Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. ENG. RAMO M. MAKANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pongezi; hongera sana kwa Wizara, Mheshimiwa Waziri na wasaidizi wake wote Wizarani. Pia hongera kwa Jeshi letu kwa upana wake ikijumuisha uongozi wa ngazi zote. Hongera sana kwa kazi iliyotukuka, sio tu kwa kuendelea kulinda mipaka yetu, bali pia kwa kuendelea kuingilia kati katika kazi na majukumu mbalimbali ya kijamii na kiuchumi kama vile ujenzi/urudishaji wa huduma za dharura kufuatia maafa, kuharakisha utekelezaji wa majukumu ya Serikali Kuu, zoezi la ukusanyaji korosho na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, teknolojia zilizopitwa na wakati; nimesoma changamoto hii katika hotuba ya Mheshimiwa Waziri (hotuba ya bajeti) katika vifaa, mitambo, vitendea kazi na kadhalika, ni jambo la kuendelea kuishauri Serikali kuendelea kuboresha bajeti ya Wizara ya Ulinzi, lakini kwa upande mwingine nashauri Wizara iboreshe mpango wa elimu endelevu kwa wataalam waliopo (Continuing Professional Development (CPD) na kuzalisha wataalam kulingana na mahitaji. Hii itasaidia uendelevu (sustainability).

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipaka; katika mpaka wa Kusini wenye jumla ya kilometa 1,536 Wilaya ya Tunduru ni sehemu yake (eneo la kandokando ya Mto Ruvuma), kutokana na ishara za kukua kwa changamoto za kiulinzi katika mpaka nashauri Kambi ya Jeshi iliyokuwepo katika eneo la Kitanda, nje kidogo ya Mji wa Tunduru irejeshwe na kuboresha kwa kuondoa changamoto zilizosababisha kambi hiyo kufungwa siku za nyuma.