Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze kuipongeza Wizara kwa kazi nzuri sana wanayoifanya ya ulinzi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu kwa Wizara ni kwamba watengeneze products nzuri sana na kutoa services ambayo kama itafanyiwa marketing ya kutosha itaongeza kipato kwa Jeshi letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kumekuwa na vijana wengi wanaomaliza shule na kubaki wakizagaa mtaani. Jeshi lingewachukua na kuwapatia ujuzi ili wanaporudi mitaani kwanza wawe wakakamavu, nidhamu na ujuzi wa kuweza kujiajiri. Lakini wakati huo huo Jeshi linakuwa na akiba ya kutosha yanapotokea matukio kama vita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine maslahi ya wanajeshi yazingatiwe sana ili kujenga uaminifu na kujiepusha na matukio yasiyofaa. Lakini pia wapewe motisha ya kuwafanya wafanye kazi kwa furaha maana kazi yao ya risk sana kwa maisha yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia wanajeshi wangekuwa wanakatiwa bima ya maisha maana tayari wameyatoa maisha yao kwa ajili ya Taifa. Wakati wowote wapo katika risk ya kupoteza maisha na wengi wanategemewa na siyo kupoteza maisha tu, hata ulemavu wa kudumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kitendo cha kuwazuia wanajeshi wapya wasioe mpaka baada ya muda fulani sioni kama ni busara, na pia kunachochea maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI na msongo wa mawazo kwa wanajeshi wetu, kitu ambacho ni hatari sana kwa watu wanaohusika na ulinzi wa nchi yetu.