Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Jeshi kutumika kisiasa, wakati wa uzinduzi wa Makao/ Ofisi za Serikali Dodoma Mkuu wa Majeshi alinukuliwa akisema kuwa Jeshi linafuatilia kauli tata zinazoashirika uvunjifu wa amani. Sio kazi ya Jeshi la Polisi kushughulikia au kupeleleza kauli tata za kuashiria uvunjifu wa amani, ni vyema Jeshi likafanya kazi yake ya kulinda mipaka ya nchi na sio kuingilia Wizara ya Mambo ya Ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uimarishaji mipaka ya nchi, Jeshi la Ulinzi lipo lakini idadi ya wahamiaji haramu kupitia njia ya panya katika mipaka ya nchi jirani yanaogezeka siku hadi siku, kwa nini hatua zaidi zisichukuliwe na hii imebainika hasa kwenye mapango ya Tanga?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya mipaka kati ya wananchi na Jeshi la Ulinzi, ipo migogoro mingi kama Pangawe, Kizuka, Mzinga na Kilombero ambayo imesababisha hata mauaji kwa askari na wananchi, iko haja mipaka ya Jeshi ikahakikiwa upya kwa kuwashirikisha wananchi waliopo kwenye maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, fidia kwa askari wanaopoteza maisha wakiwa kwenye vita nchi za nje ikilinganishwa na nchi zingine za Afrika Mashariki ni ndogo na zinalalamikiwa na ndugu, pia ipo shida ya urasimu katika kulipa fidia za wajane waliopoteza waume zao wakati wa vita.