipotosha Taifa. (Makofi)

MWENYEKITI: Mheshimiwa.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni jambo la aibu sana hili. (Makofi)

MWENYEKITI: Hebu ngoja. Mheshimiwa Mchungaji Msigwa, wewe ni term yako ya ngapi Bungeni?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Naam?

MWENYEKITI: Muhula wa ngapi huu?

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Wa pili.

MWENYEKITI: Ahaa, kwa hiyo unajua sana mambo.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Ndiyo.

MWENYEKITI: Haya.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimem-single out Mheshimiwa Profesa Kabudi alikuwa Waziri wa Katiba na Sheria, kwa hiyo we expected kwamba yeye angetu-guide na angem-lead Rais katika njia iliyo sahihi, he was responsible for that Ministry, hatuwezi kum-spare. Amelipeleka Taifa kwenye sintofahamu kwa ku-mislead nchi, ni wajibu wake kusimama hapa na kusema kitu gani kilifanya aingie kwenye mkataba wa hovyo na nchi hii, lazima… (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kuhusu Utaratibu.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Mchungaji Msigwa nimeshaliamulia, sasa unarudi hukohuko, usinilazimishe niangukie kwenye Kanuni ya 73. Haya.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba Serikali imekubali kwamba inawadanganya wananchi wa Mtwara na korosho, ina- mislead Taifa la Tanzania na kuwapa ahadi hewa… (Makofi)

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu.

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: …kwa sababu inaingia kwenye mikataba ambayo haitekelezeki.

KUHUSU UTARATIBU

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ninayoijenga hapa, Serikali ina wajibu wa welfare za wananchi. Serikali imesababisha tuko foreign, forex imeshuka kwa sababu ya mipango ya hovyo ya Serikali kuhusiana na korosho. For the first time ninyi Mawaziri, amesema hapa Kaimu Kiongozi, walimshauri Rais wakaamua kutumia Jeshi kuchukua korosho, anakuja Waziri hapa anasema eti anayeleta mkataba amekuja na ndege, anashangaa na ndege, mbona ana caravan hapa, what is ndege? Wanamshangaa eti kwa sababu amekuja na ndege ndiyo wanaingia kwenye chaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii Serikali lazima wasimame waombe radhi kwa wananchi, mnaharibu kilimo, wamewa- cripple wananchi kwa sababu ya mikataba ya hovyo, watu wengine kule Mtwara wameshindwa kupeleka watoto wao shule. Walikusanya korosho zao halafu wanasema hapa tuwapigie makofi. Mawaziri waliohusika na Waziri wa Katiba anatakiwa a-step down, amei-mislead nchi. Kuna wengine wamekufa watoto wao wameshindwa kupeleka shule halafu wanasema hapa tusiseme, tumekuja kufanya nini hapa, shame on you Government. (Makofi)