Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, bajeti ndogo; kwa mwaka wa fedha 2018/2019 Serikali ilitenga fedha za maendeleo katika Fungu 38 - Ngome kiasi cha shilingi bilioni nane tofauti na shilingi bilioni mbili kwa mwaka wa fedha 2019/2020 ambapo kwa bajeti hii imetengewa shilingi bilioni sita kama nilivyoeleza hapo juu ni pungufu ya shilingi bilioni mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa Jeshi la Kujenga Taifa, Fungu 39 fedha za maendeleo iliyokuwa imetengwa ni shilingi bilioni sita na iliyotolewa ilikuwa shilingi bilioni tano sawa na asilimia 83.33.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kutotekeleza bajeti ya maendeleo ya Wizara hii siyo tu kunafedhehesha Jeshi letu la Wananchi wa Tanzania (JKT) lakini pia kunawaweka wananchi katika hali ya hatari kubwa. Hili nalisema hivi kwa kuwa yanapotokea matukio ya ghafla ya uharibifu hata wanaopelekwa kwa ajili ya kuweza kutoa msaada wa haraka ni Jeshi la Kujenga Taifa. Mfano, kufanya huduma za ujenzi mara tu yatokeapo majanga kama mafuriko yanapoharibu miundombinu kama vile madaraja, majengo ya Serikali kuharibika, ni hawa hawa wanajeshi ndiyo wanaitwa kwa haraka kufanya matengenezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitendo cha kutopandisha vyeo Maofisa wa Jeshi kwa wakati kuna athari za moja kwa moja ikiwa ni pamoja na katika mishahara yao na pia katika pension zao, kwa hiyo askari aliyetakiwa kupandishwa cheo miaka miwili iliyopita halafu akaachwa akaja kupandishwa miaka miwili baadae atakuwa amepunjwa nyongeza yake ya mshahara ambapo ingetokana na cheo hicho na pia mapunjo hayo yanakwenda kuathiri pension za askari hao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo napendekeza Serikali ilieleze Bunge hili kama tatizo gani linasababisha wanajeshi wasipandishwe vyeo kwa wakati na kama ni bajeti finyu? Je, Serikali ina mkakati gani wa ziada wa askari hawa wanaotumikia nchi kwa moyo huku mahitaji yao yanapotekelezwa kwa wakati?