Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kupata nafasi hii na mimi mkono hoja. Nampongeza na Mheshimiwa Waziri, Katibu Mkuu na watendaji wa Wizara kwa kazi kubwa na nzuri wanayofanya. Nawapongeza sana Jeshi la Wananchi kwa kazi kubwa wanayofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo amesema Mheshimiwa mchangiaji Dkt. Mwakyembe, Jeshi limekuwa sehemu ya kimbilio sana. Tunapokuwa tunapata majanga makubwa katika nchi hao ndiyo watu ambao kwakweli wanakuwa multipurpose wanafanya kazi hiyo kwa ufanisi mkubwa, lakini vilevile tunapopata mafuriko maeneo mbalimbali wanashiriki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshuhudia hivi karibuni ukiacha shughuli kubwa ambayo wanafanya hata nje ya nchi kujenga heshima na utashi wa Tanzania na uzalendo uliotukuka, wamekuwa wakitumwa katika maeneo mbalimbali kwakweli hatujawahi kupata malalamiko kutoka huko ambako wanafanya kazi, maana yake wanabeba uzalendo, wanawakilisha nchi yetu vizuri sana na kupeleka sura chanya ya Jeshi letu nje ya mipaka ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Rais pamoja na kwamba Jeshi wanafanya kazi lakini amewapa nafasi kubwa wamefanya kazi kubwa sana ya ujenzi wa nyumba za Serikali, sasahivi wanajenga majengo hapa ya Mji Mpya wa Serikali pale Mtumba, lakini wamekabidhiwa majengo kule kwetu Ukonga, Jimbo la Ukonga pale tunashukuru sana, lakini kubwa zaidi ni kitendo cha ushujaa Mheshimiwa Rais aliona ambacho alikuwa anafanya yule Ndugu Charles Mbuge na akampandisha kuwa Brigadier General jambo kubwa sana kwa kazi kubwa anayofanya. Hii maana yake aatia nguvu wanajeshi ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa sana. Tunawathamini, tunawaheshimu waendelee kufanya kazi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema namna hiyo, nashukuru sana naunga mkono hoja. Nawapongeza sana wanajeshi na Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi kwa kazi kubwa na nzuri anayofanya. Ahsante sana. (Makofi)