Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimekuwa nikikumbusha mara nyingi sana hapa Bungeni kwa njia ya maandishi na kuhutubia kwa mdomo suala la migogoro ya mipaka kati ya Kambi ya Jeshi ya JKT iliyopo Itaka, Mbozi na wananchi wanaozunguka maeneo ya Jeshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vilivyoathirika na mgogoro huu ni Itewe, Sasenga na Mboje, zaidi ya kaya 800 zimeathirika kwa kuwa wameambiwa waache maeneo yao ambayo wamekuwa wakiyatumia tangu uhuru. GN na ramani zote zinaonesha kwamba wananchi wa vijiji nilivyovitaja awali kwamba maeneo hayo ni mali yao. Naomba Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na JKT ashughulikie jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.